Bwana Chiniko
Member
- Jul 18, 2016
- 20
- 9
Kwa mara nyingine tena, nimeona nimalize kiu na utata uliokuwa ukinisumbua kwenye kichwa changu kwa muda mrefu.
Mada mezani ni kati ya Bmw 5Series 2007 na Toyota Crown Athlete 2008, ishu imekuja kufuatia ubishani uliotekea baina ya magari haya mawili ya kampuni tofauti.
Nikianzia na BMW 5series, wapo waliosema kumiliki gari aina ya Bmw alafu ukawa nayo moja ni hatari sana hasa kwa mazingira ya bara letu la Africa.
Akidai ya kwamba joto na hali halisi kwa ujumla, hupelekea magari aina ya Bmw kushindwa kuhimili, ndio maana wamiliki wengi wa Bmw huwa wanakuwa na magari mengine ya ziada hasa kutokana na gari hilo kuwa la kilakshari zaidi.
Akaenda mbele zaidi na kudai kwamba hata service zake na vifaa vyake ni ghali zaidi, ndio maana unakuta kwenye baadhi ya magarage unakutana na Bmw bado inadai lakini imekufa tofauti na magari ya kampuni nyingine.
Akamalizia kwa kusema kwamba Bmw 5series toleo la mwaka 2007 hata kwa bei huwezi kulinganish na Crown Athlete, akiwa na maana ya kwamba Crown ipo juu zaidi ya Bmw 5series.
Pia Crown inauwezo mkubwa wa kuhimili hali ya hewa ya bara la africa na unaweza ukawa nayo moja na ukaitumia pasipo wasiwasi wowote hasa ukizingatia kampuni ya Toyota imekuwa rafiki sana wa kukopi na mazingira ya bara letu.
Nimeambatanisha picha na sifa za magari tajwa na specifications zake. Wajuvi wa mambo nahitaji mnisaidie mawazo yenu katika hili pia.
Nawasilisha
Mada mezani ni kati ya Bmw 5Series 2007 na Toyota Crown Athlete 2008, ishu imekuja kufuatia ubishani uliotekea baina ya magari haya mawili ya kampuni tofauti.
Nikianzia na BMW 5series, wapo waliosema kumiliki gari aina ya Bmw alafu ukawa nayo moja ni hatari sana hasa kwa mazingira ya bara letu la Africa.
Akidai ya kwamba joto na hali halisi kwa ujumla, hupelekea magari aina ya Bmw kushindwa kuhimili, ndio maana wamiliki wengi wa Bmw huwa wanakuwa na magari mengine ya ziada hasa kutokana na gari hilo kuwa la kilakshari zaidi.
Akaenda mbele zaidi na kudai kwamba hata service zake na vifaa vyake ni ghali zaidi, ndio maana unakuta kwenye baadhi ya magarage unakutana na Bmw bado inadai lakini imekufa tofauti na magari ya kampuni nyingine.
Akamalizia kwa kusema kwamba Bmw 5series toleo la mwaka 2007 hata kwa bei huwezi kulinganish na Crown Athlete, akiwa na maana ya kwamba Crown ipo juu zaidi ya Bmw 5series.
Pia Crown inauwezo mkubwa wa kuhimili hali ya hewa ya bara la africa na unaweza ukawa nayo moja na ukaitumia pasipo wasiwasi wowote hasa ukizingatia kampuni ya Toyota imekuwa rafiki sana wa kukopi na mazingira ya bara letu.
Nimeambatanisha picha na sifa za magari tajwa na specifications zake. Wajuvi wa mambo nahitaji mnisaidie mawazo yenu katika hili pia.
Nawasilisha