Msaada: kama upo US(Marekani)

Msaada: kama upo US(Marekani)

Bwana saimon huyo ndugu yako anadeka,
Yupo nchi za watu alafu anaona aibu kufanya kazi za unskilled labour..

Mwambie aende kwenye mahotel huko akaombe kufanya usafi,kuosha vyombo uku akiweka mambo yake sawa...

Kama vipi aje bongo kwanza alafu ajipange upya,akiendelea kukaa hivhvi mwiaho wa siku atakosa ata nauli ya kurudia nyumbani
 
akiwin case yake nipm nimpe mchongo tuje kusogeza mwendo kas huku washington d.c
 
Kuna waTanzania watatu wapo US humu JF lakini sifahamu ni State gani.
 
Akizidiwa na shida, na asione mbele wala nyuma, ajisalimishe kwa balozi wetu Masilingi.
Watanzania hata huko Boston wapo wengi na naamini kuna jumuiya za watanzania miji mbali mbali huko marekani.
Ningemshauri angetafuta hizo jumiya awaeleze shida yake, naamini lazima atakuwepo wa kumsaidia hata kwa kumsitiri kwa muda akiwa anajipanga kama anavyoeleza yeye. Sifahamu ni msaada gani anauhitaji kwako mleta mada, lakini kama haupo marekani unadhani utamsaidia vipi?! Kuleta hapa jukwaani ni njia moja lakini pale ground sijui anamudu vipi kama hana kazi kabisa.
Yeye binafsi angejisaidia kwa kutafuta jumuiya za watanzania zilizopo hapo Boston au miji ya jirani, au hata nje ya state hiyo ikibidi. Sijui ukubwa wa tatizo lake kiuhalisia licha ya mleta mada kulieleza hapo kijuu juu lakini naweza kushauri ajitahidi kutafuta watanzania hapo mjini wanaweza kumsaidia kwa namna moja au nyingine.
 
Mkuu hiyo inawezekana.. Anaruhusiwa kuishi ad mwez wa 11.. View attachment 1094629
Ikiwa hana work permit na social security number aliwezaje kuendesha truck mkuu?, Manake hata driving license hawezi kupata bila ya hivyo vitu. Muulize yupo tayari kuhama state nyengine kufanya kazi hio chini ya meza. Niongee na wasela wangu kule


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Ushauri wangu huyo dada abadili state harafu aingie kwenye construction, ndio sehemu pekee imebaki unawezafanya kazi bila vibali. Serikali haijaweza kuinforce sheria sana kwenye hiyo sector. Zaidi ahamie sanctuary city sheria loose kidogo unaweza subiria kazi kwenye ofisi za labor finder au home depot, lowes etc.
 
Kwa nchi kama marekane kuna kaz nying sana labda awe anachagua na pengine labda hana work permit mzee..mwambie asichague kaz aisee apige kaz yeyote huko hakuna anayemjua bro
 
Ni mwaminifu ila tatizo ni mgeni mkuu
Haeleweki, ndiyo maana watu wanakwambia siyo mwaminifu.

1. Kuendesha trucks bila leseni (ya Truck driving)
2. Mpaka ashinde kesi ndiyo apate makaratasi (Siyo kweli, makaratasi unapata uki - file tu, mpaka ushindwe kesi).
3. Boston watanzania na wakenya wengi.
 
Ikiwa hana work permit na social security number aliwezaje kuendesha truck mkuu?, Manake hata driving license hawezi kupata bila ya hivyo vitu. Muulize yupo tayari kuhama state nyengine kufanya kazi hio chini ya meza. Niongee na wasela wangu kule


Ndukiiiii [emoji2089][emoji2089][emoji2089]
Ndio anaweza kuhama mkuu
 
Back
Top Bottom