96.
“Baaadaye wacha niendelee na majukumu, tuna msiba mzito umetukbili na mbaya zaidi unamuhusisha raisi wa Rwanda na mke wake. Tutaonana labda baadaye nyumbani ama kesho maana shughuli ni ndefu!” Okoye akamuaga Jackky kisha akazirudishia pingu zake kiunoni nakuondoka na wenzake huku wakiwa wamebeba machela iliopkiza maiti.
Muda wote huo Alice alikuwa akitetemeka. Hakuwa akijitambua n mbaya zaidi hakuamini kama amenusurika mikononi mwa Okoye kwa jinsi alivyokuja na akivyoondoka.
“Asante sana Jacky, wewe ni rafiki wa kweli naaamini”
“Usijali sana Alice!, embu nimbie ukweli Alice unaonekana hauko sawa kabisa, kwani huyo Aloyce sijui ulioropoka unamjua?”
“Ni hadithi ndefu kidogo Jacky lakini nitakusimulia tu hata baadaye, kwa sasa akili yangu haijakaa sawa”
Alice akiwa bado yupo na Jacky katika maongezi yao mara tena akatokea mwanamke mwingine.
“Alice? Alice wajua wafanya mie niwekwe kwa hatia?”
Alikuwa ni Achieng, yule rafiki wa muda wa Alice pindi alipoingia mule chumbani kwake nakuingia chooni kisha akapanda juu ya dari na kumuacha akiwa sebuleni.
.
“Achieng, my friend. Kwanza unatakiwa uanze kwa salamu mbona upo hivyo?”
“Ohh soryy maze, wajua nilikuwa katka panic ya juu, but siyo fresh vile wanifanyaga Alice?”
“Haya, Jacky huyu ni rafiki yangu wa humu humu hotelini nimemjua na ametokea Kenya anaitwa Achieng. Achieng?”
“Yes, Alice!”
“Huyu ni my best friend wa siku nyingi na ametokea Tanzania ninapoishi. Na alikuwa miss Tanzania kipindi cha nyuma.”
“Nashukuru kwa kumjua”
“Asante, Achieng. Lakini mimi kwa sasa sipo tena Tanzania naishi huku huku Nigeria”
Kitendo cha kutambulishana pale wakijuana kikamfanya hata Achieng asahau mada iliyomleta pale ya kumlaumu Alice kwa kitendo cha kumuacha chumbani ppeke yake nakumletea matatizo. Achieng akajikuta amesahau kabisa. Story zikawanogea kwa maneno mbali mbali haswa ya urembo kwani Achieng alipenda sana ajue masuala ya urembo kiundani. Muda wote huo akili ya Alice haikuwa imekaa sawa.
“Jamani Achieng na Jacky? Samahanini mara moja nakuja naelekea chumbani kwangu mara moja”
“Akili ya Alice moja kwa moja ikahama na sasa ikahamia ni jinsi gani atajinasua pale hotelini kwa kubadilisha zile nguo kwani zilikuwa zimetapakaa damu japokuwa zilikuwa zimemganda. Mawazo ya Alice moja kwa moja yakawepo katika chumba alichokuwa amepangisha Aloyce mwanzoni wakati wa harusi kwani aliacha nguo wakati anabadilisha kuvaa gauni aliokuwa amenunuliwa na Aloyce. Akaingia ndani ya lifti mpaka ghorofa ya pili, kile chumba kilikuwa katika akili yake lakini alipofika mbele ya mlango wa kile chumba kikawa kimefungwa.
“Shiit, my God!” (Mungu wangu!)
Akajikuta nguvu za mwili kumlegea na akili kumchoka ghafla baada ya kukuta mlango umefungwa. Halamshauri ya kichwa chake ikapambanua kwa haraka zaidi ikamuamuru ashuke chini mpaka alipowaacha Jacky na Achieng. Akafanya hivyo.
“Achieng? Ujue nimesahau mkoba wako chumbani kwako si unakumbuka niliingia nao kwako?”