Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,902
- 944
MRADI WA MAJI KUTOKA ZIWA VICTORIA KWENDA MULEBA WANUKIA
Serikali kupitia Wizara ya Maji kuanza utekelezaji mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kupeleka Muleba kwa mwaka wa fedha ujao.
Hayo yametanabaishwa na Naibu Waziri Wizara ya Maji Mhe. Maryprisca Winfred Mahundi wakati akijibu swali la Mbunge wa Muleba Kusini Mhe. Oscar Ishengoma Kikoyo alilouliza Leo Jun 9, 2023 Bungeni jijini Dodoma kwa kutaka kujua mpango wa Serikali katika kutekeleza Mradi huo.
“Ni lini Wizara ya maji itaanza kutekeleza Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwaajili ya Wilaya ya Muleba? - Mhe. Dkt. Oscar Kikoyo, Mbunge wa Muleba kusini.
“Tulishakubaliana mwaka ujao wa fedha tunakwenda kukamilisha usanifu na kuona uwezekano wa kufanya Mradi huu” Mhe. Maryprisca Mahundi