Mpenzi Msafiri

Mpenzi Msafiri

sehemu ya Pili:
Sasa kazi iliyopo mbele yetu ni msako wa Guest House, ndio cha kwanza cha muhimu, huku tukiwa na hofu ya wingi wa wasafiri eneo lile usijesababisha tukakosa vyumba. Huku kigiza giza kikiwa kinachanganya, na kibaridi chake, mchakato wa kutafuta Guest ukaanza! Mimi kushoto, Milgo kulia!

Kama kawaida, John, rafiki yangu wa Kiganda ambae mpaka sasa, ameshanikubali kwa sifa zote kuwa, sasa urafiki wetu umevuka mipaka, ni ndugu sisi, na mimi huku nikijua misingi ya safari ukiwemo ule wa “MSAFIRI KAFFIRI”, bado niliendelea kuwa na imani juu ya ndugu yangu huyu wa hiyari.

Ni jioni. Mji wa Tunduma upo busy, watu ni wengi, kuna kagiza fulani hivi, na pia kuna kaubaridi chenye upepo. Watu ni wengi, wametoka Dar es salaam na wengine Mbeya Mjini, wapo waliotaka kuvuka boda kama sisi, wapo pia walotaka kulala katika hotel chache za mji ule na kisha kukicha waendelee na haraka ti zao. Alimradi hapakuwa na utulivu eneo lile. Milgo aliitumia fursa hii, kunidhihirishia namna ambavyo anaifurahia safari hii na hasa kwa kigezo kwamba, imempa mpenzi ambae kwake yeye ni kama kuwa na bahati ya MTENDE (Kumbuka nilishakueleza tangu awali kwa namna gani, mtende una bahati) Hakuruhusu kuwepo kwa umbali wowote ule baina yetu, ilikuwa ni kama ULIPO NIPO! Milgo hakutaka mtu wa tatu aingilie kile kinaendelea baina yetu, mimi na yeye.

John.
Anaonekana kwa nyuma yetu, kwa aliebahatika kumuona John katika mandhari ile ni sawa na kusema, ilikuwa bendera fuata upepo, muda wote alifanya kile ambacho mimi na Milgo tulishauriana na kufikia maamuzi. John hakupendezwa na kupotezwa kwa hadhi yake na mie afiki yake. Nililijua hilo. Nikajua kuwa kwa mara nyingine tena, namtia majaribuni John, mtu ambae kwangu ni ndugu, sio rafiki tena.

Kama ilivokuwa pale awali, John hafurahiii hali hii, hali ya mimi kumpa kipaumbele mtoto wa kike mbele yake. Kwake yeye John, hataki kukubali kuwa, kulikuwa na umuhimu wa mimi au hata sisi sote kuwa karibu na mabinti wale.

Hatukuzunguka sana. Hatimaye tuliingia ndani ya nyumba moja ya kawaida tu, wenyewe wakiwa wameipa jina kuwa ni hotel, ni mfano wa guest house za uswahilini kama vile Tandale, Buguruni au Mbagala kwa Dar es salam, au sawa na Unga Limited na Matejoo kwa kule Arusha, au Pasua – Moshi!

Chumba kikapatikana.
Milgo akashauri chumba kikaguliwe kabla ya kulipiwa. Tukakikagua. Milgo akakiri kinafaa. Ni raha ilioje kuambatana na mtoto wa kike hotel, kisha awe wa kwanza kuridhika na mandhari ya chumba kama sio hotel!
Chumba kikalipiwa papo hapo.

MAAJABU.
Nikatua begi langu. Kugeuka nyuma, zamani Milgo alishajitupia juu ya kitanda. Ni kweli huyu bint ni mzuri, lakini macho yangu hayaamini kuwa muda wote nliokuwa nae, nilichoona ilikuwa ni robo tu uzuri wake, sasa nakiri ninachokiona ndio uzuri halisi! Kitanda kimefanya uzuri wa bint huyu wa Kisomali uonekane kwa mapana yake.

Milgo akafurahi kuona angalau hatua ya kwanza ya safari yetu, imefika salama, kwake yeye na Fatma, na nafsi zao, ule ulikuwa ni ushindi, yaani kufika border ya Tanzania na Zambia, salama salmini. Vichwani mwao bado kulikuwa na kumbu kumbu za masaibu yaliowakuta wakati wanajaribu kuvuka Namanga, kutokea Kenya kuingia Tanzania, anasema Milgo, walioyaona border ya Kenya na Tanzania, wakifanyiwa wakimbizi wa kisomali, ni kinyume na ubinaadamu. Usisahau. Milgo. Fatma. Ni wakimbizi wa kisomali.

Nikamskia akinipa pole za uchovu wa safari ya kutwa nzima, Ubungo, Dsm mpaka Tunduma, kauli ile niliitafsiri kama kukaribishwa kitandani, kupumzika, yaani kuondolewa uchovu wa safari (akili haikukumbuka kuwa hata na yeye ana uchovu wa safari)

Sikujiuliza mara mbili. (udadisi ni kitu kizuri, lakini kuna maeneo usilete udadisi, utaonekana una matatizo kichwani). Nlichofanya ni kama kujitupa kitandani. Ghafla milgo wangu akasimama. Nikashtuka. Akaniita. Nikaitika. Nikavutwa kama kusaidiwa kusimama, nikasimama, nikashikwa mabega kwa mikono miwili, mimi nikashika kiuno chake kwa mikono yangu! Nikakumbatiwa. Vifua vikanasiana. Nikawa naskia mapigo ya moyo, yanadunda kwa kasi, sikuweza kujua kama yale mapigo ya moyo ni ya kwangu au ya mpenzi wangu, kitu mfano wa mawimbi ya joto yakawa yanazunguka katika mwili wangu, akili yangu ikapata kazi ya ziada kutafsiri hatua ambayo mabadiliko ya mwili yanapitia muda huu.
Ni kama sijitambui. Kwa mbali nikahisi maumivu maeneo ya zipu ya suruali yangu aina ya jinsi! Cha ajabu maumivu yale nayajua yalisababishwa na nini, na nakijua kiungo cha mwili wangu kilichokutwa na dhahama ile, lakini sikujali! Daaaaah!

“Eeeeh my boy,lets get out….!” Please, tutoke nje (katika lafudhi ya mtu asiejuwa vizuri Kiswahili) Ghafla milgo akaamrisha kuwa tutoke nje. Nikawa kama sikuelewa vile. Akarudia tena. Nikaona namna uso wa mtoto wa kike ulivokuwa ukimaanisha kuwa yuko serious!

Nikaacha kila kitu changu ndani, nikafunga chumba na kutoka nje. Mseto nliokuwa nao kichwani ni kama vile mtu aliepatwa na mshangao uliochanganyika na taharuki pamoja na sintofahamu! Unyonge ulinijaa! Nje tukawakuta Fatma na John wanaongea, sikutaka kujua wanaongea nini, ila tu nliskia Milgo akiwaomba turudi wote ndani. Huko ndani Milgo alikuwa ndio msemaji mkuu, aliskika akitoa maelezo kuwa Mimi na John tutalala pale, ndani ya chumba kile, na kwamba anatutakia usiku mwema, na kwamba asubuhi watawahi kuja kugonga mlango kutuamsha, yaani tusitoke mpaka wao watufuate asubuhi!

Kwangu yaliingilia kushoto yakatokea kulia. Sina nlichomuelewa Milgo. Hasira. Kwa mara ya kwanza Milgo ananikwaza. Anauchooma moyo wangu kwa maumivu ambayo yananipa wakati mgumu sana kuyapoza.
Wakati mimi naugulia maumivu ya kulazwa na John, sio tu chumba kimoja, bali kitanda kimoja, John alikuwa busy kupanga na kupangua vitu vyake alivokuwa navyo ndani ya begi na hasa hasa nguo. Ilionekana wazi kuwa John alishachoshwa na drama kati yangu na Milgo.

Nlipokuja kushtuka ni pale John aliponisihi tufanye mpango wa kutafuta chakula, nikakubali lakini nilitoa rai kuwa, tuanze na zoezi la kuoga kwanza kisha lifuate zoezi la chakula. John alinielewa. Ndani ya dakika fupi John akawa na bukta na singlend. Nikamuomba john akaanze yeye kuoga. John akakubali. Wakati mimi najiandaa kubadili nguo, mpaka namaliza nikiwa na pensi chini tshirt juu, bado John hajaenda kuoga, yuko busy lakini sikuelewa anafanya nini!

Nikamuuliza John: “mbona huendi kuoga, muda unaenda na baridi linazidi kuwa kali?” badala ya kwenda bafuni, John akanambia nikaanze mimi kuoga.
Mabishano yakaanza rasmi, nani akaanze kuoga. Tayari akili zangu za awali zimeshanirudia kuwa MSAFIRI KAFFIRI, na kwamba katika safari hupaswi kumuamini kiumbe wa aina yoyote ile. Na kwamba safarini, muda wote ni muda wa tahadhari. Hapa sasa nipo tayari kusimamia misingi hii. Simuamini John. Ajabu ya binadamu, nilikuwa radhi kumuamini Milgo, hata kwa gharama ya kulala nae usiku kucha. Lakini ghafla nashindwa kumuamini Mwanaume mwenzangu, John, ambae nafsi ilishakiri kuwa ni ndugu yangu, ndugu wa hiyari.

Ni kama ugomvi. Sitaki kwenda kuoga. John nae hataki kutangulia kuoga yeye kabla yangu. Ni vita ya maneno, kila mmoja anatetea msimamo wa kuwa wa mwisho kwenda kuoga. Hisia kwamba huyu John tumekutana ndani basi Ubungo Dsm, tena kwa bahati mbaya, zinazidi kunipa ujasiri wa kusimamia hoja yangu kuwa yeye anapaswa kuwa wa kwanza kuoga. Ni utata kati yangu na John. Ugomvi. Ugomvi juu ya nani wa kwanza kwenda kuoga. Imani zimetutoka. Hatuaminiani.

Hatimaye nikakubali yaishe. Nikaenda kuoga. John akanisubiri. Nilienda kuoga kwa sharti kwamba funguo ya mlango wa chumba naenda nayo bafuni. Nikarudi na John nae akaenda kuoga, bila hata ya kudai funguo ya chumba. (nilihisi ujinga). Baada ya muda mfupi tukawa tayari kwa kwenda kutafuta chakula.

Nje huko tukawa tunatafuta sehemu nzuri ya kupata chakula na angalau kuvuta muda ili angalau mpaka saa 4 usiku turudi hotelini kwetu kulala. Tukabahatisha mgahawa mmoja. Tukaingia na kuomba huduma ya chakula. Tukaanza kupata chakula huku tunazungumzia safari yetu kwa maana ya tathimini mpaka hapa tulipofikia na yaliojiri ndani ya safari.

Mara ghafla Milgo huyu hapa! Milgo mbele, Fatma nyuma.

Waione: chiko18 NYANYADO Aristidi selestin Milugwi Heaven Sent icca peterchoka Gobe loveissweet miss nuru Ngosha ze Dong Lee Cho in whitedoug3 pius manasse vesta bertha micheal HARUFU HALELUYA MOSHI
 
Last edited by a moderator:
Nje huko tukawa tunatafuta sehemu nzuri ya kupata chakula na angalau kuvuta muda ili angalau mpaka saa 4 usiku turudi hotelini kwetu kulala. Tukabahatisha mgahawa mmoja. Tukaingia na kuomba huduma ya chakula. Tukaanza kupata chakula huku tunazungumzia safari yetu kwa maana ya tathimini mpaka hapa tulipofikia na yaliojiri ndani ya safari.

Mara ghafla Milgo huyu hapa! Milgo mbele, Fatma nyuma.

Waione wote wakiwemo: chiko18 NYANYADO Aristidi selestin Milugwi Heaven Sent icca peterchoka Gobe loveissweet miss nuru Ngosha ze Dong Lee Cho in whitedoug3 pius manasse vesta bertha micheal HARUFU HALELUYA MOSHI Pritty wa joseph

​Sehemu ya Tatu:

Nje huko tukawa tunatafuta sehemu nzuri ya kupata chakula na angalau kuvuta muda ili angalau mpaka saa 4 usiku turudi hotelini kwetu kulala. Tukabahatisha mgahawa mmoja. Tukaingia na kuomba huduma ya chakula. Tukaanza kupata chakula huku tunazungumzia safari yetu kwa maana ya tathimini mpaka hapa tulipofikia na yaliojiri ndani ya safari.

Mara ghafla Milgo huyu hapa! Milgo mbele, Fatma nyuma. Namna ambavyo mimi na John tulikaa katika ile meza, ni ule mtindo wa kutizamana, wakati Milgo na Fatma wakiingia, mimi ndio niliokuwa nikiwatazama, John alikuwa amewapa mgongo.

John hakuonyesha kushtushwa na kitendo changu cha kuhamisha macho, kuhamishia uelekeo wa mlangoni, walikokuwa wanaingilia wateja, wakati mimi nikishuhudia kitu ambacho kama siamini, John alikuwa amenikazia macho mimi.

Kichwani nilikuwa nawaza vitu vingi sana kuhusiana na mabinti hawa. Kubwa zaidi ni kuwa kulikoni na haka kagiza, mabinti bado hawajapata pa kulala, ama? Kingine niliwaza, labda ni ndoto ya alinacha, huenda natafutwa kwa minajili, Milgo ameshabadili uamuzi wake na yuko tayari kulala na mimi usiku huu wa kwanza, pengine labda baada ya kujadiliana na nduguye na hatimaye wakafikia consensus, au labda kimenuka, wanakuja kuniuzia kesi!

Yote kwa yote, sikuishiwa mawazo kichwani mwangu kwa tukio lile mpaka pale John aliponishtua. Na wakati nashtuliwa na John, tayari Milgo na Fatma walikuwa hawa hapa!

Wote wawili walionyesha furaha yao baada ya kutuona sisi pale, tukipata chakula kwa umoja wetu. Wakatusalimia na kutufahamisha kuwa wamefanikiwa kukutana na wenyeji wao, ambao ni wasomali wenzao, wakazi wa Tunduma, na kwamba hata hapo Hotelini wameongozana nao, ila wamebaki nje. Milgo akanifahamisha kuwa wapo katika kutafuta vitafunwa ili wakapate chai huko watakapoenda kulala.

Kama mwanaume, tena mwenye tamaa na vitu vizuri, pale pale nikakosa amani, nikajawa na inda, maumivu ya moyo yakaibuka, nikaumia sana ndani, kichwa kikawa kizito. Kisa ni WIVU. Wivu wa mapenzi.
Sikufurahia taarifa ile ya Milgo hata kidogo. Nafsi ikashindwa kuhimili mikikimikiki ya wivu, sura ikakubali kupokea kile kinapita moyoni mwangu. Uso ukajawa na huzuni. Nikashindwa kuficha hisia zangu, maumivu. Macho yakabadilika rangi.

Mawazo.
Nikaanza kuwaza kuwa kuna mtu atajilia vyake kiulaini, tena anajilia kiulaini mzigo bint ambae nimekuwa nae kutwa nzima ya leo, sio tu kuwa nae, bali pia ukweli kwamba nimejimilikisha bint baada ya yeye mwenyewe kuonyesha nia ya kumilikiwa na MSAFIRI QAFIRI!

Nikawaza ule uzuri wa Milgo. Nikawaza alivokuwa ananikumbatia. Kwa kifupi picha zote za akilini kati yangu mimi na Milgo, za kutwa nzima zikaanza kunijia akilini, mithili ya mtu ninaeota vile, ikaja na ile picha ya pale kitandani wakati Milgo alipojipa cheo kuwa AFISA UKAGUZI, akakikagua chumba ambacho kumbe hatakilala! Milgo akakikagua na kitanda mbele ya macho yangu, na bado haikutosha, akakisifia kitanda kuashiria kwamba yuko tayari kwa tukio kabla hajaniruka mita 1000!

Niliumia zaidi baada ya kujipa hisia kuwa haya ndio malipo ninayolipwa na bint huyu, kwamba hii ni adhabu, na kwamba adhabu hii inakujaje wakati kama huu? Kwamba mapema sana kwa safari yetu, tayari yanajitokeza haya! Nilishindwa kushangaa!

Lakini kingine hiki. Je kesho kutakapokucha, nitawezaje kumuona tena? Nitampata wapi? Safari yetu kwa kesho, ya kuvuka boda, ni jioni, je huyu mrembo nitampata wapi kwa kutwa ya kesho angalau nifanye ile watoto wa kijiweni wanasema "force king!"

Picha zilikatika ghafla baada ya John kunitaka niitikie salamu ya "good night" niliopewa na Milgo na Fatma kwa pamoja. Sikumbuki kama niliitikia na hata kama niliitikia, sikumbuki niliitikiaje!

Kilicho dhahiri ni kwamba Milgo na Fatma waliondoka wakijua kuwa, taarifa yao walioileta kwetu, mimi na John, usiku ule, pale mgahawani, haikuwa njema. Ilikuwa ni taarifa mbaya, tena kwa nyakati mbaya. Kwa mara nyingine tena nikaingia katika majuto, majuto ya kujitakia. John hakuonyesha hata dalili moja ya kujutia, wala kunionea huruma. Nadhani na yeye alikuwa na msimamo kuwa haya yanayonikuta, nimejitakia mwenyewe, sipaswi kuonewa huruma!

Tukarudi hotelini. Tukazungumza kidogo na John. John akanipa tathimini yake ya safari, na mimi nikampa yangu. Ni kama vile John alisahau yote yalomkwaza wakati wote wa safari, John aliongea kwa utulivu wa kipekee, na kwa upole sana. Ikanifanya nimsikilize kwa umakini wa ziada.

John alinielezea namna alivojiandaa na safari hii kwao Kampala, Uganda, safari ya Johannesburg, kwamba ukiacha maandalizi ya kifedha na mambo mengine, alishajiandaa kisaikolojia kuwa, safari itakuwa ngumu, yenye changamoto nyingi, lakini katika kile ambacho anasema, anamshukuru Mungu, ni kwamba mpaka sasa anakaribia kuiacha ardhi ya Tanzania, mambo yako sawia.

Anasema ameifurahia safari. Safari imekuwa ya amani na ya kuvutia kwa upande wake. Anasema haya yote anayaona kuwa yana mchango wa moja kwa moja wa mimi, rafiki yake ambae, anasema nina roho ya kipekee! Anasema nimehusika kuifanya safari hii iwe nzuri kwake. Anasema anamshukuru Mungu kwa hili, na anaomba sana, rafiki yake nisibadilike!

Binafsi nilimuelewa, nikamshukuru kwa kutambua nafasi nilionayo mimi rafiki yake katika safari yetu, lakini pia nikamhakikishia kuwa, mimi na yeye ni kama ndugu, si marafiki tena, nitakuwa nae pamoja mpaka mwisho wa safari yetu.

Tuliendelea kujadili vitu vingi sana, ni kama sio sisi ambao muda mchache uliopita, ndani ya chumba hiki hiki tulikuwa tunabishana nani awe wa kwanza kuoga! Sasa hivi tunaongea na kucheka pamoja kama ndugu mapacha wanaopendana, sikumbuki nani alikuwa wa kwanza kupata usingizi, ila tu nilikuwa wa kwanza kushtuka kukiwa kumepambazuka!

Nilitumia lisaa limoja pale juu ya kitanda cha nyumba ile ya wageni, ili kuwaza na kuwazua, nikipanga na kupangua wazo moja baada ya jingine. Niliwaza kama niko sahihi kimaamuzi, niliwaza kama ndoto zangu kuhusu safari hii zitatimia! Nilitumia muda ule kuwakumbuka ndugu na jamaa zangu niliowaacha, wengi wakiwa Tabora, wengine Morogoro, na kadhaa wa Dodoma na Dsm.

Nikamkumbuka girlfriend wangu wa tangu A level. Nikamkumbuka namna alivokuwa ananibishia kuwa nisifanye safari hii. Alinisihi sana kuendelea kupambana hapa hapa bongo, alinipa hoja kuwa kwa elimu yangu ya chuo, nisingesota sana mtaani kabla ya kutoboa! Alisema anaamini sana juu ya uwezo wangu wa kuchakarika! Alidai kuwa, namna anavonijua kuwa mimi ni mpambanaji, basi hata ndani ya bongo, maisha ningeyapatia!

Maskini Lilly wa watu, hakuna nilichomkubalia, alisononeka, alinyong'onyea, alilia sana juu ya uamuzi wangu! Mwisho nakumbaka aliniombea sana kwa Mungu, nifanikiwe katika safari yangu na kule niendako, kwa ahadi kuwa atakuwa na mimi kwa kila hatua!

Kwa lilly, South Africa ni nchi wanayokimbilia vijana wasio na kazi, vijana walioshindwa maisha bongo, vibaka na wavuta bangi flani hivi wa mtaani! Lilly hakuwahi kudhani wala kujua kuwa mtu mwenye elimu ya chuo, kama mimi, ningeweza kujiwa na mawazo kama haya yaliopelekea mimi kuanzisha safari hii!

Huyu Lilly. Uhuhsiano wetu ulianzia katika harakati za kielemu high school. Sikusoma nae shule moja, ilikuwa ni katika tuition zinazohusisha wanafunzi wa kutoka mashule mbali mbali, ya jijini Dsm. Nakumbuka nilivompata Lilly. Ilikuwa ni katika ule utaratibu wa walimu wa tuition kuwafanyisha pepa wanafunzi wao kila Jumamosi, ilitokea pepa moja ambayo nilipasua kwa kupiga banda, na hakukuwa na banda lingine katika ile test pepa na bahati mbaya siku ya kurudishiwa hizo pepa, sikuwepo!

Yule mwalimu huwa hataki kubaki na pepa za wanafunzi, akalazimisha mtu anipokelee, hakupatikana mtu, lakini mwishoni mwa kipindi, Lilly alijitolea kwenda kuichukua ile pepa kwa ahadi kuwa atanifikishia mimi mhusika. Tangu Lilly anikabidhi pepa ile, nikamganda, na hatimaye tukafungua ukurasa mpya wa mapenzi!

Kwa hofu ya kumuumiza na kupata upinzani, safari ya DSM kwenda Cape town nilimficha. Na huu ulikuwa ni ujinga ambao nilikiri kwake baadae, mpaka nagonga visa ya South Africa, ya siku 90, Lilly wangu hakuwa anajua kitu, hakuwa anajua kuwa mimi ni MSAFIRI.

Sikumbuki vizuri, kama nilipatwa na akili gani, lakini tangu nigonge visa, sikuwahi kutembea bila ya passport. Kila nilipokwenda, nilikuwa nayo katika mkoba. Ikatokea siku moja nina ahadi ya kukutana na Lilly kwa maana ya kwenda kuiridhisha miili yetu, pia nilikuwa nayo.

Kama kawaida, tulikutana sehemu yetu ile ile tulioizoea, Lilly akiwa mtoto wa Tabata, na mimi nikiwa mtoto wa Temeke, nilibahatika kulijua chimbo moja hivi maeneo ya Buguruni, nyuma ya soko maarufu la Mnyamani, jirani na hospitali ya Buguruni, mkono wa kulia kama Unaeelekea Vingunguti, kulikuwa na lodge imejichanganya katikati ya makazi ya uswahilini.

Ndani chumbani, kila kitu ndani kwa ndani, ni kama vile Lilly alijua kuwa nakaribia kusafiri na kwamba nitam-miss, alinipa ile wajuzi wa mambo wanasema mseto wa hardcore seksi na crazy seksi! Lilikuwa ni tukio la kipekee sana, huwa inatokea mara chache sana!

Ilipigwa game ambayo hata yeye mwenyewe alihoji kuwa amepatwa na nini ile siku? Zile style ambazo Lilly huwa mbishi nazo, leo alikuwa anazianzisha mwenyewe! Kuna style ambazo alikuwa hazitaki, si tu kuzifanya bali hata kuziskia, lakini kwa siku hii niliruhusiwa!

Ni katika game hii hii, ndio kwa mara ya kwanza lilly aliniomba tushushe godoro chini, na nilipotaka kujua kulikoni, alitoa hoja kuwa linampunguzia ufanisi wake na kwamba pia kuna kitu special anataka kunionyesha!

Nikakubali.
Nikajikakamua mtoto wa kiume, nikalishusha godoro chini! Nipo tayari kuonyeshwa kitu special kwa ufanisi sahihi.

Waione: chiko18 NYANYADO Aristidi selestin Milugwi Heaven Sent icca peterchoka Gobe loveissweet miss nuru Ngosha ze Dong Lee Cho in whitedoug3 pius manasse vesta bertha micheal HARUFU HALELUYA MOSHI Pritty wa joseph
 
Last edited by a moderator:
Nje huko tukawa tunatafuta sehemu nzuri ya kupata chakula na angalau kuvuta muda ili angalau mpaka saa 4 usiku turudi hotelini kwetu kulala. Tukabahatisha mgahawa mmoja. Tukaingia na kuomba huduma ya chakula. Tukaanza kupata chakula huku tunazungumzia safari yetu kwa maana ya tathimini mpaka hapa tulipofikia na yaliojiri ndani ya safari.

Mara ghafla Milgo huyu hapa! Milgo mbele, Fatma nyuma.

Waione wote wakiwemo: chiko18 NYANYADO Aristidi selestin Milugwi Heaven Sent icca peterchoka Gobe loveissweet miss nuru Ngosha ze Dong Lee Cho in whitedoug3 pius manasse vesta bertha micheal HARUFU HALELUYA MOSHI Pritty wa joseph

Sehemu ya Tatu:

Nje huko tukawa tunatafuta sehemu nzuri ya kupata chakula na angalau kuvuta muda ili angalau mpaka saa 4 usiku turudi hotelini kwetu kulala. Tukabahatisha mgahawa mmoja. Tukaingia na kuomba huduma ya chakula. Tukaanza kupata chakula huku tunazungumzia safari yetu kwa maana ya tathimini mpaka hapa tulipofikia na yaliojiri ndani ya safari.

Mara ghafla Milgo huyu hapa! Milgo mbele, Fatma nyuma. Namna ambavyo mimi na John tulikaa katika ile meza, ni ule mtindo wa kutizamana, wakati Milgo na Fatma wakiingia, mimi ndio niliokuwa nikiwatazama, John alikuwa amewapa mgongo.

John hakuonyesha kushtushwa na kitendo changu cha kuhamisha macho, kuhamishia uelekeo wa mlangoni, walikokuwa wanaingilia wateja, wakati mimi nikishuhudia kitu ambacho kama siamini, John alikuwa amenikazia macho mimi.

Kichwani nilikuwa nawaza vitu vingi sana kuhusiana na mabinti hawa. Kubwa zaidi ni kuwa kulikoni na haka kagiza, mabinti bado hawajapata pa kulala, ama? Kingine niliwaza, labda ni ndoto ya alinacha, huenda natafutwa kwa minajili, Milgo ameshabadili uamuzi wake na yuko tayari kulala na mimi usiku huu wa kwanza, pengine labda baada ya kujadiliana na nduguye na hatimaye wakafikia consensus, au labda kimenuka, wanakuja kuniuzia kesi!

Yote kwa yote, sikuishiwa mawazo kichwani mwangu kwa tukio lile mpaka pale John aliponishtua. Na wakati nashtuliwa na John, tayari Milgo na Fatma walikuwa hawa hapa!

Wote wawili walionyesha furaha yao baada ya kutuona sisi pale, tukipata chakula kwa umoja wetu. Wakatusalimia na kutufahamisha kuwa wamefanikiwa kukutana na wenyeji wao, ambao ni wasomali wenzao, wakazi wa Tunduma, na kwamba hata hapo Hotelini wameongozana nao, ila wamebaki nje. Milgo akanifahamisha kuwa wapo katika kutafuta vitafunwa ili wakapate chai huko watakapoenda kulala.

Kama mwanaume, tena mwenye tamaa na vitu vizuri, pale pale nikakosa amani, nikajawa na inda, maumivu ya moyo yakaibuka, nikaumia sana ndani, kichwa kikawa kizito. Kisa ni WIVU. Wivu wa mapenzi.
Sikufurahia taarifa ile ya Milgo hata kidogo. Nafsi ikashindwa kuhimili mikikimikiki ya wivu, sura ikakubali kupokea kile kinapita moyoni mwangu. Uso ukajawa na huzuni. Nikashindwa kuficha hisia zangu, maumivu. Macho yakabadilika rangi.

Mawazo.
Nikaanza kuwaza kuwa kuna mtu atajilia vyake kiulaini, tena anajilia kiulaini mzigo bint ambae nimekuwa nae kutwa nzima ya leo, sio tu kuwa nae, bali pia ukweli kwamba nimejimilikisha bint baada ya yeye mwenyewe kuonyesha nia ya kumilikiwa na MSAFIRI QAFIRI!

Nikawaza ule uzuri wa Milgo. Nikawaza alivokuwa ananikumbatia. Kwa kifupi picha zote za akilini kati yangu mimi na Milgo, za kutwa nzima zikaanza kunijia akilini, mithili ya mtu ninaeota vile, ikaja na ile picha ya pale kitandani wakati Milgo alipojipa cheo kuwa AFISA UKAGUZI, akakikagua chumba ambacho kumbe hatakilala! Milgo akakikagua na kitanda mbele ya macho yangu, na bado haikutosha, akakisifia kitanda kuashiria kwamba yuko tayari kwa tukio kabla hajaniruka mita 1000!

Niliumia zaidi baada ya kujipa hisia kuwa haya ndio malipo ninayolipwa na bint huyu, kwamba hii ni adhabu, na kwamba adhabu hii inakujaje wakati kama huu? Kwamba mapema sana kwa safari yetu, tayari yanajitokeza haya! Nilishindwa kushangaa!

Lakini kingine hiki. Je kesho kutakapokucha, nitawezaje kumuona tena? Nitampata wapi? Safari yetu kwa kesho, ya kuvuka boda, ni jioni, je huyu mrembo nitampata wapi kwa kutwa ya kesho angalau nifanye ile watoto wa kijiweni wanasema “force king!”

Picha zilikatika ghafla baada ya John kunitaka niitikie salamu ya “good night” niliopewa na Milgo na Fatma kwa pamoja. Sikumbuki kama niliitikia na hata kama niliitikia, sikumbuki niliitikiaje!

Kilicho dhahiri ni kwamba Milgo na Fatma waliondoka wakijua kuwa, taarifa yao walioileta kwetu, mimi na John, usiku ule, pale mgahawani, haikuwa njema. Ilikuwa ni taarifa mbaya, tena kwa nyakati mbaya. Kwa mara nyingine tena nikaingia katika majuto, majuto ya kujitakia. John hakuonyesha hata dalili moja ya kujutia, wala kunionea huruma. Nadhani na yeye alikuwa na msimamo kuwa haya yanayonikuta, nimejitakia mwenyewe, sipaswi kuonewa huruma!

Tukarudi hotelini. Tukazungumza kidogo na John. John akanipa tathimini yake ya safari, na mimi nikampa yangu. Ni kama vile John alisahau yote yalomkwaza wakati wote wa safari, John aliongea kwa utulivu wa kipekee, na kwa upole sana. Ikanifanya nimsikilize kwa umakini wa ziada.

John alinielezea namna alivojiandaa na safari hii kwao Kampala, Uganda, safari ya Johannesburg, kwamba ukiacha maandalizi ya kifedha na mambo mengine, alishajiandaa kisaikolojia kuwa, safari itakuwa ngumu, yenye changamoto nyingi, lakini katika kile ambacho anasema, anamshukuru Mungu, ni kwamba mpaka sasa anakaribia kuiacha ardhi ya Tanzania, mambo yako sawia.

Anasema ameifurahia safari. Safari imekuwa ya amani na ya kuvutia kwa upande wake. Anasema haya yote anayaona kuwa yana mchango wa moja kwa moja wa mimi, rafiki yake ambae, anasema nina roho ya kipekee! Anasema nimehusika kuifanya safari hii iwe nzuri kwake. Anasema anamshukuru Mungu kwa hili, na anaomba sana, rafiki yake nisibadilike!

Binafsi nilimuelewa, nikamshukuru kwa kutambua nafasi nilionayo mimi rafiki yake katika safari yetu, lakini pia nikamhakikishia kuwa, mimi na yeye ni kama ndugu, si marafiki tena, nitakuwa nae pamoja mpaka mwisho wa safari yetu.

Tuliendelea kujadili vitu vingi sana, ni kama sio sisi ambao muda mchache uliopita, ndani ya chumba hiki hiki tulikuwa tunabishana nani awe wa kwanza kuoga! Sasa hivi tunaongea na kucheka pamoja kama ndugu mapacha wanaopendana, sikumbuki nani alikuwa wa kwanza kupata usingizi, ila tu nilikuwa wa kwanza kushtuka kukiwa kumepambazuka!

Nilitumia lisaa limoja pale juu ya kitanda cha nyumba ile ya wageni, ili kuwaza na kuwazua, nikipanga na kupangua wazo moja baada ya jingine. Niliwaza kama niko sahihi kimaamuzi, niliwaza kama ndoto zangu kuhusu safari hii zitatimia! Nilitumia muda ule kuwakumbuka ndugu na jamaa zangu niliowaacha, wengi wakiwa Tabora, wengine Morogoro, na kadhaa wa Dodoma na Dsm.

Nikamkumbuka girlfriend wangu wa tangu A level. Nikamkumbuka namna alivokuwa ananibishia kuwa nisifanye safari hii. Alinisihi sana kuendelea kupambana hapa hapa bongo, alinipa hoja kuwa kwa elimu yangu ya chuo, nisingesota sana mtaani kabla ya kutoboa! Alisema anaamini sana juu ya uwezo wangu wa kuchakarika! Alidai kuwa, namna anavonijua kuwa mimi ni mpambanaji, basi hata ndani ya bongo, maisha ningeyapatia!

Maskini Lilly wa watu, hakuna nilichomkubalia, alisononeka, alinyong’onyea, alilia sana juu ya uamuzi wangu! Mwisho nakumbaka aliniombea sana kwa Mungu, nifanikiwe katika safari yangu na kule niendako, kwa ahadi kuwa atakuwa na mimi kwa kila hatua!

Kwa lilly, South Africa ni nchi wanayokimbilia vijana wasio na kazi, vijana walioshindwa maisha bongo, vibaka na wavuta bangi flani hivi wa mtaani! Lilly hakuwahi kudhani wala kujua kuwa mtu mwenye elimu ya chuo, kama mimi, ningeweza kujiwa na mawazo kama haya yaliopelekea mimi kuanzisha safari hii!

Huyu Lilly. Uhuhsiano wetu ulianzia katika harakati za kielemu high school. Sikusoma nae shule moja, ilikuwa ni katika tuition zinazohusisha wanafunzi wa kutoka mashule mbali mbali, ya jijini Dsm. Nakumbuka nilivompata Lilly. Ilikuwa ni katika ule utaratibu wa walimu wa tuition kuwafanyisha pepa wanafunzi wao kila Jumamosi, ilitokea pepa moja ambayo nilipasua kwa kupiga banda, na hakukuwa na banda lingine katika ile test pepa na bahati mbaya siku ya kurudishiwa hizo pepa, sikuwepo!

Yule mwalimu huwa hataki kubaki na pepa za wanafunzi, akalazimisha mtu anipokelee, hakupatikana mtu, lakini mwishoni mwa kipindi, Lilly alijitolea kwenda kuichukua ile pepa kwa ahadi kuwa atanifikishia mimi mhusika. Tangu Lilly anikabidhi pepa ile, nikamganda, na hatimaye tukafungua ukurasa mpya wa mapenzi!

Kwa hofu ya kumuumiza na kupata upinzani, safari ya DSM kwenda Cape town nilimficha. Na huu ulikuwa ni ujinga ambao nilikiri kwake baadae, mpaka nagonga visa ya South Africa, ya siku 90, Lilly wangu hakuwa anajua kitu, hakuwa anajua kuwa mimi ni MSAFIRI.

Sikumbuki vizuri, kama nilipatwa na akili gani, lakini tangu nigonge visa, sikuwahi kutembea bila ya passport. Kila nilipokwenda, nilikuwa nayo katika mkoba. Ikatokea siku moja nina ahadi ya kukutana na Lilly kwa maana ya kwenda kuiridhisha miili yetu, pia nilikuwa nayo.

Kama kawaida, tulikutana sehemu yetu ile ile tulioizoea, Lilly akiwa mtoto wa Tabata, na mimi nikiwa mtoto wa Temeke, nilibahatika kulijua chimbo moja hivi maeneo ya Buguruni, nyuma ya soko maarufu la Mnyamani, jirani na hospitali ya Buguruni, mkono wa kulia kama Unaeelekea Vingunguti, kulikuwa na lodge imejichanganya katikati ya makazi ya uswahilini.

Ndani chumbani, kila kitu ndani kwa ndani, ni kama vile Lilly alijua kuwa nakaribia kusafiri na kwamba nitam-miss, alinipa ile wajuzi wa mambo wanasema mseto wa hardcore seksi na crazy seksi! Lilikuwa ni tukio la kipekee sana, huwa inatokea mara chache sana!

Ilipigwa game ambayo hata yeye mwenyewe alihoji kuwa amepatwa na nini ile siku? Zile style ambazo Lilly huwa mbishi nazo, leo alikuwa anazianzisha mwenyewe! Kuna style ambazo alikuwa hazitaki, si tu kuzifanya bali hata kuziskia, lakini kwa siku hii niliruhusiwa!

Ni katika game hii hii, ndio kwa mara ya kwanza lilly aliniomba tushushe godoro chini, na nilipotaka kujua kulikoni, alitoa hoja kuwa linampunguzia ufanisi wake na kwamba pia kuna kitu special anataka kunionyesha!

Nikakubali.
Nikajikakamua mtoto wa kiume, nikalishusha godoro chini! Nipo tayari kuonyeshwa kitu special kwa ufanisi sahihi.

Waione: chiko18 NYANYADO Aristidi selestin Milugwi Heaven Sent icca peterchoka Gobe loveissweet miss nuru Ngosha ze Dong Lee Cho in whitedoug3 pius manasse vesta bertha micheal HARUFU HALELUYA MOSHI Pritty wa joseph

haya mkuu shukran
 
Last edited by a moderator:
Ahsante sana Kiongozi.

Tena umefanya vizuri sana kumalizia na sehemu ya tatu kabisa, maana ungetuacha sehemu ya pili uhondo ungetukatisha tukabaki kusubiria kwa shingo upande.

Imetulia sana.

Nitaitafutia muda niipitie tena kuanzia sehemu ya kwanza hadi sehemu ya tatu
 
habari yako mkuu JOSEPHKoomson Slim5 vipi mwendelezo wa hii riwaya yetu maana ni muda mrefu umepita
 
Last edited by a moderator:
Last edited by a moderator:
vp kaka , au umekamatwa na skari wa tunduma? maana kimya kimezidi
 
Narudi wadau. Makontena na Bomoa bomoa vilintoa nje ya Reli!
 
>>Nahisi nipo peponi,nikiona sura yako.
Penzi lako la thamani,hakuna mfano wako.
Napata hamu moyoni,kushika kiganja chako.
Kilichokuwa laini,nalainika mwenzako.
Nikuonapo usoni,ni nyororo ngozi yako.
Sikuachi asilani,milele mimi ni wako.
Wewe ni wangu mwandani,nifanye chaguo lako.
Nitie ndani moyoni,nisije kufa mwenzako.
Kwani kwangu u moyoni,kukuacha mimi mwiko.
Sebuleni na chumbani,kwangu uje kuwa jiko.
Ni shuka langu la ndani,kwako sina hangaiko.
Nitatulia kitini,nije pata pumziko.
Nisemeze sikioni,linitoke sikitiko.
Mrembo hadi gizani,hata hujapakwa piko.
Ungelikuwa angani,malaika peke yako.
Utamu wako mezani,nilizuri pishi lako.
Oho malaika wangu,ipooze roho yangu.
Kwako sipati uchungu,upo kwenye moyo wangu.
Nishike mkono wangu,utazame mboni yangu.
Utajiona mwenzangu,wewe ulo chungu changu.
Ivisha chakula changu,kitamu kiso kichungu.
Zawadi toka kwa mungu,ilofika hapa kwangu.
Naapa haki ya mungu,paka kifo wewe wangu.
Niseme nini mwenzako,nahisi nipo peponi.
Mazuri mahaba yako,yasiyouzwa sokoni.
Mazuri mahaba yako, hayapo hata dukani.
Shairi:NAHISI NIPO PEPONI.
Mtunzi:Idd Ninga wa Tengeru Arusha.
0655519736.
 
>>Nahisi nipo peponi,nikiona sura yako.
Penzi lako la thamani,hakuna mfano wako.
Napata hamu moyoni,kushika kiganja chako.
Kilichokuwa laini,nalainika mwenzako.
Nikuonapo usoni,ni nyororo ngozi yako.
Sikuachi asilani,milele mimi ni wako.
Wewe ni wangu mwandani,nifanye chaguo lako.
Nitie ndani moyoni,nisije kufa mwenzako.
Kwani kwangu u moyoni,kukuacha mimi mwiko.
Sebuleni na chumbani,kwangu uje kuwa jiko.
Ni shuka langu la ndani,kwako sina hangaiko.
Nitatulia kitini,nije pata pumziko.
Nisemeze sikioni,linitoke sikitiko.
Mrembo hadi gizani,hata hujapakwa piko.
Ungelikuwa angani,malaika peke yako.
Utamu wako mezani,nilizuri pishi lako.
Oho malaika wangu,ipooze roho yangu.
Kwako sipati uchungu,upo kwenye moyo wangu.
Nishike mkono wangu,utazame mboni yangu.
Utajiona mwenzangu,wewe ulo chungu changu.
Ivisha chakula changu,kitamu kiso kichungu.
Zawadi toka kwa mungu,ilofika hapa kwangu.
Naapa haki ya mungu,paka kifo wewe wangu.
Niseme nini mwenzako,nahisi nipo peponi.
Mazuri mahaba yako,yasiyouzwa sokoni.
Mazuri mahaba yako, hayapo hata dukani.
Shairi:NAHISI NIPO PEPONI.
Mtunzi:Idd Ninga wa Tengeru Arusha.
0655519736.


Mkuu upon vizuri, safi sana
 
Back
Top Bottom