Msaada: Gari gani linakula mafuta kidogo?

kikaniki

JF-Expert Member
Nov 20, 2014
502
938
Wadau! Ninaishi Chanika na ninafanya kazi Kariakoo. Ninamiliki Rav4 lakini naona inanielemea kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta.

Ombi langu kwenu: Nataka kununua gari lenye CC chache ambalo halitanigharimu sana katika matumizi ya mafuta. Kupitia mawazo yenu, naweza kufikia uamuzi wa gari gani ninunue. CC 650 (gari kama Pajero mini, Suzuki Jimny) hadi CC 1500 ni muafaka zaidi.

Nawasilisha.
 
Unaweza ukakwepa bei ya mafuta ukaingia bei ya matengezo.

Baki Toyota hapo hapo.

Chukua (1) IST ila uko Chanika lazima utaamka siku imeibwa au imevuliwa kila kitu.

(2) Paso kama wewe dereva mzuri na utaridhika na ile shape mbaya.

(3) Runx/Alex kama haukai madongo kuinama sana.

JITU LA MIRABA MINNE
Mpaka hapo sina cha kuongeza mkuu umemshauri vyema.
 
7DCDD707-C5DB-4496-8495-955CDE2AA537.png
 
Few
Wadau! Ninaishi Chanika na ninafanya kazi Kariakoo. Ninamiliki Rav4 lakini naona inanielemea kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta.

Ombi langu kwenu:-Nataka kununua gari lenye CC chache ambalo halitani-cost sana katika matumizi ya mafuta. Kupitia mawazo yenu, naweza kufikia uamuzi wa gari gani ninunue. CC 650 (gari kama Pajero mini, Suzuki Jimny) hadi CC 1500 ni muafaka zaidi.

Nawasilisha
cc is 650
 
Gari inayokula mafuta kidogo ina horse power ya 58 na ni pajero mini cc650 bro ile ni taka taka.

Tuache mawazo ya kimaskini na uoga wa maisha, hicho kigari kina cylinder 3 jichanganye ukinunue, kikianza kuzingua utapiga trip za garage mpaka mafundi watakukimbia.

Ni afadhali ukanunua bajaji au boda boda 4 zikakupa hela ukaachana na hicho kidude.

Atleast tafuta gari ya cc 1200 and above itaweza kukusogeza na shida zako.
 
Sasa hivi, Toyota Vitz

Imekua ni chaguo la wengi sana.
Mfano mzuri ni hii ambayo tulimuagizia mteja hapa

Zimekuwa ni chaguo la wengi kwasasa.
Gharama ni TZS 9.8MIL pamoja na usajili.
 

Attachments

  • IMG_20220305_114026_017.jpg
    IMG_20220305_114026_017.jpg
    630.4 KB · Views: 88
Wadau! Ninaishi Chanika na ninafanya kazi Kariakoo. Ninamiliki Rav4 lakini naona inanielemea kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta.

Ombi langu kwenu:-Nataka kununua gari lenye CC chache ambalo halitani-cost sana katika matumizi ya mafuta. Kupitia mawazo yenu, naweza kufikia uamuzi wa gari gani ninunue. CC 650 (gari kama Pajero mini, Suzuki Jimny) hadi CC 1500 ni muafaka zaidi.

Nawasilisha
Chukua Suzuki Jimny. Roho ya Paka ile...
 
Back
Top Bottom