Msaada: Nimekuwa na uraibu na mtandao

Msaada: Nimekuwa na uraibu na mtandao

BUMIJA

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2011
Posts
6,182
Reaction score
11,782
Muda mwingi napenda kuwa online kama nipo free. Usiku nakesha mitandaoni, naamka nimechoka sana, huu uraibu unanitesa.

Yaani nikikosa kuingia sina raha. Imekua zaidi ya ulevi sasa. Sijui nifanyeje nipunguze hii addiction wadau.
 
Muda mwingi napenda kuwa online kama nipo free. Usiku nakesha mitandaoni, naamka nimechoka sana, huu uraibu unanitesa.

Yaani nikikosa kuingia sina raha. Imekua zaidi ya ulevi sasa. Sijui nifanyeje nipunguze hii addiction wadau.
Nilikua kama wewe mwezi wa nane mwaka jana nikauza simu zote nikanunua kitochi, siku ya kwanza nilitabika sana mpk nikatamani niende dukan kununua simu nikavumilia, mala ikapita week, mwezi na miezi nimekaa bila smartphone kwa miezi 6 , sasahivi nimeweza kubalance matumizi yangu.
 
A6340DC3-E194-4AB0-BF60-EAD2BB02EC2C.jpeg
 
Maamuzi ya kupunguza/kuacha kabisa huo uraibu, yako mikononi mwako. Hakuna atakayeweza kukutoa huko, kama wewe mwenyewe hautokuwa tayari kuacha.
 
Maisha mafupi haya Mzee . Kwanini ujibane bane, kula maisha .

Kama ipo , ipo tu na kama hakuna , hakuna
 
Unaongelea mtandao gani?
Kama Ni Tigo, nikupe pole Sana mkuu
 
Jaribu kufanya vitu vingine ili upate balance ya mambo mengi. Jitahidi hata kusoma biblia.
 
Smartphone kwa dunia ya sasa ni muhimu sana haina tofauti na computer.Kuikosa kwa kweli ni sawa na kuishi maisha ya ujima.
Inategemea unatumia mtandao wako kwa vitu gani kama ni kwa ajili ya kupiga tu majungu yasiyo na faida haina maana kwako
Kumbuka simu hiyo unaweza ongea na mtu ukiwa unamuona akakuelekeza kitu ukiwa kazini.Simu hii hii unaweza kutuma email ya kikazi.Unaweza hata kuomba kazi online kwa kutumia simu.Unaweza apply chuo ukapata kama alivyofanya binti yangu ukapata.Unaweza ukakata ticket ya ndege ukiwa kijijini kwenu Kwamsisi ukaenda kupanda ndege KIA na ukijipangia siti ya kukaa hapo hapo kwenye ndege,Unaweza lipia bili ya maji kwa simu,kwa kutumia simu yako unaweza ukawa umesahau kitambulisho chako au kadi ya benki ukatumie QR code ukaiona,unaweza save ticket ya ndege ukaiona kwenye simu yako usitembee na makaratasi.
Unaweza kufanya confrence na kikundi kingine hata mambo ya kikazi
kwa kifupi smart ukiitumia vizuri ni shule tosha sana
Kama unaitumia ku bet na kuangalia ni celebrity gani wamemsema au Diamond na msichana wake mpya wameaachana au vipi inakuwa haina faida kabisa ni bora kuacha
by the way mtoa mada una elimu gani kwanza
ungekuwa umefika chuo kikuu usingetoa hii kitu kwenye mkeka hapa
 
Nina tatizo kama lako weka applications hizi zifuatazo zikusaidie kufunga simu na hizo social media muda wa kulala
1.detox ya phone addiction hii usiku inafunga simu nzima muda ukifika ulipanga

2 app blocker.... hii inafunga baadhi ya app mida ya mchana
 
Nina tatizo kama lako weka applications hizi zifuatazo zikusaidie kufunga simu na hizo social media muda wa kulala
1.detox ya phone addiction hii usiku inafunga simu nzima muda ukifika ulipanga

2 app blocker.... hii inafunga baadhi ya app mida ya mchana
Zipo play store?
 
Muda mwingi napenda kuwa online kama nipo free. Usiku nakesha mitandaoni, naamka nimechoka sana, huu uraibu unanitesa.

Yaani nikikosa kuingia sina raha. Imekua zaidi ya ulevi sasa. Sijui nifanyeje nipunguze hii addiction wadau.
Mkuu yote ni kwa sababu una smartphone, kosa smartphone uone km utakua addicted
 
Muda mwingi napenda kuwa online kama nipo free. Usiku nakesha mitandaoni, naamka nimechoka sana, huu uraibu unanitesa.

Yaani nikikosa kuingia sina raha. Imekua zaidi ya ulevi sasa. Sijui nifanyeje nipunguze hii addiction wadau.
Tafutaaa hela,ukifanya hivyo uraibu unakutupa ✋ mkono,kama sio kukata roho😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom