Ndio ukweli, kuna mwaka flani nikiwa kwenye 33, nilikopa fedha benki kupiga dili moja na kampuni yangu. Ile dili badae wanasiasa wakaizima "abruptly" 😪
Nikajikuta kwenye madeni, miradi imesimama, pesa yote ipo kwenye miradi ile. Nilikonda nikabaki kichwa ndani ya miezi minne tuu. Nikakosa usingizi, moyo wangu ukawa na hofu kubwa sana, kila nikikaa likija wazo la miradi na fedha moyo unashituka sio kidogo. Nikaona wazi nitakufa.
Nikaamuru nifunge kwanza uendeshaji kupunguza gharama, nikafunga miradi ile nikaacha walinzi tuu kwenye miradi, wafanyakazi wote nikasimamisha. Nikarudi kwa Dingi mkoani, Dingi aliponiona akanambia, mwanangu una hatari ya kupata ugonjwa wowote wa moyo, au presha, shambulio la moyo, hali hii ikiendelea. Kweli, baada ya wiki usiku nilianza kuona kifua kinanibana, nakosa nguvu na kichwa kinaninuma sana. Usiku nashituka na moyo unaenda mbio sana, ikitokea hali hiyo jasho linakuwa jingi na napumua kwa kasi sana. Kwenda kupima nikaambia nina presha. Daktari alienipima kitu cha kwanza aliniuliza kuna mambo gani yanakusumbua? Nikamwelekeza, akanambia ndio yanakusasabishia hali hii. Sasa jitahidi kujiondoa kwenye msongo wa mawazo na mshtuko, stress na sonona. Hakunioa dawa kwanza, alinishauri nione namna ya kuomba msaada kwenye eneo la uendeshaji wa mambo yangu yale.
Nilongea na Mshua akanambia, itisha kikao cha bodi, muachie majukumu mdogo wako. Na ishu ya madeni ya benki, ikabidi tuuze mali flani kuizima. Mshua akasema tafuta sehemu nenda mbali, ukapumzike. Nikachagua kwenda sehemu na kule nikaendelea na ushauri wa daktari.
Mambo sijui ya kuitwa na Benki, Simu ukiwasha ni calls, sms za madeni, ukiona simu inaingia unastuka, sijui nani anakudai, hujalipa watu mishahara, sijui suppliers wanataka kuchukua mali zao, yakapungua na kuisha kabisa.
Baada ya miezi sita, nikarudi kwenye uendeshaji wa biashara. Na presha kwisha.
Toka hapo, nikajifunzaga kuipa thamani afya hasa ya moyo, nafanya mazoezi ever since, kitambi hakijawahi nirudia toka pale. Nikapunguza na bia pia. Japo ni ngumu ila najitahidi sana nikimbie kwa siku hata nusu saa tuu.
Bado nipo fresh na nipo kwenye late 30's. Presha ni ugonjwa wa kitu flani, au moyo kuelemewa na uzito wa kupindukia, au jambo flani kukukumba la kufanya moyo wako uelemewe, mawazo, sonona, hofu moyoni, kukata tamaa. Ni humo tuu ndo kuna leta presha hasa katika umri mdogo 30's au 40's.