Msaada: Shule nzuri ya sekondari-Arusha na Kilimanjaro

Msaada: Shule nzuri ya sekondari-Arusha na Kilimanjaro

Twilumba

Platinum Member
Joined
Dec 5, 2010
Posts
13,476
Reaction score
16,188
Habari zenu wakuu,
Mara nyingi naamini hapa JF ni jukwaa kuu lenye kuweza kusaidia kimawazo baadhi ya mambo.
Kwa minajiri hiyo ninaomba mwenye kujua shule nzuri za sekondari ya wavulana au mchanganyiko za bweni zilizo mikoa ya Arusha au Kilimanjaro.

Uzuri ninaozungumzia ni kitaaluma na malezi lkn pia ada isiwe kubwaaaaa kama yale mashule mengine.

Naomba kuwasilisha kwa ushauri na msaada kwenye hili.

Asanteni.
 
Kirinjiko islamic seminary. Ipo Same Kilimanjaro. For me it is the best school.
 
Elimo Secondary School iliyoko njiapanda ya Himo kuelekea Himo na Marangu ni bora sana. Ufundishaji ni mzuri, Mandhari, chakula na nidhamu. Pia ada ni nafuu. Chini ya 2m mtoto anapata elimu. Bora.
IMG-20180903-WA0047.jpeg
 
Maua seminary
St James seminary
Zote ziko moshi.
 
Una contact zao kiongozi?
Hizo brodher, kama huudhurii jumuia sahau, kama hujafunga ndoa ya kikatoloki sahau, kama kwenye ukoo wenu kuna mtu aliwahi kugengeuka kwa kubadilisha dini sahau, kama mwanao alikuwa hatumikii kanisani na kujiunga na vyama vya utume kuanzia utoto mytakatifu hadi wito sahau. Kama vigezo unatimiza anzia maombi jumuia ya mtaani kwako then parokiani na mwisho utume shuleni
 
Hizo brodher, kama huudhurii jumuia sahau, kama hujafunga ndoa ya kikatoloki sahau, kama kwenye ukoo wenu kuna mtu aliwahi kugengeuka kwa kubadilisha dini sahau, kama mwanao alikuwa hatumikii kanisani na kujiunga na vyama vya utume kuanzia utoto mytakatifu hadi wito sahau. Kama vigezo unatimiza anzia maombi jumuia ya mtaani kwako then parokiani na mwisho utume shuleni
Kuna vitu umeongezea sana waswahili wanasema "umetia chumvi nyingi mnoo"
Kuhusu ndoa ni kweli,kuhudhuria jumuiya na kanisani ni kweli ndiyo vingine si lazima.
 
Shule bora ni za Catholic tuu....

Hapa nita exclude Catholic Seminary...Maana hizo masharti yake ni strictly kidogo...

Hapa nitakupa list ya Catholic Managed Schools za Klm....japo ni nyingi maana kwa Moshi pekee Kanisa lina Shule zaidi ya 50...

St Mary Goret
Kibosho Girls
Anwarite Girls
Visitation Girls
St Amedeus
Bendel Memorial
Magnificat
St Eugene
Kandoto Science Girls
St Joachim
......and many moreee....


Arusha

Tengeru Boys(Holy Ghost Fathers spiritans)
St Carlos
Precious Bblood
Henry Gorgaty
Star Sec Schhol
St Theresia of Child Jesus
St Joseph
Notre Dame
St Monica

Nk nk nk
 
Kuna vitu umeongezea sana waswahili wanasema "umetia chumvi nyingi mnoo"
Kuhusu ndoa ni kweli,kuhudhuria jumuiya na kanisani ni kweli ndiyo vingine si lazima.
Brother, sisi ni wahenga, hiyo ndio misingi ya kanisa na sisi ndio ma conservative wenyewe, kama kuna waliobadilisha ni makosa, kuna mengine mengi sijasema kama kwenye ukoo kuna asili ya maginjwa ya kurithi na yenyewe unapigwa panga, ma intelijensia walikuwa wanattumwa kuchunguza mpaka maisha ya familia yenu ndio ukubaliwe. Kwa sasa wanazingatia zaidi vigezo vya kufauli mtihani na ndio maana kanisa limefika hapa lilipo
 
Sio kweli mbona kuna zingine wanasoma hadi waislamu na dini zingine pia, cha msingi ni kufuata masharti yaliyowekwa mf Huruma girls seminary ipo jimbo kuu katoliki dodoma
 
Brother, sisi ni wahenga, hiyo ndio misingi ya kanisa na sisi ndio ma conservative wenyewe, kama kuna waliobadilisha ni makosa, kuna mengine mengi sijasema kama kwenye ukoo kuna asili ya maginjwa ya kurithi na yenyewe unapigwa panga, ma intelijensia walikuwa wanattumwa kuchunguza mpaka maisha ya familia yenu ndio ukubaliwe. Kwa sasa wanazingatia zaidi vigezo vya kufauli mtihani na ndio maana kanisa limefika hapa lilipo
Nna mtu wa karibu sana amemaliza maua seminary 2014 so nafahamu sana tu mkuu.
 
Back
Top Bottom