Msaada: NIDA yangu imefungiwa

Msaada: NIDA yangu imefungiwa

Habari. Jana nilikuwa nataka kusajiri line mpya ila imenigomea naambiwa namba ya NIDA imezuiliwa naomba msaada kwa mwenye uzoefu nifanye ili nida yangu ifunguliwe. Na ni mitandao miwili tu niliyosajiria nida yangu VODA NA AIRTEL
Acha kuitumia kwa kuwasajilia wengine, huo ni uhalifu japo wewe unaona ni ujanja! Usije tena huku kutuomba ushauri ili uendeleze uhalifu.
 
Nimekwenda sehemu wanaposajiri line, nilitaka kusajiri line ya halotel mhusika baada ya kuanza process mhusika akaniambia namba yangu ya nida imefungiwa hivyo siwezi sajiri line mpya
Wewe ndo wale wa tuma kwa hii namba, polisi wangekuwa karibu wangekukamata.
 
Huyu ajafungiwa NIDA, ila ameshindwa kutoa maelezo sahihi ya kilichomkuta.

Nimehisi, Namba zake za NiDA zimefikia kiwango cha mwisho cha kusajili line kwa ajili ya matumizi ya simu, inaonekana anasajili line zake vichochoroni au kwa vijana wapita barabarani.

Hivyo, wakatumia NIDA namba zake kusajili watu asio wajue.

Abonyeze *106# kuhakikisha je, namba zilizosajiliwa na NIDA yake ni hizo anazotumia au kuna ambazo hazijui, kama zipo azifute mwwnyewe, walizonazo zitakoma matumizi.

Akishindwa afike kwenye mitandao husika ya hizo namba ambazo hazitambui, wamsaidie kuziondoa.

Asante
Hivi karibuni TCRA kuna faini walitoza kampuni za mawasiliano, baadhi ya makosa ni kampuni kutumia kitambulisho kimoja kusajili zaidi ya idadi ya namba 5. Hii inaweza kuwa sababu ya tatizo halilopata huyu mdau.
 
Kama namba yako ya Nida imehusika kusajili line iliyohusika katika uhalifu wa aina yoyote polisi hufungia namba hiyo ya NIDA,so kumbuka vizuri kama hujawahi husika na maghumashi yoyote
 
Nenda ofisi za Vodacom watakufungulia.
NB: NIDA watakurudisha hukohuko Vodacom.
Shukran sana mkuu, hii imenisaidia, nimeenda ofisi za Vodacom wamewasiliana na NIDA kujua tatizo nini, then wameifungua now ipo fresh. Ubarikiwe sana
Nenda ofisi za Vodacom watakufungulia.
NB: NIDA watakurudisha hukohuko Vodacom.
 
Shukran sana mkuu, hii imenisaidia, nimeenda ofisi za Vodacom wamewasiliana na NIDA kujua tatizo nini, then wameifungua now ipo fresh. Ubarikiwe sana
Next time kua makini... Acha kusajili laini mtaani kwa hawa mawakala njaa wanaojifanya wanasajili laini bure kumbe kuna namna wanajilipa kwa udanganyifu! Ukitaka kuongeza laini fika SHOP ya mtandao husika kabisa ndo usajili..
 
Back
Top Bottom