Mrisho nyuma!

Mrisho nyuma!

Kaka kama aliweza kupanua miguu yake akaingiliwa na mwanaume mwingine wakati mko katika mahusiano(sio kwamba labda mlipotezeana kwa muda) MPIGE CHINI!!!

Amini nakwambia ukiwa nae itakuwa inajirudia rudia kichwani mwako ukiwaza na itapelekea usimpende na hata utajikuta una mahusiano na wanawake wengine kupunguza hasira zako.

Songa mbele, kama pressure ya mama yake kaisababisha yeye mwenyewe na anastahili kupata adhabu yake.

Nilipoangalia ID yako na signature yako nikakumbuka kile kitabu cha "Mkimbizi"... Hivi huyu mwandishi aliwahi kuandika tamthiliya nyingine?
 
Wewe je haugongi nje????? kama hufanyi hivyo mpige chini ila kama ni tofauti vumilia kwani mla vya wenzie na vyake shurti viliwe ati!!!!
 
Wadau, jana niliwaombeni ushauri juu ya binti ambaye alikuwa mchumba wangu, lakini hakuwa mwaminifu, alilala kwa mwanaume mwingine toka ijumaa hadi jumapili na baadae kuja kuomba msamaha!

Leo, nataka kuwapa feedback-kwanza ile jana dada wa binti alijitahidi mpaka akaonana na mimi japo nilijitahidi sana kujenga mazingira ya mimi kuto kukutana na yeye, alipo fika tukaongea kwa kirefu juu ya mdogo wake, na yeye alikiri kwamba mdogo wake hakuwa mwaminifu, lakini wamekwisha mweka chini na wamemsema sana! Nikamwambia nashukuru kwa kulitambua hilo kwani hata mimi nilienda pale hostel bila taarifa kwani nilisha pata hizo habari za yeye kutoka kila ijumaa, hivyo nikamwambia mimi basi tena! Akajitahidi sana kunishawishi nibadili msimamo, lakini nikamgomea!

Leo hii, binti amewahi ofisini kwangu kuliko hata mfagia ofisi, nakuja nimemkuta amekaa nje ananisubiri, alipo niona tu akaanza kulia na kunishika miguu eti nimsamehe, nikamtimulia mbali, akaenda kwa bosi wangu (ni mama) kumwelezea kila kitu, amemwomba eti amsaidie kunisii mimi nimsamehe, eti ni marafiki zake walimdanganya, hata kaa arudie tena! Na ameomba sana hili swala mama yake asijue, eti anapressure anaweza kupata matatizo! Sasa huyu mama amesema niende ofisini kwake saa 8, na anaonekana anataka kunishawishi nisamehe, na mimi sipo tayari kusamehe, wadau ushauri wenu please!
Binti bado yupo hapa around, yupo kama amechanganyikiwa tena sana, kiukweli nimemsaidia sana yeye na familia yake kiuchumi, tangu akiwa kidato cha tano hadi sita, then first year hadi sasa yupo third year!

We ushaona mtu si muanifu! achana nae, kama anakusumbua sana, mwambie matendo yake ndio yatakurudisha ila ushamsamehe! unampa 5yrs ya kumchunguza
 
Nilipoangalia ID yako na signature yako nikakumbuka kile kitabu cha "Mkimbizi"... Hivi huyu mwandishi aliwahi kuandika tamthiliya nyingine?

Aliandika, MTUHUMIWA, MDUNGUAJI!! Namtafuta saana jamaa aisee
 
tabia ni kama ngozi, kama marafiki zake walimshawishi atoke, kesho watamshawishi akuue. na kama unataka maumivu zaidi ya ayo msamehe uone. wajanja hao analia hapo tu anajua kitumbua chake kimeingia mchanga. huyo bosi wako mwambie ayo masuala binafsi mtayamaliza. ila siku zote MAPENZI HAYANA USHAURI USIJE UKAWA NA WEWE NDO UMEOZA HAPO SI TWABWABWAJA HAPA) FUATA HISIA ZAKO USIFUATE MACHO YAKO KAKA.
 
Tafuta muda wa kutafakari kwanza kwa kina, husifanye kitu kwa shinikizo au mawazo ya wengi. Nafsi yako ikushuhudie mwenyewe kutoa msamaha au kuacha kabisa. Ili husije kuendelea kuwa na donda lisilopona maishani mwako kwa kukumbuka yaliyopita.
 
Mkuu nakushauri kitu kimoja ili kupunguza uchungu wa misaada yako kwake mpige mimba kwanza halafu ndoa hakuna hii ni muhumu sana kwa afya ya akili yako.kwani usipofanya hivyo sasa halafu mtu mwingine amtupie mimba hakika itakuuma zaidi ya hii ya kugongwa nje.
 
Wadau, jana niliwaombeni ushauri juu ya binti ambaye alikuwa mchumba wangu, lakini hakuwa mwaminifu, alilala kwa mwanaume mwingine toka ijumaa hadi jumapili na baadae kuja kuomba msamaha!

Leo, nataka kuwapa feedback-kwanza ile jana dada wa binti alijitahidi mpaka akaonana na mimi japo nilijitahidi sana kujenga mazingira ya mimi kuto kukutana na yeye, alipo fika tukaongea kwa kirefu juu ya mdogo wake, na yeye alikiri kwamba mdogo wake hakuwa mwaminifu, lakini wamekwisha mweka chini na wamemsema sana! Nikamwambia nashukuru kwa kulitambua hilo kwani hata mimi nilienda pale hostel bila taarifa kwani nilisha pata hizo habari za yeye kutoka kila ijumaa, hivyo nikamwambia mimi basi tena! Akajitahidi sana kunishawishi nibadili msimamo, lakini nikamgomea!

Leo hii, binti amewahi ofisini kwangu kuliko hata mfagia ofisi, nakuja nimemkuta amekaa nje ananisubiri, alipo niona tu akaanza kulia na kunishika miguu eti nimsamehe, nikamtimulia mbali, akaenda kwa bosi wangu (ni mama) kumwelezea kila kitu, amemwomba eti amsaidie kunisii mimi nimsamehe, eti ni marafiki zake walimdanganya, hata kaa arudie tena! Na ameomba sana hili swala mama yake asijue, eti anapressure anaweza kupata matatizo! Sasa huyu mama amesema niende ofisini kwake saa 8, na anaonekana anataka kunishawishi nisamehe, na mimi sipo tayari kusamehe, wadau ushauri wenu please!
Binti bado yupo hapa around, yupo kama amechanganyikiwa tena sana, kiukweli nimemsaidia sana yeye na familia yake kiuchumi, tangu akiwa kidato cha tano hadi sita, then first year hadi sasa yupo third year!
Kaka hapo kwenye bold panaashiria kitu kama unatakiwa ukamuone daktari kwa tatizo la kutokuwa na akili ya kuchukua maamuzi sahihi. Uamuzi wa kuleta uzi kwenye forum hauendani na tukio ulilofanyiwa, ulitakiwa wewe mwenyewe uchukue uamzi sahihi kabla hata ya watu kufahamu yaliyokusibu, inatia aibu!
 
We ushaona mtu si muanifu! achana nae, kama anakusumbua sana, mwambie matendo yake ndio yatakurudisha ila ushamsamehe! unampa 5yrs ya kumchunguza

Dah!hii kali 5 yrs???utakua umemuundia tume ya uchunguzi au???hii nimeipenda

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Dah!hii kali 5 yrs???utakua umemuundia tume ya uchunguzi au???hii nimeipenda

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
kwa kawaida mwanamke akikulilia ujue anajua wewe ni muowaji wengine alionao ni wachezeaje? sasa ukimpa 5yrs na kweli ukawa huna nia lazima atakimbia mwnyw kama hana feelings za ukweli.
 
Nilikuwa nacho cha Mtuhumiwa ila itanibidi kutafuta maana ni muda mrefu sana

Kwa hishima na taazima mkuu, hebu kitafute maana hakuna novel iliwahi kunisisimua na kunifundisha kama ile ya "Mkimbizi"... sijui nitamtafuta wapi yule mwandishi nimuombe aandike vitabu vingi...
 
Bro wangu aliniambiaga kuku akiisha Lala nje anageuka Kua kwale!! Achana na huyo msichana!!
 
Kwa hishima na taazima mkuu, hebu kitafute maana hakuna novel iliwahi kunisisimua na kunifundisha kama ile ya "Mkimbizi"... sijui nitamtafuta wapi yule mwandishi nimuombe aandike vitabu vingi...

Aisee nisamehe niliandika haraka haraka bila kusoma. Nilikuwa nacho cha Mkimbizi! Jamaa nilimtafuta nakumbuka nilienda kwake zamani pale Kinondoni nadhani karibu na Biafra just kumuulizia kuhusu kitabu cha Mtuhumiwa.

Sidhani kama alitoa kitabu!
 
ajira za siku hizi......awe na msimamo ila asiongee na jazba akaharibu kazi yake.Aonyeshe msimamo wake kwa busara.
 
Back
Top Bottom