msaada,gari hii nitaitoa bandarini kwa Tsh ngapi?

kwa kweli kama doc ziko kamili sioni kwa nini utoe rushwa. Kwa sasa unajua unachotakiwa kulipa na una hiari ya kuweka pingamizi iwapo haukubaliani na hesabu ya afisa wa kodi, zamani ingekuchukua wiki nzima malalamiko yako kushughulikiwa jambo ambalo liliongeza gharama za storage.
Angalizo: Iwapo invoice value ni kubwa kuliko tra calculation, invoice value will apply.
Sasa kuwepo ama kutokuwepo kwa rushwa bandarini ni mjadala mwingine, kumbuka bandari ni taasisi tofauti na tra.



Sijui kama diy - "do it yourself" inawezekana ila nijuavyo mfumo wa sasa unakulazimisha kupitia kwa clearing agent coz ndiye mwenye leseni ya uondoshaji mizigo idara ya forodha.
Niliwahi kusikia kwamba muda nao ni pesa, kutoa gari bandarini inachukua wastani wa siku 7. Ikiwa nitafanya mwenyewe manake zaidi ya siku 7 nisimamishe ratiba zingine. I would rather pay someone for that.



Hoja yangu ilizungumzia kukopa ili kuongeza kipato/ufanisi (sio kuwa pale pale) na imekaa kijasiriamali zaidi ambapo inakosa mashiko ukiitazama kwa jicho la "ponda mali kufa kwaja"....
Mwisho wa siku kila mtu amejiwekea kanuni za kiuchumi/maisha. Kwa nini unahitaji gari ndio itakuwa sababu ya kununua gari...
umewahi kusoma/kusikia nadharia ya hierarchy of needs???
450px-maslow%27s_hierarchy_of_needs.svg.png

kiongozi salute..nisameehe kama nitakuwa naonyesha kiwango cha juu cha uvivu wa kumtafuta elimu...hivi hii kitu niliyobold in blue katika mada yako ndio umei-present kwa hiyo pyramid diagram hapo chini?...ni kitu gani hasa na inahusiana nini na maisha ya kila siku ya kila mwanadamu anayeishi chini ya jua?

Shukrani mbele..na kuuliza sio ujinga bali njia ya kujifunza zaidi.
 
Mimi nimenunua 2 bila Paytrade ila ushauri wako ni mzuri kama sio mzoefu usi risk kununua bila Paytrade ila wazoefu wanazichukua tu bila paytrade kuna kampuni kubwa mule zinazoaminika

Yap kwa wazoefu haina tatizo lkn kwa njuka anayeanza anaweza aka-negotiate deal na wapopo akapigwa madafu yake....
 
kiongozi salute..nisameehe kama nitakuwa naonyesha kiwango cha juu cha uvivu wa kumtafuta elimu...hivi hii kitu niliyobold in blue katika mada yako ndio umei-present kwa hiyo pyramid diagram hapo chini?...ni kitu gani hasa na inahusiana nini na maisha ya kila siku ya kila mwanadamu anayeishi chini ya jua?

Shukrani mbele..na kuuliza sio ujinga bali njia ya kujifunza zaidi.

Kiongozi
Mwuliza swali alitaka kujua iwapo usafiri wa daladala unamwezesha kufika mahala pa kazi kwa wakati na ufanisi ukawa pale pale itamaanisha asinunue gari, kwamba yeye awe dala dala tuuu??

Pyramid nilopaste ni nadharia ya Hierarchy of Needs (ya Abraham Maslow): Kwa muktadha wa nadharia hiyo nilitaka kumwonyesha ni vipi kutimizwa kwa hitaji moja la chini huzaa hitaji jingine la juu kidogo hivyo sio lazima iwe kama nilivyosema awali kwamba "gari iwe kwa ajili ya kukuongezea kipato au ufanisi wa kazi"...pengine ukiwa na gari inakupa kukubalika (belong) zaidi ktk jamii..

Inamaanisha kuna msukumo wa mahitaji unaosababisha tufanye tunayofanya na ndicho kinatufanya kupishana...msukumo wa kupata gari nilonao ni tofauti na msukumo wa kuwa Rais alonao Ed Lowasa (sasa ninaingiza siasa kwenye thread ya kutoa gari bandarini)....turudi.
 
Sijui kama DIY - "Do It Yourself" inawezekana ila nijuavyo mfumo wa sasa unakulazimisha kupitia kwa clearing Agent coz ndiye mwenye leseni ya uondoshaji mizigo idara ya forodha.
Ahsante sana, nimeelewa ni kwa nini lazima upitie kwa agent.

Angalizo: Iwapo invoice value ni kubwa kuliko tra calculation, invoice value will apply.
Invoice value ndio kitu gani???

Kwa kweli kama doc ziko kamili sioni kwa nini utoe rushwa.
Kwani watu wanapotoa rushwa TRA ni kwa vile doc haziko kamili?

Kwa hiyo kama nina upungufu wa makaratasi naweza kutoa rushwa na nikashushiwa kodi vile vile, sio? Ikimaanisha kwamba afisa wa TRA bado ana nafasi ya kuchakachua mfumo, tena nikiwa sina makaratasi ndio poa zaidi, sio? hahahahaaa....

Usinambie huo ni mjadala mwingine. Wewe ndio mwanzoni ume introduce concept ya kwamba siku hizi mambo ni mazuri zaidi kwa vile katika mfumo mpya kuna fixed formulae za makadirio zilizo wazi, afisa wa TRA hakufanyii tathmini kivyake, yani upenyo wa rushwa. Sasa unaulizwa, kwa hiyo siku hizi rushwa hakuna, unaanza oooh...huo ni mjadala mwingine... oooh TRA na Bandari ni vitu viwili tofauti, khaa! Tunaongelea (tena wewe ndio umeanza kuongelea hilo) tunaongelea rushwa zinazohusiana na kuingiza gari, rushwa za TRA, idara ya Customs! Ni topic hii hii! Kwani topic yetu ya ushuru wa kuingiza magari hapa ina deal na idara gani, SUMATRA?

Hoja yangu ilizungumzia kukopa ili kuongeza kipato/ufanisi (sio kuwa pale pale) na imekaa kijasiriamali zaidi ambapo inakosa mashiko ukiitazama kwa jicho la "Ponda mali kufa kwaja"....
Sawa kabisa, kwa hiyo kama huna nia ya kulifanyia gari ujasiriamali, na huna nia ya kutumia gari kuongeza kipato wala ufanisi (unaweza kuwahi kazini kwa dala dala na ufanisi ukawa pale pale), ina maana katika mazingira hayo usi finance gari? Uishi kwenye vibajaji na magobole ya Mwenge-Mbagala maisha yako yote? Jibu swali, usichore ma pyramid!
 
mimi sijaelewa hapa yani hiyo Tsh. 6,845,310 ni itakayo mkosti kama kodi tu, ukitoa CIF au inclusive coz CIF yenyewe inazidi hiyo ulotaja ...ufafanuzi mkuu miye nataka kununua gari ila nashindwa pakupata maelezo sahihi. nisije lifikisha hapa likanishinda
...Tuko pamoja mkuu kwa kweli hata mimi hapa huwa pananipa utata sana. Maana hawa waheshimiwa wa kodi (TRA) wanadai wao hutafuta bei ya hiyo inapokuwa mpya kabisa then huendelea na estimates za kodi....
 
Ahsante sana, nimeelewa ni kwa nini lazima upitie kwa agent.

Invoice value ndio kitu gani???

thamani ya bidhaa uliyonunua huonyeshwa kwenye ankara/invoice au stakabadhi/receipt.

Kwani watu wanapotoa rushwa TRA ni kwa vile doc haziko kamili?

Doc zikiwa pungufu (mf. huna inspection cert) unajenga mazingira ya kuombwa/kutoa rushwa maana kuna faini.....

Kwa hiyo kama nina upungufu wa makaratasi naweza kutoa rushwa na nikashushiwa kodi vile vile, sio? Ikimaanisha kwamba afisa wa TRA bado ana nafasi ya kuchakachua mfumo, tena nikiwa sina makaratasi ndio poa zaidi, sio? hahahahaaa....
Nadhani rushwa inaongeza gharama kwa mlipa kodi (ktk muktadha huu) ila unaweza kujaribu maana tanzania kila kitu kinawezekana...

Usinambie huo ni mjadala mwingine. Wewe ndio mwanzoni ume introduce concept ya kwamba siku hizi mambo ni mazuri zaidi kwa vile katika mfumo mpya kuna fixed formulae za makadirio zilizo wazi, afisa wa TRA hakufanyii tathmini kivyake, yani upenyo wa rushwa. Sasa unaulizwa, kwa hiyo siku hizi rushwa hakuna, unaanza oooh...huo ni mjadala mwingine... oooh TRA na Bandari ni vitu viwili tofauti, khaa! Tunaongelea (tena wewe ndio umeanza kuongelea hilo) tunaongelea rushwa zinazohusiana na kuingiza gari, rushwa za TRA, idara ya Customs! Ni topic hii hii! Kwani topic yetu ya ushuru wa kuingiza magari hapa ina deal na idara gani, SUMATRA?
Ndugu naona unataka ligi tuu: unaulizaje RUSHWA HAKUNA idara ya forodha wakati kabla yake nishasema doc zikiwa pungufu unajenga mazingira ya rushwa (kuombwa au kutoa).
Swali lako la awali lilikuwa RUSHWA BANDARINI HAKUNA??? WAPI HAKUNA RUSHWA nchi hii??? (Sitaki unijibu)

Sawa kabisa, kwa hiyo kama huna nia ya kulifanyia gari ujasiriamali, na huna nia ya kutumia gari kuongeza kipato wala ufanisi (unaweza kuwahi kazini kwa dala dala na ufanisi ukawa pale pale), ina maana katika mazingira hayo usi finance gari? Uishi kwenye vibajaji na magobole ya Mwenge-Mbagala maisha yako yote? Jibu swali, usichore ma pyramid!
NAREJEA JIBU: "Hoja yangu ilizungumzia kukopa ili kuongeza kipato/ufanisi (sio kuwa pale pale) na imekaa kijasiriamali zaidi ambapo inakosa mashiko ukiitazama kwa jicho la "ponda mali kufa kwaja"....
Mwisho wa siku kila mtu amejiwekea kanuni za kiuchumi/maisha.
Kwa nini unahitaji gari ndio itakuwa sababu ya kununua gari... "

Majibu hapo juu hayaongelei kuto Finance bali ni wapi financing inatoka i.e MKOPO (ingawa kuna mikopo isiyo na riba)....Kama umepewa hela na mjombako unataka mimi ndo nikupangie nini cha kufanya???

Niwie radhi kwa kuchora pyramid
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom