Msaada: PC yangu inaonesha hivi

Msaada: PC yangu inaonesha hivi

Joined
Oct 10, 2022
Posts
26
Reaction score
22
Pc yangu inaonesha hivi, shida ni nini?
IMG-20230301-WA0000.jpg
 
Na mimi yamenikuta
Soma chini nitaweka tatizo
imecrack kioo
Kioo hakijacrak
Hapana shida ni BIOS
Shida sio BIOS shida ni kuwa pale unapowasha pc yako BIOS inafanta power on self check(POST) ili kuangalia kama vifaa vinafuction kama ram,cpu na hdd hapo imegundua kwamba Hard disk yako either haiwezi kusoma/read data hii inaweza tokana na labda umedondosha pc yako na imecorapt chansingi nenda kwa fundi ajaribu kuicheki hiyo harddisk au ununue mpya
 
Tatizo la harddisk imecheza ama imekufa jaribu kuitoa hdd uirudishe huku unahakikisha imekaza.
Hapo haijacheza HDD inasoma ila imefikia O% HEARTH
so imekuwa Smart kutokana na kuwa BAD SECTOR nyingi ambazo zimeishusha LIFE TIME YA HDD
Smart HDD inafanya kazi ila inakuwa risk kubwa kuendelea kutumia mda wowote Inaweza kufa ghlafa na kupotexa data zako zote
SOLUTION ni kubadiri HDD nyingine kbla hiyo haijakufa GHAFRA bin VUU
 
HDD = Hard Disk Drive ndio kihifadhio cha data zote zinazotumiwa na system yako na zinazotumiwa na wewe mwenyewe.

HDD imeundwa kwa kuunganisha vi sectors vingi vya kuhifadhia data kuwa kitu kimoja. Kila ki sector kimoja kina weza kutunza kiasi flani cha data. Na kila ki sector kimoja kinaweza kufa kivyake na vingine vikabaki kuwa vizima na kuendelea kuhifadhi data.

Kila ki sector kimoja kina anyani yake inayokitambulisha kipo wapi kimepakana na ki sector gani kingine na kimehifadhi nini na kina ubora gani. System iki wasiliana na ki sector flani ikagundua hakina afya njema inakipotezea na kutafuta ki sector kingine. Pia sysyem ikiona data muhimu kwa kuendesha mashine zipo kwenye vi sector vilivyochoka inahamisha hizo data na kuziweka kwenye ki sector chenye afya zaidi.

Ki sector kinaweza kufa kwa mambo manne:
1. Kimepata mkwaruzo ama mtikisiko (head inayosoma data inaweza kwaruza uso wa disk mathalan. Ama unaweza angusha pc ikasababisha hilo pia.
2. Kimezeeka
3. Kimepigwa shoti na umeme wa gafla
4. Kimejaa vumbi

Vi sectors vinaendelea kufa na kubaki vilivyo hai na system inaruka vilivyokufa inatumia vilivyohai kuhifadhi data.

Vikifa vi sectors vingi sana basi system inakupa onyo ili uchukue hatua. Ukiendelea kukaza shingo basi utakula hasara.

Hatua sahihi ni kununua HDD mpya na kuifunga kwenye mashine. So kwasasa tafuta external hamisha data zako za muhimu na uendelee kukomaza shingo siku ikifa unachukua disk ingine unafunga. Ila ujue disk ikifa inakufa na softwares zako ulizo install zote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom