Msaada kijana wangu kapinda mguu

Msaada kijana wangu kapinda mguu

WENYELE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
1,461
Reaction score
1,544
Habari wakuu,

Kijana wangu wa miaka 8 alizaliwa salama cha ajabu sasa hivi mguu umepinda.

Nilienda hospitali tukaambiwa mguu wake haujaunganika kwenye goti, nikampeleka Bugando ili afanyiwe operation bahati mbaya hakufanikiwa sababu ya daktari wake kutokuwepo kwa muda mrefu.

Kwa kuwa alikuwa hana bima na hela za kuunga unga ilibidi kumrudisha kijijini.

Sasa nimepata vihela kidogo nataka nimrudishe tena, ila natafuta kliniki ya private bora kama ipo Mwanza, nimpeleke akafanyiwe operation.

Wataalamu naomba msaada wenu kujua kliniki bora ya mifupa jijini Mwanza ili nimpeleke dogo.

Lengo langu la kutafuta private ni ili mtoto apate huduma ya haraka, pale Bugando tulienda zaidi ya miezi miwili kila siku ilikuwa lugha tu.
 
Pole sana mkuu.

Wacheki Aga Khan (nina imani wana Tawi lao huko), pia nenda Hindu ile ya karibu na Bugando ukiwa unashuka njia ya kwenda Igogo.

Ukaulizie kwanza kama hiyo huduma ipo
 
WENYELE, Ikishindikana huko mlete hata muhimbili mkuu maana hilo tatizo lisipo fanyiwa utatuzi litakuja kumletea shida sana ukubwani abaki kukulaumu. Maana wewe now ndio imeshikilia hatma ya maisha yake. Mwanza to dar ni siku moja ikishindikana huko wai fasta unaweza pata suluhisho.
 
WENYELE, Ikishindikana huko mlete hata muhimbili mkuu maana hilo tatizo lisipo fanyiwa utatuzi litakuja kumletea shida sana ukubwani abaki kukulaumu. Maana wewe now ndio imeshikilia hatma ya maisha yake. Mwanza to dar ni siku moja ikishindikana huko wai fasta unaweza pata suluhisho.
Asante sana mkuu; natamani kujua nikimpeleka Muhimbili, anaweza akapata huduma baada ya muda gani? Nitachowaza ni ile gharama ya kuishi mjini ukikaa Lodge huku ukisubiri huduma.
Kwa Dar sina ndugu ila naweza vumilia ikiwa atapata huduma ndani ya muda mfupi
 
WENYELE, Mimi nafahamu CCBRT Dar es Salaam wana huduma nzuri ya kunyoosha miguu iliyopinda. ila ni vizuri kupokea ushauri utakaokupunguzia gharama
 
Ningependa pia kupatiwa roughly cost km kuna mtu anajua pale Muhimbili, Bugando gharama ilikua 350,000 kupanda juu
 
I recommend CCBRT ni wazuri sana kwenye viungo
Nashukru sana Mkuu kwa vipimo vya awali niliambiwa mguu wake haujaungana kwenye goti kwa hiyo kuna misuli inanazidiwa na uzito that why unapinda. Ni mguu mmoja tu uliopinda.
Je CCBRT wanahuduma ya kuunganisha? Samahani wakuu wa maswali maana mimi sina uzoefu sana.
 
WENYELE,
Nenda CCBRT kama Mwanza wapo mpeleke kama hawapo Mwanza basi mpleke CCBRT ya Moshi, Kilimanjaro kwako ndio naona itakuwa rahisi. Wanasaidia sana, hata mwanangu alipataga hiyo shida ya kupinda miguu wakamtengenezea viatu sasahivi ukimuangalia hata huwezi kujua kama alipindaga miguu yupo vizuri kabisa.
 
Nashukru sana Mkuu kwa vipimo vya awali niliambiwa mguu wake haujaungana kwenye goti kwa hiyo kuna misuli inanazidiwa na uzito that why unapinda. Ni mguu mmoja tu uliopinda.
Je CCBRT wanahuduma ya kuunganisha? Samahani wakuu wa maswali maana mimi sina uzoefu sana.
CCBRT ni wazuri na wana viungo maalumu artificial vya kusaidia kuunga! Kabla hujaamua wapi uende, jaribu kupiga simu waeleze uombe appointment. Utafanikiwa na huenda hata operesheni iisifanyike
 
Miaka 8 alitakiwa awe na Toto afya ya 50400 tu. Angetibiwa popote pale.
Kakate hiyo bima, baada ya siku 90 itakusaidia endapo yatajitokeza mengine
 
Mkuu hebu ingia mtandaoni kwenye website ya ccbrt chukua namba yao ongea na customer care. Utapata information za uhakika zaidi kuliko hapa jf.
Ningependa pia kupatiwa roughly cost km kuna mtu anajua pale Muhimbili, Bugando gharama ilikua 350,000 kupanda juu
 
Mkatie toto afya kadi ya NHIF, huwezi kujua mwisho wa matibabu utakuwa lini na utakuwaje.

Kina kijana mmoja wa primary nilikutana nae ana shida ya mguu kupinda na akawa hana huduma. Nilimsaidia kumkatia tot kadi na mpaka leo hii ameshafanyiwa zaidi ya operation nane na still hajapona.

Inaonekana kuna bacteria wanashambulia mfupa. Kwa hiyo kama ana cheti cha kuzaliwa anza mchakato, inachukua siku 9 za kazi tangu ulipojaza fomu mpaka kupata kadi.

Pole sana ndugu.
 
Tatizo umesema hela ya kuunga unga, ungekuwa vizuri hata hapo Bugando ungempeleka kwenye huduma ya fast ya Private.
Au mpeleke Muhimbili lipia hiyo Fast track sijui wanaita PPM.
Hautakaa kabisa.

Au mpeleke Regency Medical Centre pale Upanga, wanakuja daktari bingwa toka Muhimbili utafanya ndani ya siku 3 tangu umpeleke mtoto kwa mara ya kwanza.
 
Bora kwenda ccbrt , kwakua mwanza nikaribu bora urudi tena Bugando iliwakufanyie vipimo upya kwaajili ya operashani...lakini ukikata bima kabla itakusaidia sana hata katika hospital stay hapa bugando na vipimo vyote
 
Back
Top Bottom