Msaada ameyakanyaga Bank ya ABC

Tafuta Wakili atakupa ushauri mzuri zaidi, ila mimi nashauri akatae kuchukua hela kwa sababu bank wamekiuka masharti ya mkataba wa mpoko hela ilitakiwa kutoka ndani ya saa 24, imetoka nje ya muda mambo yake yameshindwa kufanyika kwa wakati....

Awaonyeshe jeuri zaidi aombe compersation aseme alikuwa na biashara na iyo hela ilikuwa ya kuagiza mzigo ambao ungeuzwa sikukuu mzigo ameuza kwa hasara sababu alichelewa kupata pesa kutoka ABC aombe 20M kama hasara aafu aacue mahakama iamue 😂

NB:Tafuta wakili mwenye roho mbaya
 
Maombi ya mkopo si jinai kuwa lazima uadhibiwe hata ukighairi. Aende pale na barua rasmi na bank statement kuwa haitaji tena sababu ya muda mkopo umechelewa mpaka anaandika barua haujaingia na ushahidi ni BS yake. Barua ieleze wazi tarehe aliyoomba mkopo na muda uliopita na haitaji tena sababu dirisha la alichotaka kufanya na hiyo pesa limefungwa na kuichukua hiyo pesa ni kutengeneza non-performing loan.

Wakilazimisha asichukue pesa wala asipeleke marejesho na atoe taarifa BOT kwa maandishi kuwa analazimishwa kukopeshwa watachukua pesa yao.
 
Wazo zuri ila nina wasi wasi maana awali aliisha saini kuomba mkopo.....?
 
🤔🤔🤔 ....Ok nalo ni wazo ntamueleza kama wakimsumbua, aangalie upande huu
 
Wazo zuri ila nina wasi wasi maana awali aliisha saini kuomba mkopo.....?
Sawa ila hawakuuweka ndani ya muda unaohitajika. Bank haiwezi kulazimisha iwapo utapeleka barua rasmi ya kufuta maombi ya mkopo kabla hujawekewa mkopo. Na hata angekuwa kawekewa ila hajachukua still anaweza ghairi japo ataingia gharama kidogo ya riba ya mwezi ambayo ni chini ya 3%.
 
Shukrani sana, maana nimeanza kupata pa kumfarijia.
 
Asante sana rafiki, itabidi kuanza na namba maana s l.p hadi barua kufika siyo leo wala kesho.
 
Ok, licha ya kuwa wanamwambia imeenda hazina.... mimi nilimshauri aende polisi kupata zuio la mkopo, vipi hapo?
Ushauri uliopewa ndiyo sahihi.

Polisi na mambo ya mikopo haihusiki bwashee. Na wala hawawezi kuzuia, hata umpelekee IGP.

Nenda kwa HR wako, aandike barua ya mtumishi wake kusitisha maombi ya mkopo. Aeleze wazi sababu ni kuchelewa. Kisha agonge muhuri.

Toa copy ya barua husika. Fikisha kwa Loan department ya benki husika au kwa meneja.

Kisha wataongea watakachoongea.
 
Shukrani
 
Asante sana rafiki, itabidi kuanza na namba maana s l.p hadi barua kufika siyo leo wala kesho.
Achana na mambo ya BOT kwa sasa.

Unachopaswa kufanya ni kumalizana nao. Kuna time frame ya kumalizana na endapo mtashindwana basi swala lako ndilo unali-file BOT.

Ukiwapigia BOT watakuambia hivyo hivyo. Fuata taratibu. Usiruke hatua.

Aanze benki husika, awape muda. Wakikataa ndiyo unawaambia kabisa nina lengo la kufile malalamiko yangu BOT.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…