Msaada lodge/gesti nzuri Tanga Mjini

Msaada lodge/gesti nzuri Tanga Mjini

jembelamkono

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2015
Posts
2,733
Reaction score
2,016
Naelekea safari ya kikazi Tanga mjini. Naomba mwenye kufahamu lodge/ geust nzuri karibu na mjini anisaidie.

Iwe na essentials kama usafi wa kuridhisha, AC, TV na parking. Budget yangu ni Tsh elfu 20 mpaka 30.

Msaada wenu tafadhali.
 
Ulizia Sea Breeze!
25,000Tshs IPO Mjini karibu na Bahari na kitUo cha RATCO.
 
Ulizia Sea Breeze!
25,000Tshs IPO Mjini karibu na Bahari na kitUo cha RATCO.

Mkuu usafi na security ukoje,kidogo mwana Jf mwenzenu nitapeliwe,nimepelekwa gesti ya vichochoroni.
 
Mkuu nenda nyinda 2 ni elfu thalithini na tano lakini no poa sana
 
(Ocean Breeze)Usafi - excellent!
Security inaridhisha. Ukiwa na Laptop au valuables wanakushauri kuhifadhi reception.
 
Kwa eneo lote la chuda utapata lodge nzuri Kuna mtendele,macaroous,Nyinda Na dolfin zipo karibu Na Kama unapenda baa utaenjoy .
 
Fika nyinda mdau ila maeneo ya see breeze usiguze ni hatariiiiii
 
Pentagon Palace kwa usalama, parking, usafi na ubora wa vyumba wako vizuri zaidi na pametulia. Ila ukipenda sehemu ambako unaweza kujichanganya zaidi na watu kwa vyakula, vinywaji na "mambo mengine" Mtendele, Nyinda Executive 1 & 2, Macarious na Dolphin pote huko patakufaa. Na bei zao naona ziko ndani ya budget yako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom