Mzee,
Nikupongeze.
Maana sio kazi rahisi, changamoto ni nyingi mno ambazo naamini umekumbana nazo hadi kijana kumaliza shule.
Pia nimpongeze na kijana pia kwa kuhitimu!
Kuhusu kichapo,
Basi usimtandike tena, ataathirika kisaikolojia, na pia ataweka chuki na wewe.
Naomba ujaribu kukaa nae, uongee nae kama rafiki sasa
Umuulize kwanini anahitaji kwenda hicho chuo.?!
Akikupa sababu zake, nawe umueleweshe kwanini unakipinga na umwambie chuo ambacho unahitaji aende, umpe na sababu zako!
Naamini atakuelewa na atakwenda kwa moyo mmoja.
Ninaongea haya nikiwa kama kijana chini ya miaka 25