Ndugu zangu!
Mimi ni mara ya kwanza kujenga, na nimefanya vitu vingi tayari kilichobaki kikubwa sasa ni kuweka Gypsum, mbao ameshaweka tayari, na plaster ishapigwa wa umeme kashafanya yake pia.
Fundi aliyeweka mbao zile za gypsum ndio uyo uyo atakuja kufunga gypsum, sasa basi mwanzo kanicharge kwa kazi ya kuweka mbao kwa laki 6 sikubisha nikampa kama ilivyo, na sasa kaniambia kufunga gypsum labour charge ni 1,000,000/=.
Sasa hapa nimekuwa njia panda hii ni sahihi au amenizidishia, maana hata nikipunguza nitapunguza kwa ngapi,hii nyumba ya kawaida vyumba vitatu vya kulala, sebule, dining .
Asanteni kwa ushauri!