Mchana
Senior Member
- Sep 27, 2007
- 183
- 16
Wakuu ninayo Ipad2 3G ,inatumia line ya Airtel Microsim card. Microsim yenyewe ni simcard ya kawaida ambayo imekatwa kuipunguza,,kwani wao hawana sim card hizi ndogo. Tatizo ni kuwa ipad haina function ya simu ili niongeze salio na kununua kifurushi cha internet let say 400MB. Kabla sijaikata na kuiweka kwenye Ipad ilikuwa inatumika kwenye simu ya kawaida ambapo nilikuwa nimenunua kifurushi cha internet. Hivi sas kifurushi kimekwisha na siwezikuirudisha line kwenye simu ya zamani kwani imeshakatwa na haitakaa tena simu ya kawaida. Je wataalamu, ikiwa ni pamoja na watu wa Airtel humu jamvini mnanishaurije? Naomba msaada!