Mimi nilifiwa na mzazi wangu wa kiume ambaye alikuwa mwajiriwa serikalini. Baada ya mazishi kikao cha wanandugu kilimteua baba mdogo kama mfuatiliaji wa mirathi. Lakini tangu kuteuliwa kwake huyo baba mdogo hafuatilii waa haonyeshi juhudi zozote. Swali kwenu ndugu zangu wana jf,SHERIA INASEMAJE KUHUSU KUMBADILISHA MSIMAMIZI WA MIRATHI ENDAPO ALIYEPO HAONYESHI KUWA ACTIVE? Naombeni msaada kwa hilo kwa mwenye uzoefu wa kesi hiyo ama mwenye ufahamu wa sheria juu ya hilo