Msaada namna ya kupata Driving Licence na gharama zake

Man Mvua

JF-Expert Member
Apr 12, 2016
2,184
3,517
Salaam.

Wakuu naomba Mwenye kufahamu procedures za kupata leseni ya udereva kuanzia pikipiki na private cars na gharama zake anijuze.

.......
 
Salaam.

Wakuu naomba Mwenye kufahamu procedures za kupata leseni ya udereva kuanzia pikipiki na private cars na gharama zake anijuze.

.......
Nenda chuo cha udereva kinachotambulika, Ada haizidi laki 2 halafu elfu 3 ya Lena andaa elfu 40, utakuwa umefikia kiwango cha awali cha udereva utapewa daraja "A", "B" na"D" ukitaka na E itabidi uongee na vehicle kwa herufi kubwa hiyo herufi kubwa haina risit hivyo hata kiwango hakijulikani
 
Ok, japo zipo njia za shortcut kupata lessen baadhi ya madaraja lakini gharama zake zinazidi mtu aloenda chuo hivyo inategemea na uhitaji wako
Nilikuwa nataka nianze na ile ya pikipiki hadi private cars ya chap chap lakini.
 
Salaam.

Wakuu naomba Mwenye kufahamu procedures za kupata leseni ya udereva kuanzia pikipiki na private cars na gharama zake anijuze.

.......
Nenda TRA na cheti chako cha udereva kutoka chuo kinacho tambyulowa na ser
Nilikuwa nataka nianze na ile ya pikipiki hadi private cars ya chap chap lakini.
Mkuu jiangalie kwa makininkupitia hapa hapa kwenye hitaji lako la shortcut utashtuka umesha tapeliwa fuata taratibu
 
Hizo shortcut mnazotaka kumpa kesho nisisikie lawama kua kuna dereva ame-indicate kushoto alafu kalala nayo kulia mazima maana tunaona kila siku maajabu barabarani mpaka unajiuliza uyu mwenzetu udereva kasomea wapi.
 
ukitaka kufuata procedures ni kama ifuatavyo:
1. uwe na cheti cha kuhitimu mafunzo ya udereva (mafunzo ni mwezi 1 kwa VETA ada ni 187,000/= kwa vyuo vya private bei ni juu zaidi)
2. nenda ofisi za TRA chukua TIN (kama huna), ni bure
3. toa copy cheti chako cha udereva, TIN na kitambulisho (200/=)
4. peleka TRA hivyo vitu waambie unahitaji leseni ya udereva.
5. utatozwa 53,000/==>10,000/= kwa ajili ya kukata learner, 3000/= ada ya mtihani wa majaribio (kujaribiwa kama unajua kuendesha na unajua alama za barabarani na 40,000/= ni kodi ya leseni kwa miaka 3.
6. ukimalizana na TRA unaenda kwa traffic officer kujaribiwa, hapa ndo huwa kunachelewesha, manake kumpata wa kukujaribia ni ishu, kila ukienda unazungushwa unaambiwa askari wote wako bize...
7. baada ya kujaribiwa askari atakomenti kwenye form kwamba upewe leseni umefuzu mtihani..
 
Back
Top Bottom