Mrisho nyuma!

Kuteleza kupo katika maisha, ila sio kwenda kulala na bwana mwingine, tena kila ijumaa. Huyo tena si bahat mbaya bali alikusudia. Take your time man, think widely then decide precisely
 
Usaliti unauma sana sana.Wewe msamehe na kama wadau wengine walivyosema,akapime vvu na akupe muda wa kufanya maamuzi.Kwani ingekuwa mmefunga naye ndoa hapo ndipo pangekuwa pagumu kuachana.
 
Binti bado yupo hapa around, yupo kama amechanganyikiwa tena sana, kiukweli nimemsaidia sana yeye na familia yake kiuchumi, tangu akiwa kidato cha tano hadi sita, then first year hadi sasa yupo third year!

Mwambie umesamehe na MSAADA utaendelea kutoa kama kawaida ila uhusiano wenu basi.
naaamini atakubali kwani shida yake ni huo msaada na sio kuwa nakupenda.

endelea kumsaidia kwani amebakiaza muda mchache sana ajiriwe na akipata kazi basi majukumu ni yake.
 
Usaliti unauma sana sana.Wewe msamehe na kama wadau wengine walivyosema,akapime vvu na akupe muda wa kufanya maamuzi.Kwani ingekuwa mmefunga naye ndoa hapo ndipo pangekuwa pagumu kuachana.

Huyu afugiki kwani kinachomfanya alie ni huo msaada tu!
 
Mkuu mtu analala kwa mwanaume mwingine ijumaa hadi jumapili halafu anasema amedanganywa na rafiki zake,aarrgh ngumu kumeza,mimi sitaki kusema ila cha kufanya unakijua wala halihitaji degree hilo kuamua,na huyo bosi wako unaweza kumkatalia vilevile,kwa kuwa hiyo ni private matter,cha msingi muhakikishie bosi kuwa haita athiri utendaji wako wa kazi,ila huyo mtu hakufai.
 
Huyo ni malaya kabisa. Tena utakuta anao wa kupangwa toka Ubungo hadi Kigoma.
Mi nakushauri piga chini huyo hana lolote kwako. Mwambie majuto ni babu.
Tena ningekuwa ni mimi ningempiga kama mpira ndo aondoke. Kama anasema kadanganywa na marafiki leo ina maana hata ukimwoa ataendelea kudanganywa na hao hao marafiki zake wa wajinga wajinga.
Mshenzi kabisa huyo. Nitumie namba yake nimtukane laivu. Mabinti wanatafuta waume wa kuwaoa yeye anachezea nafasi.
 

Nadhani sapoti uliyompa hadi kufikia hapo inatosha na inabidi amshukuru Mungu.
Btw kwani mmeshakula kiapo kuwa ni kifo tu ndicho kitawatenganisha? Sioni sababu ya kuachana naye, itamsaidia ktk mahusiano yake na mwingine mbele ya safari atakuwa mke bora na mwaminifu kwa mume wake.
 

duh!! give her a kiss of death,not all goodbyes are said in words..
some by silence and marching orders as Judas did to Christ..
wewe sio mwokozi wa maisha yake wala usitake kutuaminisha hilo.kama zanigua we tembea mbio tuu..
wadau washasema sana hapa
unachotaka ni kuamrishwa jibu..,you just met,you did your naivety part of life drama.let others kill the play.
you're not the only actor in the stage homie..let others take care of that too.
yangu mi ni hayooo,samahani kwa metaphoric language of mine..
 

Mama, huyo dada sio mkewe, ni rafiki mchumba/ mke mtarajiwa. Hakuna agano la "hadi kifo kitutenganishe" hapo, so kama ni kipindi cha matazamio ameshafeli sasa ya nini kujitia majaribuni? Akimwacha naamini litakuwa somo tosha kumfanya huyo dada awe mwaminifu kwa mumewe wa baadaye.
 
Naomba samahani, mi ndo nilikuwa naye na tulianza tangu mwaka juzi. Kwa kweli binti anaweza mambo na yeye anasema hatatuacha maana katupanga kama ifuatavyo;
Mimi ni ni mgegedaji.
SINAI ni mrekebisha mambo yote ya uchtmi.
Yupo jamaa mwingine,yeye ni wa masuala ya kitaaluma zaidi.
Mwingine Lecture. Yeye ni handsome kuliko sisi wengine wote.
Kwa kweli kati ya wote, mimi ndo nafaidi mautamu maana nimepangiwa siku 3 kwa wiki wakati wenzangu wote wana siku moja moja tu kwa wiki.
NAOMBA SAMAHANI SANA MME MWENZANGU SINAI. TATIZO TUKO WENGI SANA KWA HUYU MDADA. USIJITOE, TWENDELEE TU KILA MTU KWA NAFASI YAKE ILA KUMBUKA TU KUTUMIA KONDOM. Over
 

Dada, huyo alikuwa mumeo na una watoti naye.
Huyu aliyeleta mrejesho ni rafiki/ mchumba/ mke mtarajiwa. Kujiingiza kichwa kichwa ati atakuja kuwa mwaminifu siku akimuoa ni kujitia majaribuni. Labda haombi sala ya "Baba yetu...na usitutie majaribuni bali utuepushe na yule mwovu".
Yawezekana ndio hapo Mungu amemwepusha na yule mwovu.
 
Last edited by a moderator:
Kaka kama aliweza kupanua miguu yake akaingiliwa na mwanaume mwingine wakati mko katika mahusiano(sio kwamba labda mlipotezeana kwa muda) MPIGE CHINI!!!

Amini nakwambia ukiwa nae itakuwa inajirudia rudia kichwani mwako ukiwaza na itapelekea usimpende na hata utajikuta una mahusiano na wanawake wengine kupunguza hasira zako.

Songa mbele, kama pressure ya mama yake kaisababisha yeye mwenyewe na anastahili kupata adhabu yake.
 

Bado huna ndoa weye, ndo maana wasema hivyo.
Nilipokuwa sijaoa nilikuwa na mawazo kama yako. Baada ya kuoa na kuwa mtu mzima, na majaribu ninayopitia naona any one is vulnerable and can fall in adultery-especially men. Kama Mungu alitusamehe na anatusamehe why not forgive your spouse? Huwezi kumwacha mumeo au mkeo simply like that unless unfaithfullness imekuwa sehemu ya maisha yake.
Kwa bandiko la ndugu aliyeleta mrejesho, nashauri aachane naye kwa kuwa sio mkewe na hawajaingia agano la ndoa.
 
ungekuwa mwanaccm ningekushauri umng'oe kucha,kama ni mimi ningemshindilia mangumi hata huyo dadake.ulimwengu wa leo kufanya mapenzi nje ya mahusiano ni kaburi tosha.haki ya nani mtu anayekusaliti katika zama hizi ni muuaji kabisa.vipi ulale kwa mwanaume kila ijumaa mpaka jumapili halafu leo uje kwangu eti umechanganyikiwa mimi ningemuumiza.tupa kuleee kahaba huyo
 

Kumbe wewe ndo ulikosea......Ulimpenda kwa sababu ya unyonge wake kiuchumi. Na yeye alilazimika kukubali kwa kuwa hakuwa na jinsi kiuchumi. Sasa amekuwa na akili zake ameamua kuwa na mtu ambaye moyo unampenda ambaye sio wewe......Kwa hiyo kaka uanze kuzoea tu kwamba huyo dada si wako hata kama anaomba msamaha. Aanomba msamaha ni kwa vile bado anauhitaji msaada wako kiuchumi ili amalizie mwaka wake wa mwisho. Fanya kuwa ule msaada uliomsaidia yeye na familia yake ni msaada wa kawaida ni si wa kimapenzi. Pole sana kwa hilo. Tafuta mwingine ambaye si mnyonge kiuchumi utaona matatizo kama hayo hutayapata tena.
 
naunga mkono hoja!!!!!!

Poti,kesi ya gfsonwin ni tofauti na hii ya ndugu yetu Sinai. Gfsonwin anazungumzia mume wake halali aliyepewa na Mungu na wazazi wao na kuapa mbele ya watu-ni kifo tu ndicho kitawatenganisha.
 

Kama hamjui maandiko kwenye biblia inafaa kukaa kimya. Ni andiko gani kwenye biblia linaruhusu uzinzi? Huyu bwana na huyo mwanamke wake ni wazinzi kwa mujibu wa maandiko. Kwa hiyo umejaribu kutoa ushauri amwache kwa kuwa hajamwoa. Kwani kuna andiko linasema ukiwa hujafunga nae ndoa ndo umwache akizini na mtu mwingine ambaye si wewe? Au kuna andiko ukiwa umefunga nae ndoa kwa kosa kama hilo usimwache kisa ni wanandoa? Uzinzi unabaki kuitwa uzinzi tu hata kama hamko kwenye ndoa ama vinginevyo.
 

Mkuu, soma upya maoni yangu maana nadhani hujanielewa.
Lkn nakubaliana nawe, maandiko hayaruhusu uzinzi, tena ktk amri kumi, moja inasema USIZINI.
Nimeshauri kwa mleta mada kuwa aachane naye kwa kuwa si mkewe. Pia nimetofautiana na Gfsonwin kuwa kesi iliyotokea kwa mumewe akamsamehe ni sawa kwa kuwa ni mume wake na waliapa kuwa ni kifo tu ndicho kitawayenganisha.
Hizo ni scenario tofauti kabisa lkn pia kumbuka UPENDO ndio amri kuu na sio zile za "usi".
 
ukitaka kumuua nyani usimuangalie usoni, tupa kule
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…