Mramba amwaga fweza Rombo

Mramba amwaga fweza Rombo

Geza Ulole

Platinum Member
Joined
Oct 31, 2009
Posts
75,552
Reaction score
106,957
Inasemekana yule Mbunge machachari wa Rombo mwenye kesi mahakamini ya Ufisadi kipindi cha uongozi wake katika wizara nyeti ya Fedha amekuwa akigawa Tshs 5000 kwa kila mwanakijiji huko kijijini kwake ilihali Takururu wakishuhudia vituko hivi! wanakijiji wanasema kigogo huyu huwaita mmoja baada ya mwingine na hukaa katika baraza ya juu (kwa kiingereza balcony) huko ghorofani kwake hapo kijijini kwake Shimbi na kudondosha Tsh 5000 taslim!
 
Mramba ana mabaya yake lkn tumtendee haki,uvumi wa uongo tuachanae nao.Siamini kama kuna kiongozi yoyote anaweza kugawa pesa kwa njia kama unayosema wewe.
 
Kwa jinsi ufisadi/ubadhilifu ulivyozoeleka kwa watanzania pale ambapo mhusika anapokamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria, tunawaona kana kwamba ndio ma-victim/wamefanyiziwa. Inashangaza sana kuona watanzania bado tuna-sympasize na wezi hawa!
 
Mramba ana mabaya yake lkn tumtendee haki,uvumi wa uongo tuachanae nao.Siamini kama kuna kiongozi yoyote anaweza kugawa pesa kwa njia kama unayosema wewe.
waliopewa hela ndo wanadai hivyo sasa kama mnabisha ngojeni watajitokeza watu humu ndani ya forum kusema ukweli suala ni kutoa hongo hapa whether ghorofani au chini ya uvungu! ninachoomba Mungu TAKURURU wafanye kazi yao na wasiishie kwa Mramba tu hata wabunge wengine wa CCM na upinzani
 
Si kwa sababu ameua ATCL na kuanzisha Precision? Mwache tu mungu yupo!
 
Uzushi wa namna hiyo haukubaliki hata kidogo, Mramba sio mpumbavu kiasi hicho hadi awe anawadondoshea wanakijiji pesa, hata kama wakijitokeza tutawaamini vipi? Kweli ni mtuhumiwa wa ufisadi lakini hiyo imezidi.
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni!
Mramba ana kesi sasa hivi... halafu ajiongezee nyingine ya kugawa rushwa jimboni kwani hajitaki?
Kama kuna wanakijiji wamekudokeza basi hizo ni porojo za kijiweni tu.Haiingii akilini kwamba huyu bwana anaweza kufanya hivi!
 
Si kwa sababu ameua ATCL na kuanzisha Precision? Mwache tu mungu yupo!

Mkuu japo ni haki yako kutoa maoni lakini hili umekosea na uko mbali saana na ukweli

hakuna uhusiano wowote kati ya Kudorora kwa ATCL na kukuwa kwa PW( precision AIR) proprietor wa PW alitangaza kwenye magazeti ya TZ pamoja na The east african mtu au kampuni inayotaka share, walijitokeza KQ wakaninua share ,na kuchukua management, maendeleo yote unayoyaona PW yameletwa na Wakenya na sio Mramba wala ATCL.
 
Inasemekana yule Mbunge machachari wa Rombo mwenye kesi mahakamini ya Ufisadi kipindi cha uongozi wake katika wizara nyeti ya Fedha amekuwa akigawa Tshs 5000 kwa kila mwanakijiji huko kijijini kwake ilihali Takururu wakishuhudia vituko hivi! wanakijiji wanasema kigogo huyu huwaita mmoja baada ya mwingine na hukaa katika baraza ya juu (kwa kiingereza balcony) huko ghorofani kwake hapo kijijini kwake Mengwe na kudondosha Tsh 5000 taslim!

Can you prove it a bit!
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni!
Mramba ana kesi sasa hivi... halafu ajiongezee nyingine ya kugawa rushwa jimboni kwani hajitaki?
Kama kuna wanakijiji wamekudokeza basi hizo ni porojo za kijiweni tu.Haiingii akilini kwamba huyu bwana anaweza kufanya hivi!


Kama mramba mwenyewe bila kulazimishwa alisema watanzania bora wale majani lakini ndege ya rai lazima inunuliwe, mnamtetea kwa lipi? au mli kula naye pesa ya ATC?
 
Mkuu japo ni haki yako kutoa maoni lakini hili umekosea na uko mbali saana na ukweli

hakuna uhusiano wowote kati ya Kudorora kwa ATCL na kukuwa kwa PW( precision AIR) proprietor wa PW alitangaza kwenye magazeti ya TZ pamoja na The east african mtu au kampuni inayotaka share, walijitokeza KQ wakaninua share ,na kuchukua management, maendeleo yote unayoyaona PW yameletwa na Wakenya na sio Mramba wala ATCL.

Kweli nilikosea, siyo ATCL ni enzi za ATC wakati wa ubinafsishaji hapo ndo Basil Pesambili Mramba alikula mlungula na akaiua ATC na kisha ikauzwa.

 
Kama mramba mwenyewe bila kulazimishwa alisema watanzania bora wale majani lakini ndege ya rai lazima inunuliwe, mnamtetea kwa lipi? au mli kula naye pesa ya ATC?

Kwa vile alisema ndio ushahidi kuwa kila lisemwalo juu yake ni kweli? Hebu usichekeshe watu..toa ushahidi ndicho tunachoongelea hapa! Vingenevyo ni umbeya na majungu... kesho wakisema wewe ulifanya A, B ,C, KWA VILE TUNAKUCHUKIA BASI TUKUBALI TU KWA VILE kuna bias against you?

Hatumtetei bali tunatafuta kuwa objective katika mjadala. Hatusengenyi hapa...tunajadili ishu....
 
Hivi mtuhumiwa wa ufisadi tena ana kesi mahakamani, anaruhusiwa kugombea ubunge? kama hivyo ndivyo nchi hii imeoza
 
Kwa vile alisema ndio ushahidi kuwa kila lisemwalo juu yake ni kweli? Hebu usichekeshe watu..toa ushahidi ndicho tunachoongelea hapa! Vingenevyo ni umbeya na majungu... kesho wakisema wewe ulifanya A, B ,C, KWA VILE TUNAKUCHUKIA BASI TUKUBALI TU KWA VILE kuna bias against you?

Hatumtetei bali tunatafuta kuwa objective katika mjadala. Hatusengenyi hapa...tunajadili ishu....
TAKURURU wanamuwinda na watamdaka soon si mnataka ushahidi msije mkasema anaonewa tu! maana hapa naona kama kuna kautetezi fulani nenda jimboni kwake utaambiwa hii story na inakuwaje ni yeye tu ahusishwe na kutoa fweza while kuna wagombea wengi tu hatuskii wakitoa buku tano tano?
 
Si kwa sababu ameua ATCL na kuanzisha Precision? Mwache tu mungu yupo!

Mkuu Magezi nakubaliana na wewe kuwa Mramba alipokuwa waziri wa Fedha alihujumu sana ATCL kwa kukaidi maagizo ya muungwana kuhusu kuipa ruzuku ATCL na sio hivyo tu bali hata pale fedha ilipotolewa ilikuwa inacheleweshwa hivyo kuathiri utendaji wa shirika!! Alipoondolewa hapo wizara ya fedha ,yakabakia masalia yake yaliyoendeleza libeneke la kulihujumu shirika na sasa ndio hao hao wanashabikia kua ATCL ivunjwe ili Mramba na Precision yao wavune kwa kuwa na monopoly!! Mungu mkubwa atamuhukumu na kumpa adhabu yake hapa hapa duniani na wala sio adhabu ya kula manyasi bali mbaya zaiadi!!
 
Mkuu Magezi nakubaliana na wewe kuwa Mramba alipokuwa waziri wa Fedha alihujumu sana ATCL kwa kukaidi maagizo ya muungwana kuhusu kuipa ruzuku ATCL na sio hivyo tu bali hata pale fedha ilipotolewa ilikuwa inacheleweshwa hivyo kuathiri utendaji wa shirika!! Alipoondolewa hapo wizara ya fedha ,yakabakia masalia yake yaliyoendeleza libeneke la kulihujumu shirika na sasa ndio hao hao wanashabikia kua ATCL ivunjwe ili Mramba na Precision yao wavune kwa kuwa na monopoly!! Mungu mkubwa atamuhukumu na kumpa adhabu yake hapa hapa duniani na wala sio adhabu ya kula manyasi bali mbaya zaiadi!!

....kama unaamini hayo basi wewe IQ yako ni infinitesmal! hivi wakati ule jamaa flani waliponunua midege miwili mibovu ulishazaliwa weye? Mishirika kibao ilifilisika kwa UTENDAJI MBOVU na UKWAPUAJI ulofanywa na mijamaa ambao referees wao ni ................! Refer to HUJUMA kama hizi kujenga mada...na sio submission ya pumba kwenye space hii inayoweza kutumiwa vyema zaidi?
 
Mkuu Magezi nakubaliana na wewe kuwa Mramba alipokuwa waziri wa Fedha alihujumu sana ATCL kwa kukaidi maagizo ya muungwana kuhusu kuipa ruzuku ATCL na sio hivyo tu bali hata pale fedha ilipotolewa ilikuwa inacheleweshwa hivyo kuathiri utendaji wa shirika!! Alipoondolewa hapo wizara ya fedha ,yakabakia masalia yake yaliyoendeleza libeneke la kulihujumu shirika na sasa ndio hao hao wanashabikia kua ATCL ivunjwe ili Mramba na Precision yao wavune kwa kuwa na monopoly!! Mungu mkubwa atamuhukumu na kumpa adhabu yake hapa hapa duniani na wala sio adhabu ya kula manyasi bali mbaya zaiadi!!
Aliyeuwa ATC ni Chenge maana yeye ndiye aliyesaini mkataba ulikula upande wa Tanzania akiwa AG wakati huo! na anayeiua ATCl sasa ni Nyang'anyi na Mataka. Lets be objective hapa na tusiende nje ya topic kuna hili la kumwaga fweza
 
Aliyeuwa ATC ni Chenge maana yeye ndiye aliyesaini mkataba ulikula upande wa Tanzania akiwa AG wakati huo! na anayeiua ATCl sasa ni Nyang'anyi na Mataka. Lets be objective hapa na tusiende nje ya topic kuna hili la kumwaga fweza

....ilishakufa kabla ya hapo ikabaki ICU baada resuscitation. Chenge na wenzake waliendelea kubadili mitungi wa OXYGEN tu!
 
Back
Top Bottom