Mradi wa Bagamoyo ulitakiwa uanze kabla ya Bwawa la Nyerere, Rais Samia umetuheshimisha

Kwan mkuu ww kuna mkataba uliokwishawah kuuona??Mbna unapose question kwenye mkataba huu Tu wa bagamoyo!!
 
Kama umesoma na kuelewa nilichoeleza katika pongezi hizi kwa dikteta Magufuli na hiki nilichoandika leo utaona wazi leo sipingi mradi wa umeme bali nimependekeza kuwa bandari ingeanza kisha umeme na SGR vifuate
@yeriko.hv Kati ya umeme na badari kipi kinafaida kubwa?? Eleza namna mladi wa bagamoyo utakovyo mnufaisha mtu alieoko uvinza au nyakahoza??
Think big yeriko au nawe umooo??
 
mbaya kabisa akawadanganya na chadema kwenye siasa mpaka sasa wamekwenda na maji.

ukituliza kichwa chako sawa sawa unaiona bandari ya bagamoyo kama geti la uchumi labda,vipi bandari ya dsm unaiweka wapi??
 
Pale Twiga ni upuuzi mtupu. Hakuna mabadiliko chanya. Ungejua kilichomo kwenye mkataba usingesifu chochote. Hakuna anayeweza kuutoa hadharani ule mkataba, kutokana na aibu. Magufuli was a good president for the fools.
kwamba una guts zote za kuita watu fools!!!

mkuu kujiona una akili zaidi nao ni ugonjwa.
 
Kama kulikuwa hakuna mkataba contraction ilikuwa ya nn?? Unanajua mkataba huo ulisainiwa lini na katika awam ipi??

Mkuu think big.. ndo maana mashart yake magumu
 
aaah weee usikimbie kisogo chako.

chuki kwa magufuli ni kiini cha upinzani wako kwake,mengine ni miamvuli tu ya kujifichia.
hauwezi kusema mtu alikuwa mwongo kupita kiasi,alidanganya wapi,kuhusu nini??
mtu akikwambia gari lako ni bovu,kufika safari uliyokuwa uende hakumfanyi yeye kuwa mwongo.

nakuulize swali rahisi tu,kwanini ujenzi wa bandari ya nne kubwa zaidi wakati tatu zilizopo hazijapewa uwezo stahiki!!!
 
Juzi mama aliongea na rais wa China kwa simu ya kiganjani. Leo mama kasema bandari inajengwa............??????!!!!!!!!##
 
Hii nchi hatuwezi kutoka kwenye mkwamo kwa kuogopa kuchukua maamuzi makubwa yenye maslahi mapana kwa Taifa eti kwa sababu uwekezaji unasimamiwa na sekta binafsi.

Hata Uganda wangekomaa na ujinga wa kusema eti wapate 50/50 na Total hakuna kitu wangefanya hadi leo.

Uchumi sio Kodi tuu bali value chain ya mradi husika,imagine tumepoteza mradi wa LPG Lindi dola za kimarekani bil.30,,hizi pesa zingeingia kwenye uchumi wetu leo tusingekuwa tunaongelea madarasani na vyoo vya watoto.

Uzuri wa miradi hii mikubwa inajenga taswira nzuri kwa wawekezaji wengine kwamba kumbe nchi ina stable economic policy na hivyo ingefungua fursa kwa wengine.

Nchi hii iko vizuri kiusalama na kwa hiyo ilotakiwa kuwa kitovu cha uwekezaji kwa EAC yote maana hatuna changamoto za kiusalama kama kwingine.

Mama Songs na miradi yote iliyokwama kwa miaka na miaka ,tukipata robo tuu kwenye kila mradi inatosha sana maana value chain yake itaifaidisha nchi kuliko kuangalia kodi za directly
 
Kama akili yake ndo ilipoishia sasa ulitaka asemaje?

Swala ni kuvunja mkataba au kuuboresha?
 
What a load of rubbish. Mbunge Godbless tunammiss sana kwa busara zake, hapa angetusaidia

Eti:
............Serikali ya awamu ya nne ilianzisha mradi wa kimkakati kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara duniani, mradi huu ilikuwa ni kujenga bandari ya Bagamoyo kwa ubia kati ya China na Omani wenye thamani ya dola bilioni 10, Serikali ya Tanzania katika mradi huu ilikuwa haiweki pesa yoyote ISIPOKUWA ARHI na raslimali zingine, huku Uchina na Omani wakiweka mtaji na UTAALAM........

Hapa unamaanisha kuwa ardhi haina thamani, kwa sababu hizo $10billion zingerudi kwenye mapato ya kodi unazoziita ZA UBIA. If it is so simple kwa nini hawakubaki huko huko kwao? Ni kwa sababu hawana ardhi ndiyo maana wakaja hapa. Kwa nini hawakuenda Argentina au Mongolia au Finland? Kwa sababu hawana Bandari ya Bagamoyo. Ardhi is a rare commodity, to them, si ya kubeza.

Umesema wangeleta utaalamu? Mbunge Lema hizo uwa anaziira PowerPoint presentations.

Anawejeza $10 billion, payback period within 3 years kama bandari itachakarika kama wanavyodai, miaka 99 ya nini? TPA sasa hivi wanakusanya kiasi hicho kila mwaka.

Huko nyuma mikataba ya PowerPoint presentations inetuumiza sana. Makaburu walipoweka "investment" kufufua TBL walipata majumba ya thamani uzu guni, wakayauza kwa mabalizi na kuwejeza Treasury bills zeny yield ya 60% wakati huo, hela yao yote inaudible within 18 months,not 99 years. TTCL walitaka kufanya hivyo hivyo, na Barrick Gold, tukagutu Magufuli akawa firm.

Tunaisubiri kwa hamu hii bandari tuoneshwe PowerPoint presentations.
 
Nna uhakika location ya bagamoyo wameifanya kutokana na strategic kulingana na upembuzi waliofanya wataalamu wangeweza kwenda kokote.

Habari ya accacia hapo nakuunga mkono ila ni tofauti kwa kuwa mradi wa madini huwa unafika muda madini yanaisha tofauti na bandari na strategic location kijiografia haina mwisho. Huwezi kufananisha swala la madini na bandari kuna walafi wachache wamefikiri kwa kutumia matumbo yao hawakuwaza kizazi kijacho cha taifa hili kwenye madini.
 
Mkuu sa iv watu wote waliokuwa adui wa serikal ni marafik wa serikal subr tu uone huko mbele
Inaonekana hao watu ndiyo wazalendo wa kweli. Hawaangalii chama bali wanaangalia maslahi ya nchi.

Mama Samia, nina imani kubwa ana uzalendo wa hali ya juu. Anaangalia zaidi Taifa kuliko matakwa ya wajinga waliopo ndani ya chama chake.

Mimi kwangu kilicho muhimu siyo CCM wala CHADEMA au CUF au ACT, kilicho muhimu ni Taifa letu.

Kama kutakuwa na kiongozi mzuri ndani ya CCM hii mbaya, kiongozi asiye mnafika na mwongo kama alivyokuwa marehemu, nitamwunga mkono kiongozi huyo.
 
Mama kawekwa mfukoni na uncle aliyesema msibani Hana ugomvi na marehemu. TATIZO. Bora wamchukue mfumgwa wao tu.
 
Sawa
 
Akiandika yericko mwisho kabisa anatangaza kitabu na bei zake utasikia ujajsusi wa kidola
 
Uliwahi kudai Mkataba wa ununuzi wa Ndege na ujenzi wa kiwanja Cha Ndege chato?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…