Msaada: Mwanangu kameza bolt, nimsaidieje?

Msaada: Mwanangu kameza bolt, nimsaidieje?

uko sawa kabisaaa mkuu jf iwe hatua ya mwisho kwenye kutatua tatizo na sio hatua ya kwanza... miaka ijayo utashangaa mtu anaomba ushauri ndugu yake anakaribia kukata roho so afanyaje

unadhani watu wote tunaishi mjini? Bolt imeshafika tumboni, si kila kitu upanic, unawezakimbilia kupasua tumbo wakati hiyo ni hatua ya mwisho
 
uko sawa kabisaaa mkuu jf iwe hatua ya mwisho kwenye kutatua tatizo na sio hatua ya kwanza... miaka ijayo utashangaa mtu anaomba ushauri ndugu yake anakaribia kukata roho so afanyaje
kweli kbsa mkuu.na katika hili,Endapo akajaribu kufata ushauri wa watu wengine humu bac ataua mtoto.mtu unawahi kwanza hospital upate ushauri wa daktari ndo mengine yafate.ila humu ndani kuna majb mengine ukisoma unaweza kuzimia kwa kucheka mkuu.duh
 
SAUTI YAKO hivi mtu anaweza akawa katika hatari ya afya halafu una log in JF kupata ushauri? Tanzania huduma za afya zimesambaa kila kona... Ni ujinga ikiwa umepata shida inayohitaji mahitaji ya dharula, halafu wewe waingia mtandaoni kuuliza maswali...

mkuu jf ina wataalamu mbalimbali hadi madokta nadhan mleta mada alihitaji kujiridhisha kwa msaada zaidi ya mawazo hata kama alienda hospitali.
 
Last edited by a moderator:
Mwanangu wa miaka mitatu amemeza kabolt kadogo, nimejaribu kumshindilia ugali ili ajisaidie bila mafanikio. Msaada wapendwa kabla sijampeleka hospitali kesho.

Usihofu ndugu!kuwa mtulivu hakikusha unakagua choo chake kila anapojisaidia huchukua siku 5-7 kutoka.wa kwangu alimeza sarafu ila ilishatoka na anaendelea vyema.nilimpeleka hospitali kupiga picha ya xray kujua kama ilishafika tumboni kilichofuata kila siku nakagua choo chake mpaka nikaipata.
 
jamaa kaomba ushauri sema watu wa hapa hajamjibu vizur na anajua hapa ndo hom pa ma great thinker ss mtu anasema mpe spana pamevamiwa hapa hamna kitu.

Mkuu don't take Jf that much serious. Huu ni mtandao na kuna watu wa kila aina na wenye utaalamu na mitazamo tofauti. Humu kuna mazuri na mabaya, hivyo chukua yanayokufaa mengine achana nayo. Niliposoma post ya 'mpe spana au grisi' nusura nipaliwe kwa kucheka. Ni kweli kuna mtu ana tatizo lakini mwingine anaamua kuchekesha. Hiyo ndo mtandao.
 
Mwanangu wa miaka mitatu amemeza kabolt kadogo, nimejaribu kumshindilia ugali ili ajisaidie bila mafanikio. Msaada wapendwa kabla sijampeleka hospitali kesho.

kama upo karibu na kituo chenye huduma ya xray, mpeleke akapigwe xray kubaini bolt ipo sehemu gani, halafu kesho usipoipata kwenye kinyesi mrudishe kufanya control xray kubaini kama inashuka au imekwama. Kama imekwama inawezekana akahitajika kutolewa kwa njia zingine za kitaalamu. Ila sio dharura kihivyo.
 
Acha umaku ---- ww unaushauri mmbaya hvyo kwenye matatizo ya wengine,ebu kuwa japo kidogo.

Wewe ndo uache umaku!!mtoto kapata tatizo unakimbilia kuandika thread humu,hiyo nguvu unaipata wapi,ulitakiwa uwe hospitali,sio humu,kitimoto we!
 
Vipi mtoa mada mtoto anaendeleaje? Hope ilitoka
 
Back
Top Bottom