Msaada kwa watu wanaotaka kutoka kwenye ndoa

Msaada kwa watu wanaotaka kutoka kwenye ndoa

Walnut Creek

JF-Expert Member
Joined
Mar 17, 2009
Posts
5,812
Reaction score
6,327
Habari za leo wadau,

karibuni pamekuwa na kesi nyingi za wanandoa kukosa uamininifu na mabalaa mengine kibao.

Mimi nadhani imefika wakati watu waanze kutanguliza furaha na afya zao mbele kuliko kufurahisha jamii. Kuna wanandoa wapo kwenye ndoa kwa kujikaza na kuvumilia tu lakini ile furaha na mapenzi ya ndoa hawana.

Je ni sawa kweli watu wazima kuishi maisha kama jela? Je watu waliochoka ndoa zao hawana haki ya kuondoka na kutafuta furaha sehemu nyingine? Baada ya maswali hayo mawili ningependa nijue njia za kisheria ambazo watu waliochoka ndoa zao wanaweza kuzifuata kuachana na ndoa zilizowashinda.

N.b: Sijaoa lakini nadhani imefika wakati ndoa zisiwe jela bali ushirika wa furaha.
 
Hicho ulichokiongea ni romous tu. Utaletaje hapa mambo ambayo hujayafanyia uchunguzi?
Hhapo ni sawa na kuelezea utam wa mwanamke ambaye bado hujamuonja ila kwa vile uliskia tetesi kuwa ana maji au mkavu na ww ndio unatuelezea hapa.
Ntakuja kukubaliana na ww mpaka pale utakapo kujaoa.
Watu wengi humu jf mnazielezea ndoa tofauti sana wakat hata hamjaingia kwenye ndoa.
Babu zetu na baba zetu pamoja na bibi na mama zetu wangekuwa na mitazamo kama yetu hata mm na ww yawezekana tusingezaliwa au tungekuwa single parent family
 
Kitendo cha kutokuwa kwenye ndoa ina maana hakuna familia, kama hakuna familia hakuna uzao duniani jambo ambalo liktauwa ndio mwisho wa dunia au dunia isiyokuwa na maadili. Kumbuka kuna single parent familly, lakini zina matizo yake.
 
Habari za leo wadau,

karibuni pamekuwa na kesi nyingi za wanandoa kukosa uamininifu na mabalaa mengine kibao.

Mimi nadhani imefika wakati watu waanze kutanguliza furaha na afya zao mbele kuliko kufurahisha jamii. Kuna wanandoa wapo kwenye ndoa kwa kujikaza na kuvumilia tu lakini ile furaha na mapenzi ya ndoa hawana.

Je ni sawa kweli watu wazima kuishi maisha kama jela? Je watu waliochoka ndoa zao hawana haki ya kuondoka na kutafuta furaha sehemu nyingine? Baada ya maswali hayo mawili ningependa nijue njia za kisheria ambazo watu waliochoka ndoa zao wanaweza kuzifuata kuachana na ndoa zilizowashinda.

N.b: Sijaoa lakini nadhani imefika wakati ndoa zisiwe jela bali ushirika wa furaha.
Nasubiri thread yako utakayoiandika pindi utakapokuwa kwenye ndoa!
 
Sasa utaandika mambo.ya dunia wakati hujaingia au umeandija kihisia maisha yoyote ya binadamu yanachangamoto zake pia uzuri wake usiishi kwa kucremisha kwahyo kwa ajili ya matatizo yanayotokea watu wasiwe na ndoa think beyond pilipili usiyo ila ya kuwashia nini
 
Unataka watoke kwenye ndoa wawe ""wahuni""kama wewe mfanane?
 
ndoa ndoa ndoa ndoa...................................
 
kila nikichabo jf ndoa ndo mada kuu,what is going on.........
 
Nyie wapinga kristo mumetokea wapi? Ndoa ndoa najua lala 0 huyu ...
 
ukiwa muumini wa dini yoyote utakuwa unajua kuwa ndoa ni fungate lililo chini ya mamlaka ya mungu hivyo ukiona ndoa imedumu ni kwa baraka za mungu na kama imevunjika pia ujue ni mpango wa mungu kuepusha dhambi zaidi kwa kutendeana uovu na uzinzi..waweza ona kuwa wanandoa wanateseka kwa ajili ya ndoa yao ni kweli but ujue pia watu hao wanahanagaikia pepo yao na furaha ya watoto wao ukiona unakua na mawazo mepesi ya kuachana na ndoa ujue unasehemu kubwa sana ya ubinafsi kwenye moyo wako na hivyo hustahili kuingia kwenye ndoa... ni vyema uelewe kuwa ndoa ni taasisi siyo mahusiano ya kimkataba ambapo parts za contract zinaweza kurescind na kuvunja mkataba kwa hiari .je umewahi kujiuliza kwanini hitimisho la ndoa ni fungate mbele ya Padre au sheikh kwanini isingekua holela tu..nadhani kama hukidhi vigezo vya ndoa bora uiache usijechuma dhambi bure
 
Back
Top Bottom