Msaada kuhusu ununuzi wa hii nyumba

Msaada kuhusu ununuzi wa hii nyumba

vamda

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2012
Posts
919
Reaction score
598
Nawasalimu wana JF wote,

Kuna mtu ameniomba msaada kuhusu jambo lifuatalo: Rafiki yake anataka kumuuzia nyumba iliyojengwa kwenye kiwanja ambacho bado hakijapimwa. Karatasi ya manunuzi ya kiwanja hicho haikushirikisha serikali ya kijiji, yaani iliandikwa kienyeji ingawa kulikuwa na mashahidi.

Je, afanyeje akitaka kuinunua nyumba hiyo ili asipate matatizo hapo baadae?

Nimemwambia suala hili nitalipeleka kwa wana JF ili watoe ushauri.
 
mwambie waende wakaandikishane mahakamani, kwani huko hata garama kama za mashahidi na za selilari ya kijiji hazita kuwepo, mahakama hukata asilimia ndogo sana ukilinganisha na ambayo angeilipa ktk selilari za mitaa
 
kama ardhi ambayo nyumba hiyo imejengwa ipo ndani ya ardhi ya kijiji basi ipo chini ya usimamizi wa serikali ya kijiji, cha kufanya kwanza ni kwenda kwenye serikali ya kijiji ili kujiridhisha kama wanamtambua muuzaji kama mmiliki halali wa eneo hilo,ni vema pia ukapitia kwa majirani wa eneo hilo ili kujiridhisha na mipaka na uhalali wa umiliki wa muuzaji.Mauzo yote ya ardhi ndani ya mipaka ya kijiji ni lazima yashuhudiwe na serikali ya kijiji kama wasimamizi wa ardhi ya kijiji kwa niaba ya wanakijiji wote na endapo itatokea utata kati ya umiliki serikali ya kijiji itaitwa mahakamani kuthibitisha uhalali wa manunuzi uliyofanya. Zingatia kumuuliza muuzaji kama ameoa au la na pia kama ardhi ile ni ya ukoo au yake binafsi kwa kuwa itahitaji uthibitisho wa mke wake katika hati ya ununuzi au uthibitisho wa kikao cha ukoo kumruhusu kuuza ardhi hiyo.
 
Kama kiwanja hakina mizengwe anunue ila ahakikishe anakipima. Aulizie kwa majirani halafu afuate process kwenye serikali za mitaa.
Nawasalimu wana JF wote. Kuna mtu ameniomba msaada kuhusu jambo lifuatalo: Rafiki yake anataka kumuuzia nyumba iliyojengwa kwenye kiwanja ambacho bado hakijapimwa. Karatasi ya manunuzi ya kiwanja hicho haikushirikisha serikali ya kijiji, yaani iliandikwa kienyeji ingawa kulikuwa na mashahidi. Je, afanyeje akitaka kuinunua nyumba hiyo ili asipate matatizo hapo baadae? Nimemwambia suala hili nitalipeleka kwa wana JF ili watoe ushauri.
 
asinunue kabla hajaenda kuhakiki wizarani hicho kiwanja ni makazi au la asije uziwa mbuzi kwenye gumia kesho akaiona serikli imemuonea kutokuawa na document kiwanja kisichopimwa ni kawaida akishahakikisha ni halali wizarani atapima then atapata document halali kisheria.
 
Nawashukuru wana JF kwa taarifa. Namwambia kadiri mnavyoendelea kutoa ushauri wenu.
 
Usiende mahakamani utaingia chaka;
1. Tafuta town planner au surveyor acheki status ya eneo cost sio zaidi ya 200,000/=
2. Tafuta wakili lakini mashahidi lazima baadhi watoke eneo husika especially local gvt leaders wa eneo hilo.
 
Back
Top Bottom