Lucchese DeCavalcante
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 5,471
- 733
Baada ya klabu ya Yanga kukataa kumruhusu mchezaji mrisho ngasa kwenda Norway kwenye klabu ya Lov-Ham Football kuwahi usajiri wa dirisha dogo, uongozi wa Lov-ham Football uliamua kuachana na Ngasa na kumchukua Mcameroon a mbaye ndiye atakayewahi ulaji huo uliokuwa dhahiri kwa Ngasa.
Lakini juhudi za wakala wa Ngasa kuwashawishi Lov-Ham wawe na subira na waongeze pesa zaidi ya kiasi walichokubali awali cha Dola 50,000 za malipo kwa Young African F.C. Lov-Ham wamekubali kuwa na subira lakini wamekataa kuongeza pesa kwani wanaamini 50,000 USD ni nyingi kwa mchezaji wa kitanzania kutokana na ukweli kwamba hapajawahi kutokea mchezaji wa kitanzania kufanikiwa katika mpira wa kulipwa ulaya hivyo basi kumchukua Ngasa ni kama kucheza mchezo wa bahati na sibu.
Lov-Ham wamekubali kwa sharti jipya kwamba laziwa iwe mwezi huu au mwanzoni mwa mwezi ujao na safari hii atalazimika kafanyiwa majiribio kwani hakuna tena ulazima na uharaka wa kuwahi dirisha dogo kutokana na Mcameroon kuchukua nafasi ya Ngasa
Tayari Lov-Ham wameuandikia uongozi wa Yanga kama walivyoelekezwa na wakala wa Mrisho Ngasa anayetambuliwa na FIFA ndugu Yusuf Bakhresa.
Klabu ya Lov Ham Bergen ni timu iliyopo ligi daraja la kwanza (inayofahamika kama Adeccoligaen) nchini Norway na iko mji wa Bergen. Ligi kuu ya nchi hiyo inafahamika kama Tippeligaen yenye timu kongwe kama Rosenborg BK, Valerenga IF Oslo na Lillestrom SK.
Je wachezaji wetu wafanye nini ili wapete na kufanikiwa kucheza soka la kulipwa ulaya kama kina Shabani Nonda?
Lakini juhudi za wakala wa Ngasa kuwashawishi Lov-Ham wawe na subira na waongeze pesa zaidi ya kiasi walichokubali awali cha Dola 50,000 za malipo kwa Young African F.C. Lov-Ham wamekubali kuwa na subira lakini wamekataa kuongeza pesa kwani wanaamini 50,000 USD ni nyingi kwa mchezaji wa kitanzania kutokana na ukweli kwamba hapajawahi kutokea mchezaji wa kitanzania kufanikiwa katika mpira wa kulipwa ulaya hivyo basi kumchukua Ngasa ni kama kucheza mchezo wa bahati na sibu.
Lov-Ham wamekubali kwa sharti jipya kwamba laziwa iwe mwezi huu au mwanzoni mwa mwezi ujao na safari hii atalazimika kafanyiwa majiribio kwani hakuna tena ulazima na uharaka wa kuwahi dirisha dogo kutokana na Mcameroon kuchukua nafasi ya Ngasa
Tayari Lov-Ham wameuandikia uongozi wa Yanga kama walivyoelekezwa na wakala wa Mrisho Ngasa anayetambuliwa na FIFA ndugu Yusuf Bakhresa.
Klabu ya Lov Ham Bergen ni timu iliyopo ligi daraja la kwanza (inayofahamika kama Adeccoligaen) nchini Norway na iko mji wa Bergen. Ligi kuu ya nchi hiyo inafahamika kama Tippeligaen yenye timu kongwe kama Rosenborg BK, Valerenga IF Oslo na Lillestrom SK.
Je wachezaji wetu wafanye nini ili wapete na kufanikiwa kucheza soka la kulipwa ulaya kama kina Shabani Nonda?