Msaada kwa anayejua kuhusu Recategorization

Msaada kwa anayejua kuhusu Recategorization

mteule senior

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
296
Reaction score
197
Poleni na majukumu wakuu. Mungu ni mwema kila wakati..

Kwa wale walio kazini nafikiri watakuwa wanajua kuwa, mtu aliyesoma degree tofauti kwa mfano katika Elimu anaweza akafanya Postgraduate Diploma in Education na akaajiriwa kama mwalimu sawa na yule mwenye Bachelor of Education.

Sasa kwa mfano, mwajiriwa alisomea degree tofauti na Computer Science kwa mfano, na akafanya Postgraduate Diploma in Computer Science, je anaweza kufanyiwa recategorization na kutambuliwa sawa na yule aliyekuwa na Bachelor ya field husika? Maana nasikia kwa upande wa masters tofauti na degree ya kwanza haiwezekani

Naombeni uzoefu wenu kwa wanaojua suala hili
 
Kuna baadhi ya field inakubalika lakini kuenda Ualimu ni shida sana na simply haiwezekani hasa kama unategemea muajiri wako awe Mkurugenzi mkoani au wilayani. Ila kama ni vyuo vya umma may be yes.

Simply napenda watu wajue, Degree yako ndiyo fani yako. Degree ya kwanza ndio ina define Taaluma yako. Hata kama unafanya Postgraduate diploma hakikisha upo within a field usiende mbali sana

Zala Na Nga
 
Hazchem plate,
Sijui ni typing error ila kama umemaanisha nakupinga. Postgraduate kwenda ualimu ni rahisi na wengi ufanya hivyo na wanaajiriwa kama walimu baada ya kujiongeza na postgraduate ya education huku background akiwa na fani tofauti na elimu.

Mfano ict, sheria n.k
 
Back
Top Bottom