Sukari Yenu
JF-Expert Member
- Dec 8, 2014
- 1,698
- 1,260
Habari wana jamvi, mimi ni kijana na nina mchumba wangu wa muda mrefu kidogo ingawa tuna misukosuko mingi sana. Ili ujue tatzo la mchumba wangu huyu, naomba usome mlolongo wa matukio ktk uhusiano wetu kwanza.
Tulifahamiana mwanzoni mwa mwaka 2011 tukapendana. Mwaka huo huo mwezi Octoba nilienda kuanza chuo kikuu mjini Dodoma hivyo nikamwacha mtaani.
Yeye alikua anaishi na dada yake jirani na nyumbani. Hakufurahia kuondoka kwangu, na alijua nitamwacha na kufuata mabinti wasomi yeye ana elimu ya msingi tu.
Aliniambia nimuachie ujauzito na nimtambulishe nyumbani, wazo ambalo mimi sikuliafiki. Nikaondoka akiwa amekasirika sana mpaka akawa hapokei simu zangu lakin alikuja kunielewa tukaendelea.
Kuna kipindi alienda kwao wakataka kumuozesha akakataa kwa sababu yangu na nilimtumia pesa ya nauli akatoroka.
Alipotoroka alipitia Moshi kwa ndugu zake wengine ambako alipata matatizo ya kubakwa na mtu aliyekua akimsumbua sana kumtaka kimapenzi, baada ya kumlaghai.
Tukio lile lilisababisha,mimba ambayo ni mtoto aliyenae kwa sasa. Haukuchukua muda alirudi jijini Dar tulikutana na tukawa tunashare kitanda lakin hakuniambia kama alibakwa. Badae akabaini ujauzito na alijua fika ni wa yule jamaa wa Moshi ila akaniambia ni wangu.
Nilikua mgumu kuukubali na tuligombana sana cause nilikua nafuatilia tarehe zake. Wakati huo hakua na msaada wowote hapa jijin cause dada yake alisharudi kijijini kwao ila bado alikua anaweza kwenda kazini kwake (waiter katika mgahawa ) nami pia nikimsaidia matumiz madogo madogo na nikilea mimba fifty fifty.
Mara nyingi alitishia kujiua endapo ningemwacha. Aliniomba fedha nyingi ya nauli na matumiz arudi kwao akajifungu, mimi nilimshauri abaki Dar cause mama yangu yupo atamhudumia lakini alikataa, akazidi kunipa mashaka.
Pesa nilimpatia. Baada ya kumbana sana mimba ilipokua kubwa na akagundua nimejua sio yangu akaacha kuwasiliana na mimi kabisa wakati huo nilikua masomoni Dodoma.
Kumbe nilipompa pesa hakuondoka kwao akahama alipokua anakaa na kwenda sehemu nyingine, ndipo nikagundua nimeingizwa mjini ila kwa sababu nilikua nahudumia mimba fifty fifty sikuumia sana.
Alipoenda kujifungua alipata matatzo zaidi, alilazwa amana baadae akapoteza faham akawa referred muhimbili.
Dadake alinipigia simu kunipa taarifa za mtoto wa kike aliejifungua na kwamba anahitaji pesa za matibabu ikiwepo chupa 1 ya damu. Hapo alishaongezewa 1 ikawa inahitajika nyingine. Mimi nikamjibu sitoi hiyo pesa na arudi kumuuliza mdogo wake baba wa mwanawe.
Yule dada alishtuka cause hata yeye alimficha siri ile na alidhani mimi ndie baba wa mtoto. Aliporudi wodini na kumbana mdogo vizuri binti akasema ni kweli mimi sio muhusika wa mimba ile na hakua tayar kuelezea tukio la kubakwa
. Dada alipata hasira akamuacha mdogo wake muhimbil bila msaada wowote kwa wiki 1 na alipoenda alikuta bado yuko vile vile bila msaada na damu yazidi kushuka ila alimchukua mtoto na kurudi nae home.
Siku moja mgonjwa alikamatwa akitaka kutoroka, alilia sana na akang'ang'aniza aruhusiwe aondoke. Madaktar wakampa vitabu akasaini wakamwacha. Akamchukua mtoto na kumpeleka Moshi kwa familia ya mzazi mwenzie.
Walimpa pole na kumlaumu kijana wao tu, wakamwomba bint abadili dini aolewe na mbakaji wake nae akakataa kubadili dini. Au amuache mtoto na wamlipe pesa atakayo akakataa pia. Alichotaka ni matunzo ya mtoto tu. Baada ya kuona familia ya mbakaji haieleweki akajiondoa zake na kwenda Babati kwa ndugu zake wengine na mwanae.
Akajipanga akarudi mjini, maisha yakamuia magumu alifumwa akimbana pumzi mtoto ili afe asiendelee kuteseka. Ni mkatili sana huyu binti. Kipindi hicho chote tangu akate mawasiliano na mimi tulikua hatujawahi kuonana. Mwakajana mwishoni tumeonana na akaniomba msamaha.
Sikumsamehe kwanza, nilitaka kujua kwann alinisingizia mimba. Ndipo alinieleza chanzo cha mimba ile na masahibu yote yaliyomkuta mpaka hapo alipo na kuongeza kuwa alifanya vile ili nisimwache coz alikua bado ananipenda sana. Akaongeza tena kuwa hata jina la pili la mwanawe ni langu mimi na hatolibadilisha.
Nilimwonea huruma sana na maisha anayoishi sasa ni magumu sana sana, plus incidence ya Muhimbili n.k nikajionea sina haja ya kisasi nae. Nimemsamehe. Ila nikamuomba afike nyumbani amuombe radhi mama yangu pia cause anajua kila kitu.
To cut the story ni kwamba ameniomba turudiane na kudai ananipenda sana.
Nikamtega, nikamkubalia kizushi ili nione kama kweli kabadilika na sijala tunda lake mpaka leo hii tangu Novemba mwaka jana aliponiomba turudiane. Kiufupi hatujalala tena pamoja tupo kaka na dada tu.
Sasa kinachonishangaza ni kwamba amekua mtu wa kulalamika sana maisha magumu, anaweza kuniahidi atakuja nyumbani kwangu nilikopanga haji, nikimuuliza anadai kazi nyingi sana. Anadai mtoto anasumbua anaumwa umwa sana cause ana pumu.
Anadai Huko nyuma alidhani mi nimemfanyia ushirikina apate tabu ndio maana akanitafuta aombe radhi. Somtym anahusisha matatizo yake na wazee wake kijijini aliowakimbia kuolewa. Kumbuka tangu 2012 hajarudi kwao baada ya kutoroka. Anawaza kurudi Irangi Kondoa kijijini kwao akaombe radhi wazee wake. Waliotaka kumuozesha ni upande wa mama yake.
Baba yake mzazi hamjui na mama yake amekufa siku nyingi. Kuna siku nimemkuta analia kwake kule na anadai laiti mama yake angelikua hai asingepata tabu zote hizo. Baba wa mtoto hawaelewani tena. Alitaka ahamie kwangu nimemkatalia.
Amekua mtu wa kukata tamaa ya maisha sana. Anaweza hata kuua yule mtoto au kujiua mwenyew yule. Yaani haeleweki tu. Je, nimrudie kiukweli kweli, mi napenda awe tu rafiki yangu tu cause ana attitude ya utafutaji pesa and I like that. Na mtu huyu anahitaji msaada gani?
Tulifahamiana mwanzoni mwa mwaka 2011 tukapendana. Mwaka huo huo mwezi Octoba nilienda kuanza chuo kikuu mjini Dodoma hivyo nikamwacha mtaani.
Yeye alikua anaishi na dada yake jirani na nyumbani. Hakufurahia kuondoka kwangu, na alijua nitamwacha na kufuata mabinti wasomi yeye ana elimu ya msingi tu.
Aliniambia nimuachie ujauzito na nimtambulishe nyumbani, wazo ambalo mimi sikuliafiki. Nikaondoka akiwa amekasirika sana mpaka akawa hapokei simu zangu lakin alikuja kunielewa tukaendelea.
Kuna kipindi alienda kwao wakataka kumuozesha akakataa kwa sababu yangu na nilimtumia pesa ya nauli akatoroka.
Alipotoroka alipitia Moshi kwa ndugu zake wengine ambako alipata matatizo ya kubakwa na mtu aliyekua akimsumbua sana kumtaka kimapenzi, baada ya kumlaghai.
Tukio lile lilisababisha,mimba ambayo ni mtoto aliyenae kwa sasa. Haukuchukua muda alirudi jijini Dar tulikutana na tukawa tunashare kitanda lakin hakuniambia kama alibakwa. Badae akabaini ujauzito na alijua fika ni wa yule jamaa wa Moshi ila akaniambia ni wangu.
Nilikua mgumu kuukubali na tuligombana sana cause nilikua nafuatilia tarehe zake. Wakati huo hakua na msaada wowote hapa jijin cause dada yake alisharudi kijijini kwao ila bado alikua anaweza kwenda kazini kwake (waiter katika mgahawa ) nami pia nikimsaidia matumiz madogo madogo na nikilea mimba fifty fifty.
Mara nyingi alitishia kujiua endapo ningemwacha. Aliniomba fedha nyingi ya nauli na matumiz arudi kwao akajifungu, mimi nilimshauri abaki Dar cause mama yangu yupo atamhudumia lakini alikataa, akazidi kunipa mashaka.
Pesa nilimpatia. Baada ya kumbana sana mimba ilipokua kubwa na akagundua nimejua sio yangu akaacha kuwasiliana na mimi kabisa wakati huo nilikua masomoni Dodoma.
Kumbe nilipompa pesa hakuondoka kwao akahama alipokua anakaa na kwenda sehemu nyingine, ndipo nikagundua nimeingizwa mjini ila kwa sababu nilikua nahudumia mimba fifty fifty sikuumia sana.
Alipoenda kujifungua alipata matatzo zaidi, alilazwa amana baadae akapoteza faham akawa referred muhimbili.
Dadake alinipigia simu kunipa taarifa za mtoto wa kike aliejifungua na kwamba anahitaji pesa za matibabu ikiwepo chupa 1 ya damu. Hapo alishaongezewa 1 ikawa inahitajika nyingine. Mimi nikamjibu sitoi hiyo pesa na arudi kumuuliza mdogo wake baba wa mwanawe.
Yule dada alishtuka cause hata yeye alimficha siri ile na alidhani mimi ndie baba wa mtoto. Aliporudi wodini na kumbana mdogo vizuri binti akasema ni kweli mimi sio muhusika wa mimba ile na hakua tayar kuelezea tukio la kubakwa
. Dada alipata hasira akamuacha mdogo wake muhimbil bila msaada wowote kwa wiki 1 na alipoenda alikuta bado yuko vile vile bila msaada na damu yazidi kushuka ila alimchukua mtoto na kurudi nae home.
Siku moja mgonjwa alikamatwa akitaka kutoroka, alilia sana na akang'ang'aniza aruhusiwe aondoke. Madaktar wakampa vitabu akasaini wakamwacha. Akamchukua mtoto na kumpeleka Moshi kwa familia ya mzazi mwenzie.
Walimpa pole na kumlaumu kijana wao tu, wakamwomba bint abadili dini aolewe na mbakaji wake nae akakataa kubadili dini. Au amuache mtoto na wamlipe pesa atakayo akakataa pia. Alichotaka ni matunzo ya mtoto tu. Baada ya kuona familia ya mbakaji haieleweki akajiondoa zake na kwenda Babati kwa ndugu zake wengine na mwanae.
Akajipanga akarudi mjini, maisha yakamuia magumu alifumwa akimbana pumzi mtoto ili afe asiendelee kuteseka. Ni mkatili sana huyu binti. Kipindi hicho chote tangu akate mawasiliano na mimi tulikua hatujawahi kuonana. Mwakajana mwishoni tumeonana na akaniomba msamaha.
Sikumsamehe kwanza, nilitaka kujua kwann alinisingizia mimba. Ndipo alinieleza chanzo cha mimba ile na masahibu yote yaliyomkuta mpaka hapo alipo na kuongeza kuwa alifanya vile ili nisimwache coz alikua bado ananipenda sana. Akaongeza tena kuwa hata jina la pili la mwanawe ni langu mimi na hatolibadilisha.
Nilimwonea huruma sana na maisha anayoishi sasa ni magumu sana sana, plus incidence ya Muhimbili n.k nikajionea sina haja ya kisasi nae. Nimemsamehe. Ila nikamuomba afike nyumbani amuombe radhi mama yangu pia cause anajua kila kitu.
To cut the story ni kwamba ameniomba turudiane na kudai ananipenda sana.
Nikamtega, nikamkubalia kizushi ili nione kama kweli kabadilika na sijala tunda lake mpaka leo hii tangu Novemba mwaka jana aliponiomba turudiane. Kiufupi hatujalala tena pamoja tupo kaka na dada tu.
Sasa kinachonishangaza ni kwamba amekua mtu wa kulalamika sana maisha magumu, anaweza kuniahidi atakuja nyumbani kwangu nilikopanga haji, nikimuuliza anadai kazi nyingi sana. Anadai mtoto anasumbua anaumwa umwa sana cause ana pumu.
Anadai Huko nyuma alidhani mi nimemfanyia ushirikina apate tabu ndio maana akanitafuta aombe radhi. Somtym anahusisha matatizo yake na wazee wake kijijini aliowakimbia kuolewa. Kumbuka tangu 2012 hajarudi kwao baada ya kutoroka. Anawaza kurudi Irangi Kondoa kijijini kwao akaombe radhi wazee wake. Waliotaka kumuozesha ni upande wa mama yake.
Baba yake mzazi hamjui na mama yake amekufa siku nyingi. Kuna siku nimemkuta analia kwake kule na anadai laiti mama yake angelikua hai asingepata tabu zote hizo. Baba wa mtoto hawaelewani tena. Alitaka ahamie kwangu nimemkatalia.
Amekua mtu wa kukata tamaa ya maisha sana. Anaweza hata kuua yule mtoto au kujiua mwenyew yule. Yaani haeleweki tu. Je, nimrudie kiukweli kweli, mi napenda awe tu rafiki yangu tu cause ana attitude ya utafutaji pesa and I like that. Na mtu huyu anahitaji msaada gani?