Msaada kuhusu ushauri wa kodi za magari

Msaada kuhusu ushauri wa kodi za magari

shaurimbaya

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2013
Posts
1,915
Reaction score
2,337
Heshima kwenu wadau

Kwa ufupi nimenunua gari yangu ya kwanza mwez huu na umeingia nchini last week..

Agent wangu akafanya taratibu zote za assesment na nikapewa karatasi inayoonesha kodi nayopaswa kuilipa tra..

Ile fomu imeandikwa commissioner wa customs na ikawekwa account no. na jina la bank ambayo commissioner ana miliki account ambayo imeandikwa bank of tanzania..


Baada ya agent kunipa hiyo fomu nikaichek na kwenda bank yangu napotumia crdb na kulipa hiyo kodi kwenye account ya kwenye fomu yangu ya assesment ambayo nilituma straight BOT kwenye account ya commissoner wa customs kwa tt transfer.

Then nikamjib agent nimeshalipa na kumpa copy ya tt..

Sasa agent kaenda port kufatilia release order kaambiwa kodi haionekani kwenye system..

Ningepaswa kuilipa kwa ku deposit kawaida kwenye bank yoyote so gari haipewi release order.

Hapo ndipo nimedata sijui hata nianzie wapi
 
Huyo Agent wako nae mie namshaka nae.
We Agent gani anashindwa kukusaidia Customer wake kesi ndogo kama hii.
Mie gari yangu ya mwanzo nilinunua hapahapa,na ya pili hapahapa kukwepa huu usumbufu.
Nikinunua ingine ndio nafikiria kuagiza,maana gari ya mwanzo roho juu,maana hapo haiafikla ila sipati picha moyo wako siku ya kuiona itakuwaje,either furaha au msiba mwingine.

Hili tatizo mwenye uwezo wa kukusaidia ni Agent wako,pesa sio lazima u deposit on Cash,huu mfumo haupo kabisaa.Unaweza ku deposit kwa mfumo wowote muhim pesa zimeingia kwenye account.
Tatizo hizi kazi siku hizi ujanja ujanja mwingi sana,na baadhi ya Agents wanakuwa wanahusika pia.
 
Mchunguze huyo agent wako vizuri alitaka kukuingiza mjini umpe cash akalipe kidogo nyingine atie mfukoni ndio michezo yao hao maagent. Haiwezekani ulipe pesa halafu isionekane kwenye statement labda hiyo account uliotuma TT yako ipo hongkong au vietnam na sio tanzania.
 
Mchunguze huyo agent wako vizuri alitaka kukuingiza mjini umpe cash akalipe kidogo nyingine atie mfukoni ndio michezo yao hao maagent. Haiwezekani ulipe pesa halafu isionekane kwenye statement labda hiyo account uliotuma TT yako ipo hongkong au vietnam na sio tanzania.

ndio hapo ninaposhangaa.. yaani gari nimelipia kodi na bado release order nazungushwa..

kwanza kodi wame uplift sana na bado nikailipa kama ilivyo..

eti wananiuliza why nimetuma kwa wire transfer..

nimeshangaa TT kuchelewa kuonekana wakati ndio mfumo wa fasta..

wakati nanunua gari japan nilituma tt saa 4 asubuh baada ya masaa 3 jamaa wa japan akaiona kwenye account yake na kunijibu amepata hela.

but hawa wabongo wanasema hela haionekani na hii hela tt crdb kaifanya wife mwenyewe haina hata makosa
 
Back
Top Bottom