Kwamba hata kufuata barabara itakuwa shida mpaka aishi mtaroni? Nimemshauri aongee na bosi afanye mazoezi kwa kutumia gari ya kazi.Ndugu kuwa muelewa.. gari usipoendesha muda mrefu unaloose control.. ndio maana kazi za madereva zinataka experience.. yaani asome veta mwezi mmoja ajue kisha akae mwaka mzima bila kugusa gari.. halafu asikosee kweli?
Hii imenifanya nicheke, kwa hiyo madereva wanaenda wapi na kuwaachia wachuuzi wa barabarani wajibu wa kuyasogeza magari yao?Kama una muda uwe unaenda mitaa ya Bandarini kuanzia geti namba 5 muda ya saa 10 foleni ikianza.
Jichanganye uongee na wale madogo wa kuuza karanga/sigara uwa wanaachiwa kusogeza gari za trip town zenye container empty.
Kule utapata uzoefu mzuri wa manual maana madereva wenye Mishe zao huacha gari wasogezewe, utapata kujiamini kwa kuendesha manual vigongo za Madina 2001 na Motichand.
Kweli mkuu veta tunafata cheti tu ila gari kujua ngumu sana maana practical zao ni muda mchache sanaVETA nilifanya mazoezi na mtihani pia nimefanya ila unapokuja suala la control barabarani kwa aliyepitia hapo VETA ataniunga mkono,
Kwa sheria na alama za barabarani nipo vizuri sana tena sana, na ndio kipaumbele chuoni.
Pia ahsante kwa ushauri wako mzuri nitaufanyiakazi mungu akubariki
Hapana mkuu, nishafanya kazi nyingi sana kulingana na elimu yangu na pia sijawahi kuogopa kuacha kazi kikubwa ni maslahi gani napata kulingana na kazi nnayofanya.Gari ushajua Ila tatizo nikama ilivyoanza KUSEMA umetokea familia maskini, ndiyo kinachokunyima Amani bado minyororo ya UMASKINI wa familia imekuzonga. Kuna watu hawaendelei kwa kwakuwa hawaamini Wanachokifanya. Usikute hata kuacha huo ulinzi UNAOGOPA. Kuukata UMASKINI NI sawa na kujitoa kwenye unyororo. Unahitaji pia moyo wa kijasiri.
😂😂Yaani kamanda gari la boss wa masaki hutaki kulitia mtaroni ila langu la kukufundishia unataka kulitia mtaroni
Huko veta hamkufanya Practically
Hii hata mimi ningekuwa boss nisingekubali.Kwamba hata kufuata barabara itakuwa shida mpaka aishi mtaroni? Nimemshauri aongee na bosi afanye mazoezi kwa kutumia gari ya kazi.
Mkuu,boss wako usimwambie ukweli kuwa huna uzoefu.Nitafanya hivyo mkuu
Ubarikiwe na mungu akuzidishie palipo punguaNimekuonea huruma. Kama bado hujapata mtu. Nicheki nikupe namba za mwamba bosi wa garage. Atakufundisha bure tena hata kwa gari manual. Mchawi itakua kuweka mafuta. Tena yupo Kigamboni hukohuko.
Unashangaa nini mkuu? sasa kuanzia asubuhi hadi jioni gari yenyewe jiniHeeeee!
Sawa mkuu..gari gan hiyo kwanza!Unashangaa nini mkuu? sasa kuanzia asubuhi hadi jioni gari yenyewe jini
Kiluvya kwa KombaUnapatikana wapi mkuu utakuwa umenisaidia sana
GRANDE INJINI YA 1-JZSawa mkuu..gari gan hiyo kwanza!
Hapo sawaGRANDE INJINI YA 1-JZ
Kwa hiyo VETA wanawapa watu Vyeti na Leseni bila uwezo wa kuendesha gari? Ina maana vijana wetu wanapoteza pesa bure kusoma VETA.Habari Wakuu,
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 30 elimu yangu ni form IV natokea kwenye familia ya kimaskini iliyopo Kigamboni jijini Dar.
Kutokana na changamoto na ugumu wa maisha nikaamua kujiunga na kazi ya ulinzi (nimepitia kazi nyingi za msoto).
Hivyo kutokana na changamoto nikaona nisave kipato changu ili angalau niwe na fani yoyote, nashukuru mungu nilifanikiwa kusave nikaenda VETA kusomea udereva (basic driving course) na nikafanikiwa kupata cheti na leseni.
Sasa hapa lindoni kwangu ninapolinda (nalinda nyumba ya mtu binafsi masaki) huyu boss nimejaribu kumwelezea changamoto za maisha ninayopitia alichoniambia kama naweza kuendesha gari nimpelekee cheti na leseni yangu, hivyo vyote nnavyo tatizo sina experience/control hasa vurugu za barabarani naogopa kulitia mtaroni gari la watu nikapata lawama zaidi.
Mwenye nia na uwezo wa kunisaidia niweze kupata uzoefu naomba anisaidie.
Kuhusu pesa ya mafuta nitakuwa nachangia kadri jinsi tutakavyokubaliana.
Naombeni msaada wenu please.
Ahsanteni