Msaada: Mwanangu kameza bolt, nimsaidieje?

Msaada: Mwanangu kameza bolt, nimsaidieje?

sirluta

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2012
Posts
6,324
Reaction score
2,494
Mwanangu wa miaka mitatu amemeza kabolt kadogo, nimejaribu kumshindilia ugali ili ajisaidie bila mafanikio. Msaada wapendwa kabla sijampeleka hospitali kesho.
 
Acha atainya ila kwa huduma ya kwanza huwa wanapewa maji ili kuona kama hiko kooni au vp, kama imeshapita kooni bas huwa wanakuambia ataitoa kwa haja kubwa ila chakuzingatia tu kuwa asijisaidie choon awe anajisaidia chin na akimaliza bas kagua kile kinyesi kwa makin mpk siku atakapoitoa
 
sa utampaje ugali halafu ajisaidie ghafla? mpee msos laini mwingi na matunda kama vile papai, parachichi akishiba haina noma. asubuhi ataitoa apende aspende.
 
Usiwe na wasiwasi mtoto wa jirani yangu yeye alimeza sh 100 lakini ilipitia haja kubwa hivyo nakushauri mnunulie pot awe anajisaidia humo kazi yako ni kukagua zikipita siku 4 haijatoka muone daktari japo naamini ndani ya siku tatu utatupa hapa majibu mazuri
 
Aaaah 2 tu atainya hyo wala usiwe na wasiwasi na ye mtoa wasi2 pia bse hofu hutengeneza tatizo jingine
 
Pia hakikisha unampatia lishe nzuri yenye madini ya chuma kama maini ya ngombe au maini ya kuku, nyama nyekundu, dagaa maana mtoto kupenda kulambalamba vitu vya chuma na kupelekea kumeza bolt inaweza kuwa dalili ya ukosefu wa madini ya chuma ktk lishe yake.
 
hivi jamani ishu kama hii ndo ya kuiletea utani namna hii?
 
Wewe unadhani watu wote humu wana akili timamu kama wewe...wengine ni vichaa huwa wanaiba computer za waangalizi wao na kupost upuuzi...humu..

ila jaman hata mleta mada namshangaa!! mtoto yuko kwenye hatar na hujui huko tumbo kitu kimekaaje, unakimbiia huku kwa watu ambao hawana vifaa wala hawamuoni mwanao yukoje...!

ndo maana wengine wanaonna mleta mada hayuko serious na maisha ya mwanaye!! sasa kama mwenye mtoto anawaza MMU badala ya hospital ya karibu nani atakuwa serious!!? pipo they not serious!!! mleta mada mwenyewe anatania
 
Back
Top Bottom