Wakati mwanzilishi wa thread akisubiri kupata msaada alioomba na mimi naomba kwa mwenye kufahamu jina la wimbo na la mwimbaji wa wimbo wenye maneno yafuatayo:
...Bwana wangu, bwana wangu mwokozi.
Ninakupa, maisha yangu....
Mimi hivi, hivi nilivyo,
Ninakupa, maisha yangu.....
Nakumbuka tu kwamba wimbo wenyewe umeimbwa na mwanaume na mtangazaji George Kanuti Njogopa aliyekuwa Clouds FM alikuwa akipenda sana kuupiga wimbo huo katika kipindi cha Gospel Songs (Gospel Music?) siku za Jumapili. Hiyo ilikuwa 2006-2007 kama sikosei.
Natanguliza shukurani wandugu.