Msaada: Nyani wanakula kuku wangu

Mimi shambani kwangu nafuga kuku na nalima matikiti na jirani yangu analima mpunga , kuna nyani wanakuja wanaanza na mpunga (wali) then wanakuja kwenye kuku alafu wanamalizia na kuyala matikiti. ..yaani full menu ya hotel na nimewapiga na bunduki baada ya siku 3 wanarudi tena kupiga menu yao... dawa kuwatega na wao kuwala tu.
 
Hakuna kitu kingne kinachozuru kuku zaid ya nyani hapa nilipo hao mbwa wanapigwa makofi mpaka basi! Labda ufuge elf 20
Hahaha,aisee hii nimecheka mpaka basi,duhhhhh
Nyani wakiwa wengi aisee watemi kweli,duhhh
Hahaha
tatizo la Nyani ukiwategea Umeme,basi wakijua unapiga shoti basi wanahamisha nyaya wanakuwekea na wewe uone cha moto
Hahahaha,Nimewaona sana Mkuranga hao jamaa
Na nguruwe Pori
 
tafuta mbwa wenye nguvu kama German Shepherd na uwalishe fresh. siyo kuwalisha mihogo na matikiti.
 
tengeneza banda imara ufugie huko
 
Kafungue kesi ya madai TANAPA. But make sure hujaingilia eneo la hifadhi maana wale wakija watafyeka kila kitu.
 
Jamani mm ninakofugia kuna nyani kuku wangu wanaliwa sana nifanyeje????
Pole, sasa dawa iko namna hii, kama utaweza kumtega ukamkamata akiwa hai utafanikiwa, ukimpata tu unavalisha kengere zile za kuchezea ngoma ya kienyeji, halafu unamuachia aende zake, sasa ile kengere itakuwa inalia akiwa anakimbia na kurukia miti, sasa nyani wenzake watamkimbia yeye mwenyewe kengere, hapo itasababisha wakimbie umbali mrefu Sana, kwani wao hutembea kundi kubwa. Kwa kifupi watakuwa wamehama eneo hilo. Tuliwahi kufanya hivyo tabora kwenye shamba la mahindi wakahama jumla.
 
wapi huko mkuu?
 
Kupambana na nyani sio kazi rahisi kwa sababu wana akili kama binadamu kwa hiyo majibu rahisi hayawezi kufanya kazi. Nakumbuka miaka ya nyuma kule Uganda kaskazini kuna mkulima mmoja ambaye alilima nahindi na nyani wakuwa wanakula kila siku. Siku moja aliweka ulinzi akiwa na upinde na mishale. Nyani wakaja kama kawaida yao wakaingia shambani kula mahindi yeye akiwa amejificha sehemu tayari kwa mashambulizi. Basi akavuta upinde na kurusha mshale uliompata barabara nyani mmoja na kumuua.
Wenzake walikimbia kisha baadaye wakarudi kubeba nwili wa "marehemu" na kwenda nao wanakojua wao "kwa ajii ya mazishi". Walikuwa wakiomboleza kama watu.
Basi hao nyani wenye hasira walimjua huyo mkulima na nyumbani kwake walipajua! Chezea nyani weweeee! Wakaitisha kikao cha dharura kutafakari hatua gani wachukue dhidi ya huyo mkulima. Cha ajabu pamoja na hasira walizokuwa nazo walisubiri muda muafaka wa kulipiza kisasi. Bila kukosea walikuja nyani kama 30 hivi usiku wa manane nyumbani kwa huyo mkulima wajavunja mlango na kuingia ndani. Walimtoa kitandani mzega mzega hadi nje wakamchana tumbo na kutoa utumbo nje! Walipohakikisha amekufa wakaondoka zao. Sasa ona kwamba walijua kuwa usiku mnene hangepata msaada wa majirani kwa hiyo wakachagua muda huo kufanya mashambulizi!
Mimi ninachoshauri ni kubadilisha mazao na kupanda vitu ambavyo nyani hawana shida navyo.
 
If U want to catch a monkey, U should learn how to jump like a monkey!
 
hii kali
 
hao hawawezi kuwa nyan wa kawaida wakutumwa hao
 
Anza kuwala wao sasa...kamata,chinja,unaweza kuchoma au kupika mchuzi!!ukipata jike nadhani ndo watamu zaidi
 
!
!
Tafuta sumu weka wakafiage mbele huko... Yena wape ile ya Panya ya kukausha ile ndio hatariiiii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…