Msaada: Mabinti hawa email zao zinafanana

Msaada: Mabinti hawa email zao zinafanana

...kama wamekufuata dictate hii movie, wambie waje hapo ulipo na project zao mkononi, from there kila hatua unafanya na mwanasheria wako...
 
Hao sio mabint ni madume, hutumia majina mazuri ya kike ili wawaibie wanaume wazembe.

Ukiangalia wote hutaka uwape email yako wakijifanya hawana muda wa kuwa fb. Mi nishawazoea ukifungua profile zao utakuta kapicha kamoja au tuwili pia utakuta ana friends wasozidi 5.

Ukiwa makini utagundua hii account magumashi tupu. Majina yao wengi from West Africa.

Awake my fellow members!
 
Hao sio mabint ni madume, hutumia majina mazuri ya kike ili wawaibie wanaume wazembe.

Ukiangalia wote hutaka uwape email yako wakijifanya hawana muda wa kuwa fb. Mi nishawazoea ukifungua profile zao utakuta kapicha kamoja au tuwili pia utakuta ana friends wasozidi 5.

Ukiwa makini utagundua hii account magumashi tupu. Majina yao wengi from West Africa.

Awake my fellow members!
Wewe nakuona kama nabii kwani unayoyasema yako hivyohivyo.

Hao wote sijaona wana mutual friend yeyote, na picha zao hazizidi 2.

Du mwenye ule wimbo wa umasikini huu utaisha lini atuwekee humu tutafakari.

Nawashukuru wadau.
 
Mkuu hata mimi leo imenitokea hiyo binti anatoka senegal anaitwa Jennth Jobe, nimegundua ni wezi mkuu, hapa najipanga nimtukane!

Usipoteze muda wako bure kuchafua moyo wako, bora ukakaa kimya maana haikupunguzii kitu.
 
Mimi pia napataga ila ile messege nairipotigi FB kama harrassment wanaidelete. Sio siri wanakera sana
 
wachache sana wenye bahati kama yako
kama vp tafuta hata nauli mfuate hukohuko kapige bingo wewe ooh..!?
 
Ndugu chomoka kama mshale bila kugeuka nyuma,hata mimi walitaka kunitapeli ila nikawagundua yaani upate 20 percent hivi hivi kiulaini ?
 
Habari zenu wakuu.Mimi ni mtumiaji pia wa facebook.Kuna mabinti sasa wanafikia watatu ambao waliniomba niwe mshirika wao wa biashara kuwekeza nchini kwetu TZ.Kwa nyakati tofauti wamekuwa wakiomba ushirikiano wa kibiashara.Lakini hadi hapa nimegundua yafuatayo:
1.Maelezo yao kwenye email yanafanana
2.Maeneo wanayojieleza kutokea yanafanana(Senegal,Siera Leon)
3.Sababu ya kuwa kambi za wakimbizi zinafanana(Baba zao walifariki na walikuwa viongozi wa serikali au wafanya biashara.)
4.Hawataki tuwasiliane kwa facebook ila kwa email tu.
Hao wote wametaka maelezo yangu binafsi,maisha na akaunti za benki ila sijawapa.Haya ni majina yao;Tina Thiara,Queen Thiara na Minnie Bagbo Sankawulo.
Ndugu zangu,huu mchezo unaitwaje na je niko salama?Kuna yeyote amewahi kukutana na majina hayo?Nahitaji msaada wenu zaidi hapo.

FUTA DELETE KABISA!...mpaka hapo walishakuibia!
 
Wezi hao ukisikia Hackers ndo hao sasa na kwakifupi wengine ni wanaume tena wengi wao.
 
Aende nao mwishoni starling awe yeye

Kuna mmoja nilienda naeeeeee,ikafika point eti anataka nimtumie dola 8000 ku faciltate mambo,mi nikamwambia ntamtumia fasta ila atume yeye kwangu dola 1000 tu ili ziniwezeshe kupata anazotaka!jamaa likapotea likaninyima u sterling aisee!
 
uko duniani gani hujashtuka hadi leo?
huo ni wizi wa kizamani sana.
wengine sasa wanatuma email kukuarifu kuna doc wamekutumia click here and enter your email and password
ukijaribu tu umeliwa,wanaita phishing sites ..
ignore those stupid emails.
 
Ushirika wa biashara unatafutwa facebook?! walipenda picha yako au?
Hata hukujiuliza? Ushirika wa biashara wewe ikiwa kama nani? Kwanini wewe?
Hadi mkatwe vichwa ndio muelewe kupenda vitu vya bure bure!

Ama kweli, "..watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa"
 
Habari zenu wakuu.Mimi ni mtumiaji pia wa facebook.Kuna mabinti sasa wanafikia watatu ambao waliniomba niwe mshirika wao wa biashara kuwekeza nchini kwetu TZ.Kwa nyakati tofauti wamekuwa wakiomba ushirikiano wa kibiashara.Lakini hadi hapa nimegundua yafuatayo:
1.Maelezo yao kwenye email yanafanana
2.Maeneo wanayojieleza kutokea yanafanana(Senegal,Siera Leon)
3.Sababu ya kuwa kambi za wakimbizi zinafanana(Baba zao walifariki na walikuwa viongozi wa serikali au wafanya biashara.)
4.Hawataki tuwasiliane kwa facebook ila kwa email tu.
Hao wote wametaka maelezo yangu binafsi,maisha na akaunti za benki ila sijawapa.Haya ni majina yao;Tina Thiara,Queen Thiara na Minnie Bagbo Sankawulo.
Ndugu zangu,huu mchezo unaitwaje na je niko salama?Kuna yeyote amewahi kukutana na majina hayo?Nahitaji msaada wenu zaidi hapo.

Hahaha,,
Hii ishakuwa kawaida fanya hivii,,,,,,
CHUKUA EMAIL YAKE ICOPY KAMA ILIVO NA UIWEKE GOOGLE THEN ISEARCH
UTAONA MASWALI YAO MWANZO HADI MWSHO,,
THEN UKISHAYAJUA HAYO MASWALI SASA,,ENDELEA KUCHAT NAEEEEE,,,UTACHEKA SANA MAANA MTIRIRIKO UTAKAOUONA GOOGLE NDVO WATAENDA NAO MPAKA UTAKAPOACHA,,
TEST UONE
 
Ni kweli. Hao wanaitwa scrammers. Tulizoea wengi from Nigeria, ila siku hizi ata Dar wapo.
Kama umeshawapa Email, usiogope, wala hawatakuibia kiuchawi, ila kama unatamaa ya hela, ndio utaibiwa, tena kwa kutuma mwenyewe hizo hela.

Chukua sehemu ya hiyo msg/email waliokutumia kisha u-google, utaona walalamikaji walivo wengi. Na wengine wamelizwa.
 
Back
Top Bottom