Imani yangu inanambia utafanikiwa mkuu, nia uliyoiweka lazima itakuwa na njia. Cha muhimu tu sala na kumtanguliza Mungu kwa kila hatua unayotaka kupiga.Ahsante sanq Mkuu,niombee nifanikiwe kwa hili.
Ahsante sana Mkuu,kariakoo anapatikana mtaa gani?.
Hongera Kiongozi,naimani kuwa ipo siku nitatoka pia!!.Nipo hapa Allepo libya tunapambana na hali zetu, huku ni weekend kula tu bata pande za hizi
Amen mpiganaji,watu wenye michango chanya kama wako ni wachache kiongozi,Ahsante kunitia sana moyo.Imani yangu inanambia utafanikiwa mkuu, nia uliyoiweka lazima itakuwa na njia. Cha muhimu tu sala na kumtanguliza Mungu kwa kila hatua unayotaka kupiga.
Mkuu huyo agent si ni wale wale wa 14 days?
Ahsante kiongozi,ngoja nijaribu kesho,maana nimetoka Airport saa hizi,nimeambulia patupu,maagent wengi ni wa 14 days tu,sijafanikiwa.Maajent ni wengi mkuu.
Maajent wengine watakwambia upate mdhamini kama hujawah kufika dubai jaribu kumwambia unakwenda kibiashara mambo mengine utafanya ukifika duba.
Shukrani.Amen mpiganaji,watu wenye michango chanya kama wako ni wachache kiongozi,Ahsante kunitia sana moyo.
Ndio maana nimekuja hapa kuuliza Mkuu,maagent wengi wananiambia wanatoa visa ya siku 14 tu(Tourist Visa),na hakuna kuongeza siku pia si ruhusa kutafuta kazi kwa hiyo Visa.Ongea nao vizuri ukihitaji visa kuanzia miezi3 au miezi 6 unaweza kuongezewa harama.
Nakushauri chukua visa ukifika dubai kila kitu unafanya kuongeza muda.
Ongeza nyama MkuuDubai hata airport unapata Visa
Ukifika Airport ya Dubai kama huna visa wanatoa hapo hapo.Ongeza nyama Mkuu
Ahsante sana kiongozi,kwa hiyo nisigusie kabisa suala la kazi kipindi natafuta Visa si ndio Mkuu Daby?duke wewe nenda hata kama utapewa viza isiyohitaji kutafuta ajira ukifika tafuta hakuna atakayekufuatilia kuangalia kama unatafuta.
ya miezi 3 au miwili inakutosha kutafuta kazi.
Ahsante Mkuu!!.Ukifika Airport ya Dubai kama huna visa wanatoa hapo hapo.
Au kwa ushauri nenda kwenye Ubalozi wao
Cha muhimu ni wewe kupata data za uhakika kama ukienda na ya siku 14 unaweza kupata kazi, na kama ukipata kazi watakukubalia kubadilisha na kubaki huko huko. Ni vizuri sana upate mtu aliyeko huko akuelezee. Usikubali kuondoka bila kuwa na uhakika kwani utajikuta umerudishwa Bongo na fedha zako zimepotea bure.Ahsante Mkuu!!.
Halafu mkuu kuna huyu member wa JF yeye alifuata mkondo huo huo unaotaka kufuata. Soma hii thread aliyoeleza jinsi alivyokwenda na masaibu aliyopata ili ufanye uamuzi wa busara. Jaribu ku-PM ni mtu member ambaye anaona yuko wazi sana atakakupa maarifa zaidi. Thread yake ni hii: Hatua nilizopitia mpaka kufika Ukraine, na bado niko njiani kwenda nchi ya ahadi NorwayShukrani Boss!!.
usigusie hata kidogo.... ila sisitiza unahitaji ya kuanzia two month.Ahsante sana kiongozi,kwa hiyo nisigusie kabisa suala la kazi kipindi natafuta Visa si ndio Mkuu Daby?
Kwl Mkuu,ndiyo maana nimeandika kama kuna mtu aliyeko Dubai angenipa taarifa kamili ingenisaidia sana!!.Cha muhimu ni wewe kupata data za uhakika kama ukienda na ya siku 14 unaweza kupata kazi, na kama ukipata kazi watakukubalia kubadilisha na kubaki huko huko. Ni vizuri sana upate mtu aliyeko huko akuelezee. Usikubali kuondoka bila kuwa na uhakika kwani utajikuta umerudishwa Bongo na fedha zako zimepotea bure.
Achana na nchi yako. Kajenge uchumi wako binafsi. "nchi" ni mwanamke mgumu sana na wanamtumia vibaya sana. Pambana mkuu, na hivi bado upo single, time ni sasa.Ni wazo zuri kiongozi,nimeshajaribu pia,kuhusu kujenga uchumi wa nchi yangu,naimani hata nikiwa huko bado naweza kuujenga,si lazima niwe hapa hapa nchini Mkuu!!.