Mrisho Gambo aongea na wanahabari

Mrisho Gambo aongea na wanahabari

Channel ten haikuonyesha kitu na walikuwapo!!Tusubiri ITV na TBC nao kabla ya kutoa nasaha zetu kwa tasnia ya habari... Ila nia aibu na inasikitisha sana
 
ITV bado taarifa haijaisha na TBC hakuna kitu, wanaonyesha uzinduzi wa nembo mpya nyekundu ya Vodacom!!! Duh!! Kazi kweli kweli, sasa ssubirini magazeti ya kesho... Tanzania, nakupenda Tanzania
 
Kama kweli UVCCM wanakitakia mema Chama chao na nchi kwa ujumla, basi wajitokeze na kutamka hadharani kuwa hawakubaliani na Ufisadi. Baada ya hapo wawataje Mafisadi hao kwa majina na nafasi zao ktk Chama, na kuwataka waondoke ktk Chama ili watu wafanye kazi za kujenga nchi badala ya kutumia muda mwingi kuchekea "upumbavu" ndani ya Chama.

Tualitaka hili lifanyike pia kwa CCM wenyewe. Kwanini munaoneana haya wakati munaangamia? Munategemea nini? Yaani Chama na nchi viangamie kwa sababu ya watu wachache saaana? Nani kasema maneno hayo? Wakati wa mageuzi ndani ya CCM ni sasa.

Wajitokeze mara ngapi? Malumbano haya si ndo yameanzishwa na waliojitokeza! CCM ni kama dala ... inaongozwa na utingo, dereva kazi yake ni kushika usukani, kukanyaga breki na kuongeza mafuta. Utingo wenyewe ni EL na RA, wakipiga bati tu wakasema shusha, dereva anabinya breki na kisha wanawatupa watu. Waliwatupa wengi huko UVCCM kwenye nafasi ya uongozi wa vijana na juzi juzi wakamshusha Sita kwenye Uspika na hata ukamanda wa vijana mkoa wa Tabora.
 
Kabla ya kikao cha uvccm mallisa alichukuliwa na bashe na milliya kwenda kwa el na ndio maana hajasema chochote kalishwa unga wa ndele
 
Mengi aliongea baada ya Dr Slaa kuwataja mafisadi papa 11 pale kidongo chekundu. Walitangaza kuwa wataenda kumshtaki lakini hakuna aliyethubutu kwenda mahakamani. Na kumuandama JK ni kwasababu nae yumo kwenye list na vilevile ni kwasababu yeye ana mamlaka kwahiyo angeweza kuwachukulia hatua mafisadi lakini anaogopa.
 
Alaa, kumbe machalii wa Arusha hawawezi kupambana hadi mazagazaga ya ccm yaje kuwasaidia? Waombe radhi wana Chadema wa arusha tafadhali. Hawahitaji walioshindikana ccm

ukisoma vizuri maelezo yangu utanielewa. Nimesema kama anafanana na cdm kiitikadi, mtazamo na msimamo basi aje ajiunge nasi tufanye kazi. Hatuangalii katoka chama gani. Cha msingi ni ulinganifu tulionao. Kama hatuna imani inayotuweka pa1, hakika hatuwezi kuwa nae. Hata Dr Slaa alikuja cdm baada ya kuona anafanana na cdm kifikra na kile tunachokiamini!
 
Kwa kweli baada ya kusoma na hii hapa chini, huyu kijana nimemkubali sana

LOWASA KATIKA HARAKA ZA KUNUNUA URAIS 2015 ameanza na Sh billioni 8
WAZIRI Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya mkataba tata wa Richmond, Edward Lowassa ameelezwa kuwa na mradi wa karibu Sh. 8 bilioni wa “kujisafisha” na kumwingiza ikulu.
Lowassa alipoulizwa na gazeti hili kuhusu mradi huo, alijibu kwa mkato, “Mimi sijui.”
MwanaHALISI limeelezwa kwamba fedha za “kumsafisha” Lowassa zimeahidiwa na swahiba wake, Rostam Aziz ambaye wamesimama pamoja muda wote wa sakata la kashfa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond iliyothibitika kuwa feki.
Richmond ilipewa mkataba wa kufua umeme ikiwa haina fedha, wataalam wala uzoefu katika eneo hilo; huku nyaraka zilizopo juu ya kashfa hiyo zikionyesha kuwa mkataba ulipatikana kwa njia ya upendeleo – tuhuma ambazo zinamwangukia Lowassa.
Taarifa zinasema mabilioni hayo ya shilingi yamelenga kutumika kulegeza wajumbe wa vikao vya maamuzi vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) hasa kuelekea, na wakati wa mkutano mkuu ndani ya chama hicho ambao utafanyika mwaka kesho.
Fedha hizo pia zinadaiwa kulenga kuyumbisha jumuiya za CCM – Umoja wa Wanawake (UWT), Jumuiya ya wazazi na Umoja wa Vijana (UV-CCM).
Wengine ambao wanadaiwa kulengwa katika hatua ya kushawishi, kulegeza na kushirikisha katika mradi wa kusafisha Lowassa ni wabunge, vyombo vya habari na waandishi wa habari mmojammoja.
“Mradi wa kumsafisha Lowassa” umeelezwa kuwa chini ya kundi la watu watano. Mbali na Lowassa mwenyewe na Rostam, wengine waliotajwa ni Andrew Chenge, Makongoro Mahanga na Peter Serukamba.
Chenge ni mbunge wa Bariadi Magharibi; Mahanga ni mbunge wa Segerea na Serukamba ni wa Kigoma Mjini. Taarifa zinasema tayari baadhi ya wajumbe wa kundi hilo wamefanikiwa kushika nafasi za juu za Kamati za Kudumu za Bunge.
Walioshika nafasi hizo ni Lowassa (Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama) na Serukamba (Miundombinu).
Gazeti hili limeelezwa kuwa mgogoro unaoendelea ndani ya UV-CCM, unatokana na “kasi ya mbio za Lowassa kugombea nafasi muhimu” ndani ya chama chake na baadaye urais.
Kwa wiki mbili sasa, viongozi wa vijana wamekuwa wakisutana, kulaumiana na kutuhumiana kujenga makambi ndani ya umoja huo. Wiki iliyopita walimrukia waziri mkuu mstaafu, Frederick Sumaye wakimtuhumu kuhujumu chama “kwa kuzungumza nje ya vikao.”
“Sikiliza bwana ee, vurumai hii ya vijana ni ya kutafuta kujenga kundi la kumsafisha Lowassa. Wapo wanaofanya kazi hiyo kwa kujua na wapo wanaofanya hivyo bila kujua,” ameeleza kiongozi mmoja mwandamizi wa CCM.
Hatua ya baadhi ya viongozi wa vijana, kurukia kila wanayeona ana uwezekano wa kupinga Lowassa na kundi lake, inaelezwa kutokana na waliokuwa wapinzani wao wakuu kubaki serikalini na wao (akina Lowassa) kuwa nje ya utawala.
Wanaotajwa kuwa serikalini, lakini wanadaiwa kuwa wapinzani wa Lowassa katika mgawanyiko wa wanaopinga ufisadi na wanaoutetea, ni pamoja na Samwel Sitta, ambaye hivi sasa ni waziri wa Afrika Mashariki.
Wengine ambao akina Lowassa hawakutegemea kuwemo serikalini, ni waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa, Benard Membe; naibu waziri wa ujenzi, Dk. Harisson Mwakyembe na mkuu wa wilaya ya Masasi, Nape Nnauye.
Lowassa hakuwa na simile pale alipohojiwa kwa njia ya simu kuhusu “mradi wa kujisafisha.”
Swali: Mheshimiwa, tumepata taarifa kuwa una mradi wa Sh. 8 bilioni kwa ajili ya “kujisafisha kisiasa.” Je, hii ni kweli?
Lowassa: Muulizeni huyo mpuuzi aliyewaambieni.
Swali: Gazeti linakuliza wewe kwa kuwa ndiyo mwenye mradi.
Lowassa: Mimi sijui. Sitaki kusikia mambo ya kijinga…”
MwanaHALISI liliripoti katika toleo lake la Machi 9 – 15 mwaka huu, chini ya kichwa cha habari kisemacho, “ Siri ya Edward Lowassa nje,” juhudi za mbunge Beatrice Shelukindo “kumsafisha” Lowassa.
Katika ujumbe wake wa maandishi kwa mbunge mwenzake, Pindi Chana, Shelukindo alisema ameambiwa na Nabii Joshua wa Nigeria kuwa “rais ajaye ni Edward Lowassa” na kwamba maisha yake ya nyuma yanayomhusisha na kashfa ya ufisadi, “si kitu.”
Joto la Shelukindo katika mawasiliano haya lilitokana na kile alichoeleza kuwa, “Mungu ni wa ajabu. Lowassa ameniombea kura pasipo maelezo. Ameandaa lunch na dinner (vyakula vya mchana na usiku) ambako amekuwa akiniombea kura. Mungu ana njia za ajabu za kufanya mambo.”
Shelukindo alikuwa akirejea fadhila za Lowassa kumwombea kura wakati wa kugombea nafasi ya kamishena wa bunge. Alishinda.
Naye Rostam alitafutwa kwa simu bila kupatikana. Hatimaye alipelekewa swali kwa njia ya sms.
Swali: Kuna taarifa kuwa umeahidi kumwezesha Mhe. Edward Lowassa kwa Sh. 8 bilioni katika kile kinachoitwa “mradi wake wa kujisafisha kisiasa.” Je, hii ni kweli? Simu yako haiitiki.
Tofauti na Lowassa aliyesema hataki kusikia “mambo ya kijinga,” Rostam alijibu kwa sms, “Sidhani Lowassa anahitaji mradi wa kumsafisha maana si mchafu,” kauli ambayo haikushangaza kwa kuwa ilitoka kwa swahiba mkuu wa wakati wa jua na mvua.
Rostam aliandika, “Isipokuwa nimetenga pesa kuwasaidia nyie MwanaHALISI mnunue mtambo wa kuchapisha gazeti bila bughdha!”
Hata hivyo, gazeti hili lina uhakika kuwa Rostam hana mtambo wa kuchapa magazeti yake ya Mtanzania, Rai, The African, Bingwa na Dimba. Anayachapia kampuni ya Mwananchi Communications Limited.
Majibu ya Rostam yameelezwa kuwa ya kumfariji swahiba wake kwa msingi mmoja tu; kwamba wameshiriki – kwa njia mbalimbali – katika kutafuta miradi ya kufua umeme, ambayo imeleta kashfa na kumfikisha Lowassa alipo sasa.
Mtoa taarifa amesema kundi la watu watano limekuwa likifanya vikao; lakini ni kikao cha Dar es Salaam cha mwishoni mwa mwaka jana, ambacho kiliweka mkakati wa Lowassa kujitokeza hadharani “kila inapobidi,” kushiriki mikutano na kutolea matamko hoja kadhaa zinazoibuka ili aonekane karibu na wananchi.
Maswali yaliyotumwa kwa wajumbe wengine wa kundi hili ambao simu zao ziliita bila kujibiwa au hazikupatikana, hayakujibiwa.
Wakati hayo yakifanyika, taarifa zinasema baadhi ya wajumbe wa NEC wamejipanga kupeleka hoja katika vikao vya juu kutaka watuhumiwa wote wa ufisadi waenguliwe kwenye nafasi zao za uongozi ndani ya chama.
“Tunakwenda kwenye NEC tukiwa na dhamira moja ya kumuondoa Rostam, Lowassa na Chenge katika vikao vya maamuzi vya chama chetu. Huo ndio mkakati wetu na lazima tuutekeleze ili kukinusuru chama,” ameeleza mmoja wa wajumbe wa NEC.
Katika minyukano hiyo, vijana ambao wasiokubali kuingia katika mradi wa kumsafisha Lowassa wameanza kusakamwa. Tayari mjumbe wa Baraza Kuu la uongozi la UV-CCM kupitia mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amesimamishwa uongozi na baraza la vijana la mkoa huo.

Pamoja na kutuhumiwa kuhujumu kampeni za mgombea ubunge wa jimbo la Arusha Mjini, Baltida Buriani, Gambo anatuhumiwa kumweleza mmoja wa watu walio karibu na Lowassa kuwa “hafai kabisa”, akitumia maneno ambayo, kwa kuzingatia maadili, gazeti hili haliwezi kuyachapisha.

Kauli ya Gambo ilipofikishwa kwa mtoto wa Lowassa, Frederick, mtoto huyo alimwandikia Gambo sms ifuatayo: “Gambo unayo haki ya kumchagu mtu yeyote unayemtaka na siyo kumutukana mzee wangu. Hiyo siyo siasa, lakini endelea.” Ilikuwa 4 Machi 2011, saa 2:14:39 usiku. Gazeti hili limeona mawasiliano hayo.
Uhusiano wa Gambo na wafuasi wa Lowassa ulizidi kuwa mbaya kutokana na kunukuliwa akielezea wajumbe wa baraza la vijana la taifa mjini Dodoma wiki mbili zilizopita kuwa, sababu kubwa iliyofanya CCM kufanya vibaya katika uchaguzi uliopita, “ni chama kukumbatia watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini.”
“Lowassa na Rostam ndio wanakipotezea mvuto CCM. Tusitafute mchawi. Watanzania wanakerwa sana na Richmond na Dowans na lazima CCM iwashughulikie wahusika wote ili kujenga taswira mpya kwa chama chetu,” alieleza.

msource wanahalisi​
 
Kwanza kabisa, naomba tuweke rekodi zetu sawasawa, Kamati ya Utekelezaji na Baraza la mkoa vilipangwa siku nyingi kabla ya baraza kuu la taifa, kwahiyo tusimtafutie mtu sympathy, havina mahusiano. Yeye labda alilitumia baraza kuu ili apate umaarufu na ili asifukuzwe, kwasababu alikuwa anafahamu kwamba lazima atajadiliwa na kufukuzwa tu.

Mimi nilichoshangaa sana kikubwa leo ni jinsi huyu kijana alivyotoka na kumtetea Kikwete na Batilda, labda kwa wale ambao hawamfahamu, huyu kijana ni mzaliwa na mkazi wa hapa Kariakoo Dsm na alienda Arusha miaka mitatu iliyopita na huko akakutana na rafiki yake kipenzi James Millya, ambaye alimtambulisha kwa Wamasai, Wa-Iraq, Wachaga, Wameru, Waarusha, Wasonjo na makabila yote kwenye wilaya zote za mkoa wa Arusha na kumuombea kura, kwasababu hamna mtu aliyekuwa anamjua, na akachaguliwa kuwa mjumbe wa baraza kuu taifa kuwakilisha mkoa. Alipokuwa Arusha aliishi kwa Mlezi wa James Millya pale Sakina na baadaye akachukuliwa na Mzee Elisa Mollel, ambaye amemlea kwa miaka hii mitatu kama mwanawe - Ninashangaa leo anavyothubutu kutukana ufisadi. Elisa Mollel ndiyo aliyofilisi kampuni yetu ya National Milling Corporation, na Nyerere akamshughulikia ipasavyo, ni bepari na beberu kwelikweli. Akiwa Arusha alimtukana Batilda matusi makubwa sana na kumhusisha Kikwete kwa maneno ambayo siwezi kutumia hapa - Huyu kijana ameshakuwa MCHAWI, siyo mnafiki tena.

Chuki yote hii ya huyo kijana kwa CCM ilianza pale Elisa Mollel aliposhindwa kura za maoni na Ole Medeye, na tena aliachwa kwa mbali sana - Medeye zaidi ya kura 10,000 akifuatiwa na Sabaya aliyekuwa na kura 8,000 na baadaye Elisa kura 2,000. Huyu kijana ndiyo alikuwa kampeni meneja. Baada ya matokeo hayo wakaunda genge la mtandao wa kuhujumu CCM Arusha Mjini kwa rafiki yao Felix na Arumeru, na hapa ndiyo nasema nashangaa.

Akiwa Arusha alikimbia vikao vyote alivyoitwa, siyo mwanaume huyo! KIla akinusa, hapashikiki. Kwani hatujui kwamba ndiyo mbeba mikoba wa Mbunge wa Arusha, UVCCM Mhe Catherine Magige?? Na hapo amefuatwa nini?? Tumbo linamsumbua. Ni aibu hata kumjadili huyu kijana hapa, hasathili. NI UCHAFU

Huyu kijana akiwa Arusha anajigamba na tena kwa matusi mazito kabisa jinsi ambavyo amewachakachua CCM kwenye kompyuta za manispaa na kuisaidia Chadema, mimi ningetegemea kuwa angetoka kwenye vyombo vya habari na kusema NINAHAMA CHAMA na ni kweli nimefanya hayo niliyoyafanya, na ndiyo maana hakuweza kuita waandishi wa habari kule Arusha, wasingemuelewa. Kwa Mhe Membe akamuita Dsm na kumuandalia mtaalamu wa fitina-Mbaraka Islam, kuandaa waandishi wa habari pale TAMAL Hotel.

Huy kijana siyo msaada kwa CCM na anatikiwa kufukuzwa Chama kabisa, na pia simuoni kama anaweza kukisaidia Chadema, tayari Chadema kina vijana wenye msimamo wa ukweli kama wakina Albert Msando pale Arusha na hawayumbishwi kwa matumbo yao kama huyu kijana. Ni aibu kuwa na vijana kama hawa kwenye jamii. Hafai kwa Chama chochote. Alipewa kazi manispaa ya Arusha kwa kifua cha CCM, vijana wengi wenye ouwezo Arusha mjini wakanyimwa kwasababu ya u-CHAdema wao, ndiyo maana leo hajui pa kukimbilia
 
Kwanza kabisa, naomba tuweke rekodi zetu sawasawa, Kamati ya Utekelezaji na Baraza la mkoa vilipangwa siku nyingi kabla ya baraza kuu la taifa, kwahiyo tusimtafutie mtu sympathy, havina mahusiano. Yeye labda alilitumia baraza kuu ili apate umaarufu na ili asifukuzwe, kwasababu alikuwa anafahamu kwamba lazima atajadiliwa na kufukuzwa tu.

Mimi nilichoshangaa sana kikubwa leo ni jinsi huyu kijana alivyotoka na kumtetea Kikwete na Batilda, labda kwa wale ambao hawamfahamu, huyu kijana ni mzaliwa na mkazi wa hapa Kariakoo Dsm na alienda Arusha miaka mitatu iliyopita na huko akakutana na rafiki yake kipenzi James Millya, ambaye alimtambulisha kwa Wamasai, Wa-Iraq, Wachaga, Wameru, Waarusha, Wasonjo na makabila yote kwenye wilaya zote za mkoa wa Arusha na kumuombea kura, kwasababu hamna mtu aliyekuwa anamjua, na akachaguliwa kuwa mjumbe wa baraza kuu taifa kuwakilisha mkoa. Alipokuwa Arusha aliishi kwa Mlezi wa James Millya pale Sakina na baadaye akachukuliwa na Mzee Elisa Mollel, ambaye amemlea kwa miaka hii mitatu kama mwanawe - Ninashangaa leo anavyothubutu kutukana ufisadi. Elisa Mollel ndiyo aliyofilisi kampuni yetu ya National Milling Corporation, na Nyerere akamshughulikia ipasavyo, ni bepari na beberu kwelikweli. Akiwa Arusha alimtukana Batilda matusi makubwa sana na kumhusisha Kikwete kwa maneno ambayo siwezi kutumia hapa - Huyu kijana ameshakuwa MCHAWI, siyo mnafiki tena.

Chuki yote hii ya huyo kijana kwa CCM ilianza pale Elisa Mollel aliposhindwa kura za maoni na Ole Medeye, na tena aliachwa kwa mbali sana - Medeye zaidi ya kura 10,000 akifuatiwa na Sabaya aliyekuwa na kura 8,000 na baadaye Elisa kura 2,000. Huyu kijana ndiyo alikuwa kampeni meneja. Baada ya matokeo hayo wakaunda genge la mtandao wa kuhujumu CCM Arusha Mjini kwa rafiki yao Felix na Arumeru, na hapa ndiyo nasema nashangaa.

Akiwa Arusha alikimbia vikao vyote alivyoitwa, siyo mwanaume huyo! KIla akinusa, hapashikiki. Kwani hatujui kwamba ndiyo mbeba mikoba wa Mbunge wa Arusha, UVCCM Mhe Catherine Magige?? Na hapo amefuatwa nini?? Tumbo linamsumbua. Ni aibu hata kumjadili huyu kijana hapa, hasathili. NI UCHAFU

Huyu kijana akiwa Arusha anajigamba na tena kwa matusi mazito kabisa jinsi ambavyo amewachakachua CCM kwenye kompyuta za manispaa na kuisaidia Chadema, mimi ningetegemea kuwa angetoka kwenye vyombo vya habari na kusema NINAHAMA CHAMA na ni kweli nimefanya hayo niliyoyafanya, na ndiyo maana hakuweza kuita waandishi wa habari kule Arusha, wasingemuelewa. Kwa Mhe Membe akamuita Dsm na kumuandalia mtaalamu wa fitina-Mbaraka Islam, kuandaa waandishi wa habari pale TAMAL Hotel.

Huy kijana siyo msaada kwa CCM na anatikiwa kufukuzwa Chama kabisa, na pia simuoni kama anaweza kukisaidia Chadema, tayari Chadema kina vijana wenye msimamo wa ukweli kama wakina Albert Msando pale Arusha na hawayumbishwi kwa matumbo yao kama huyu kijana. Ni aibu kuwa na vijana kama hawa kwenye jamii. Hafai kwa Chama chochote. Alipewa kazi manispaa ya Arusha kwa kifua cha CCM, vijana wengi wenye ouwezo Arusha mjini wakanyimwa kwasababu ya u-CHAdema wao, ndiyo maana leo hajui pa kukimbilia


ngo ma naon inogile. huyu ndio mpambanaji. kwa kweli kuna watu wakiona Mtu anaitukana CCM basi huyo mtukanaji yeye ni shujaaa, bila hata kuangalia uzito wa anayoyasema.

kwa kweli mtasubiri sana mkono uanguke
 
Hivi wakati haya yanatokea Benno Malisa alikuwa wapi? Au nae kishawekwa ktk kapu la mafisadi?

Nasema Benno kwa sababu hakuna asiyejua kuwa Shigela ni kibaraka wa mafisadi na yupo pale kulinda maslahi zao. Siku zenu zinahesabiwa, hakuna kupona ktk hili la kuiangamiza nchi. Hivi ni nani asiyejua kuwa suala la Richmond na Dowans, EPA na Kagoda, Deep Green na Meremeta ndio vilivyoipunguzia CCM kura ktk uchaguzi uliopita?

CCM sio ya watu wachache kama wengi wanavyofikiria, hiki ni chama cha wananchi. Wale wote wanaotuhumiwa na Ufisadi walioko ndani ya CCM waondoke kabla hawajaondolewa na nguvu ya Umma.

Mkuu hilo ni lakuuliza tena!

Simple: If you can't fight them, join them.

 
Hivi wakati haya yanatokea Benno Malisa alikuwa wapi? Au nae kishawekwa ktk kapu la mafisadi?

Nasema Benno kwa sababu hakuna asiyejua kuwa Shigela ni kibaraka wa mafisadi na yupo pale kulinda maslahi zao. Siku zenu zinahesabiwa, hakuna kupona ktk hili la kuiangamiza nchi. Hivi ni nani asiyejua kuwa suala la Richmond na Dowans, EPA na Kagoda, Deep Green na Meremeta ndio vilivyoipunguzia CCM kura ktk uchaguzi uliopita?

CCM sio ya watu wachache kama wengi wanavyofikiria, hiki ni chama cha wananchi. Wale wote wanaotuhumiwa na Ufisadi walioko ndani ya CCM waondoke kabla hawajaondolewa na nguvu ya Umma.
Jamani nyie mnaosema kuwa mtawatimua SISIEM hao mafisadi mtaweza?????????? Sasa wanajichimbia mizizi hadi watoto wao wana madaraka makubwa ndani ya UVWCCM na SISIEMU!!!!!!! Kwa hiyo si rahisi kama mnavyo fikiri, wana fedha na ukitilia maanani ni watu wachache wa kukataa mshiko, labda huyo kijana wangu Mrisho Gambo!!!!!!!
Hivyo hima bila kupoteza muda hamia kwenye chama makini cha kukomboa Watanzania CDM. Prof Safari kaonyesha njia!!!!! Chama chenye nia ya kuondoa uozo wote uligubika taifa hili la TZ!!!!
Hawa mafisadi hawatapata muda wakusumbua watu maana wote wataingia lupango wajibu tuhuma za kutuibia fedha zetu. Sio kuwabembeleza eti warudishe mbilion yetu!!!! Toka lini ukaona mwizi eti arudishe alicho iba ili asishitakiwe???????????Taifa la ajabu hili, eti wezi wanaogopwa nani kasema????????
 
Akina Aloyce Kimaro, sherukindo, selelii wako wapi. Nimekuwa napingana sana na mtazamo wa wapambanaji kujitoa ndani ya CCM. Kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hii, Waziri Mkuu Edward Lowassa na mawaziri kadhaa walilazimika kujiuzuru kwa sababu ya kazi kubwa iliyofanyika ndani ya CCM ndio maana naamini kuwa kupambana ukiwa ndani kunaweza kuleta mageuzi.


Hivi kwani mtu hawezi kuwa mpambanaji mpaka atoke ndani ya ccm? Mi sikubaliani na wote wanaotaka wanaopambana na ufisadi watoke ccm kwanza.

Wako wapi kina Mpendazoe, Mrema nk? Wote wamechemsha baada ya kuhama CCM.

Mpambano ni lazima uwe ndani ya chama ili kuwang'oa wezi wa nchi hii. Nashauri wapiganaji wote wasihame CCM ila wawe makini na michezo michafu inayofanyika ndani ya CCM.

"msiwaachie nguruwe wale shambani peke yao"
 
Back
Top Bottom