Mada inahusu namna ya kuanzisha kampuni ya ulinziHuu uzi umenikumbusha kitambo Sana.
Nakumbuka nilikua naogopa Sana bunduki.
Ma Askari walipo kua wamakabidhi silaha kutoka ma lindoni.
Wakati wa kuandikishiana makabidhiano ya bunduki nilikua naogopa Sana bunduki.
Badae nilikuja kuzoea mpaka leo hii Huwa siogopi mtu akiwa ameshikilia bunduki karibu yangu.
Nili enjoi Sana kuwa taasisi ya kijeshi.....pale Ni neno Moja tu.... Unaitikia......WAZI AFANDE
NILI HUSIKA SANA KWENY MAMBO MENGI KU RECRUIT, KUPANGA OFF ROSTER.
Pia Kuna kuibiwa malindoni.
Kuna kisa kimojaa kilitokea kilisisimua sanaa.
Kuna bwana mdogo mmoja royal na humble raia alikuja kuomba Kazi ya ulinzi.
Nakumbuka nilimfanyia recruitment tukamchukua huyu dogo nilizoea kumpanga Kwa RPC Mmoja lindo la Mchana pia kwa Director mmoja wa shule.
Mkasa ulianza ivi huyu dogo tulimwamisha akapelekwa kweny lindo la hardware Moja kubwa.
Ipo barabarani na Kuna full camera.
Nikiwa njian kwenda ofsn napokea simu kutoka KWA director wangu kunatukio kimetokea.
Kufika eneo la tukio hakuna palipo vunjwa kweny eneo la mbele la hardware ambalo Askari wetu alikua analinda.
Nyuma ya hardware KULIKUA na ukuta mrefu na umeunganika na ukuta wa nyumba ya familia Moja.
Nyuma ya hardware KULIKUA na mlango mmoja heavy sanaaaa.
Tunaenda kweny jicho la mwewe.
Tukiwa Na maAskari polisi....picha lina Anza.
Ilikua Usiku wa kuamkia Jumapil majira ya saa 7
Jamaa mmoja asiye juliana anaonekana anatumbukia kweny ukuta.
Alipofika chini Cha kwanza akavaa mask yake.
Camera zinaonyesha clear Ila black & white
Then anaonekana ameenda pembeni ya ukuta dakika Chache akaenda kweny ule mlango heavy akagusagusa sekunde Chache anaonekana yupo ndani.
Camera za ndani zinaonyesha akienda direct counter na kufungua fungua ma drow akaonekana akachukua kitu na kutoka haraka akipenya alipo ingilia Na ule ukuta mrefu sijui aliruka vp.
Ntaendelea jioni ngoja Ni ingie kulitumikia taifa.