Poluyakhtov
JF-Expert Member
- May 9, 2017
- 365
- 306
Habari za asubuhi wana JF,
Kama kichwa cha thread kinavyojieleza, kuna ndugu yangu wa kiume mwenye umri wa miaka 30. Yeye ni mhitimu wa chuo kikuu miaka 5 iliyopita, alisomea Bachelor of Human Resources Management.
Alipohitimu tu;akabahatika kufanya kazi ya muda kwenye ofisi moja ya shirika la umma. Kazi hiyo hakudumu nayo sana kwani aliarifiwa kuwa kazi hiyo ilikuwa imemalizika.
Tangu hapo, mdogo wangu amekuwa ni mtu wa huzuni na kukata tamaa, na kuna muda anawaza hata kujitoa uhai, hasira hata kwa vitu vidogo tu. Hata kulala kwake ni mtihani. Anamuona kila mtu kama adui kwake.
Natamani sana kumsaidia ndugu yangu, tatizo sijui nianzie wapi au ni hospitali ipi inatoa huduma kwa matatizo kama hayo.
Naomba msaada wa maelekezo wa sehemu husika na gharama kama itawezekana.
Asanteni.
Kama kichwa cha thread kinavyojieleza, kuna ndugu yangu wa kiume mwenye umri wa miaka 30. Yeye ni mhitimu wa chuo kikuu miaka 5 iliyopita, alisomea Bachelor of Human Resources Management.
Alipohitimu tu;akabahatika kufanya kazi ya muda kwenye ofisi moja ya shirika la umma. Kazi hiyo hakudumu nayo sana kwani aliarifiwa kuwa kazi hiyo ilikuwa imemalizika.
Tangu hapo, mdogo wangu amekuwa ni mtu wa huzuni na kukata tamaa, na kuna muda anawaza hata kujitoa uhai, hasira hata kwa vitu vidogo tu. Hata kulala kwake ni mtihani. Anamuona kila mtu kama adui kwake.
Natamani sana kumsaidia ndugu yangu, tatizo sijui nianzie wapi au ni hospitali ipi inatoa huduma kwa matatizo kama hayo.
Naomba msaada wa maelekezo wa sehemu husika na gharama kama itawezekana.
Asanteni.