Msaada mtoto wangu mbegu moja imepotea

Zina tabia ya kutoroka wakati wa baridi. Ondoa shaka zitarudi
Ndio wanaita Ngiri au Kasongo hua inakua hivyo pumbu zikipigwa baridi Gololi zina kawaida ya kuingia ndani zinakimbilia tumboni halafu inauma balaa mtoto anaweza akawa hasemi ila anasikia maumivu na kulia tu sema zina kawaida ya kurudi pumbu zikishapata joto lake la kawaida
 

1: Ngiri kavu=hernia
2: Ngiri maji=busha/hydrocele.
 
Ni mtoto wangu wa kwanza tulimpeleka kituo cha afya akapatiwa dawa ila hali bado. Kwa anaejua zaid kwa mliotangulia kupata watoto kabla naomba msaada wa mawazo
Pole,
1: Kende hutengenezwa tumboni, kabla mtoto hajazaliwa hushuka sehemu yake/korodani.

2: Kuna baadhi ya wakati, njia zilipopita huwa haijafunga vyema.

3: Wakati wa baridi kende hupanda juu ili kufuata joto la mwili. Kama njia inakuwa haijafunga basi hupitiliza kurudi tumboni au sehemu ya tumbo.

4: Si vyema kuziacha kende ndani ya tumbo kwani joto likiwa kali huweza kubadili seli za kende na kupoteza uwezo wa kufanya kazi au madhara zaidi. Nfo maana joto likiongezeka kende huning'inia mbali na mwili.

5: Unachotakiwa ni kuwaona wataalamu wa afya ili kujua iko wapi na kama inaweza kushuka au la ili kuyoa usaidizi.
Maamuzi yanategemea na hali halisi. Altrasound huweza kusaidia hapa kwenye uchunguzi.

Pia kuna haja ya kujua kama haikushuka tangu alipozaliwa ambalo hili ni tofauti na hapo juu(undescended test).

Wajusishe wataalamu wa afya mapema iwezekanavyo.
 
Haziumi.. zikiuma ujue kuna shida
 
Pumbu mkuu
Sasa pumbu unaliitaje mbegu? Una uhakika wakati anazaliwa yote yalikuwa yameshuka? Kuna situation wakati wa kuumbwa huwa yanagoma kutelemka ama yote mawili (bilateral) au moja (unilateral) cryptorchidism. Katika umri wa miezi 6 yanaweza kutelemka yenyewe ila muda huo ukipita inabidi umpeleke kwa daktari pengine watashauri afanyiwe upasuaji hasa kama yamekwamia tumboni au kwenye inguinal! Bila msaada wa kuyatelemsha dogo anaweza kuja kuwa tasa pamoja na kwamba ataweza kubabua mbunye kama kawa, ila mbegu zitakuwa zinaunguzwa na joto la tumboni!
 
Atapona tu ni suala la muda mwili waa mtoto au mtu yoyote unajijenga wenyewe haujemgwi na Daktari ungekua mwili unajengwa na Daktari Papa asingekufa maana Madaktari wamehangaika wameshindwa ngoma ngumu
 
wamemroga huyo fika kwa kalumanzila alieoko karbu yako haraka sana kwa msaada zaidi.
 
mwanao ana miaka mingapa baada ya oparesheni?
 
Ni mtoto wangu wa kwanza tulimpeleka kituo cha afya akapatiwa dawa ila hali bado. Kwa anaejua zaid kwa mliotangulia kupata watoto kabla naomba msaada wa mawazo
Ana umri gani? Mpeleke hospitali inayoeleweka. Watafanya ultrasound kuangalia location ilipo, then kuna possibility ya kufanya upasuaji ishushwe na hiyo nafasi ambayo inaitumia kuascend iweze kuzibwa.

Testis haitakiwi kuwa juu, zinatakiw ziwe kwenye it's normal anatomical position chini.
 
4yrs si conclusion ya kukufanya wewe uone kuwa hiyo op. Haina madhara ama la,ni vizuri kutumia dawa za asili kuliko op. mkuu.
Unaweza kuwa sahihi sijui Sana kuhusu hili ila mbali na huyu mtoto wa brother nae alifanyiwa akiwa form 1 akiwa na miaka 13, mpaka sasa ni mtu nzima miaka 28 na tayari ana mtoto. Japo yeye walisema imeshakufa hivyo waliitoa kabisa ikabaki 1
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…