Kwa lugha nyepesi ni kuwa huyo mpenzi wako hakupendi ninapo sema hivyo nina maanisha kuwa ametoka nje kabisa ya dhumuni la mapenzi ambapo ni kusaidiana kwenye shida na raha na kutiana moyo wakati wa kipindi kigumu huku mkipeana matumaini yenye mafanikio.
Mpenzi anayekupenda kutoka moyoni hawezi kuwa miongoni mwa wanaokurudisha nyuma bali miongoni mwa watu wanaokupa moyo ili usonge mbele mpenzi anayekupenda kwa dhati hawezi kuwa miongoni mwa watu wanaofurahia anguko lako au mateso yako bali anatakiwa awe ni mtu anayepambana na wewe bega kwa bega katika kuyakabili mahangaiko yako na kukufariji na kukupa moyo pale unapotaka kukata tamaa.
Kama mpenzi wako anaona upo kwenye kipindi kigumu alafu anapuuza au kukwamisha juhudi zako za kujikwamua kutoka hapo ulipo tambua kuwa huyo si mtu mzuri kwenye maisha yako na yakufaa kumuepuka mara moja kwa wakati huu usiupe moyo wako nafasi ya kuamua jambo zito kama hili kwani moyo unaongozwa na hisia za kimapenzi bali unatakiwa utumie uhalisia wa jambo na akili yako kufanya maamuzi.
Jaribu kuwatazama watu walionyuma yako wanahitaji msaada wako ,jaribu kuthamini juhudi za waliokufikisha hapo ulipo sahihi tathimini hasara na jitihada walizoonyesha wazazi wako hadi kukufikisha hapo je ungependa hayo yote yapotee kwa sababu mtu mmoja mpuuzi mliyekutana tu maishani.
Je upo ladhi kumwona mzazi wako akiteseka kwa kukosa msaada wako kwa ajili ya mtu asiye jua hata uchungu wa mahangaiko waliyopitia wazee wako hadi wewe kufika hapo kuachana nae haimaanishi kuwa hautopata mwingine mzuri kama yeye isipokuwa utapumzika huku ukimsubiri yule aliyeumbwa spesho kwa ajili yako wanawake warembo wamejaa kila kona na kila pembe ya dunia.
THINK BIG
Habari wana Jamii forums.
Naingia kwenye jukwaa hili kwa mara ya kwanza nami kutafuta ushauri juu ya yanayonisibu. Najua Jamii forums ni elimu tosha kwa kuwepo watu wa aina tofauti tofauti.
Mimi ni kijana niliyemaliza chuo mwaka juzi mkoani mwanza katika chuo kimoja maarufu. Kwa sasa nafanya vibarua tu vya kuunga unga ili kusogeza siku, nina mpenzi ambaye naye kwa mwaka na nusu sasa na tunapendana sana.
Mwaka huu nahisi nitapata bahati ya kuingia katika jeshi la wananchi. Sasa tatizo ni kwamba mpenzi wangu huyu hataki mimi niende huko na kwamba nitakaponyanyua tu mguu kwenda huko na huku nyuma ndo basi tena sina changu.
Kiukweli nami nampenda sana na sijui nifanyeje kwa kweli. Wana Jamii forums najua kuna watu wana busara na hekima zao humu ambao wana uwezo wa kutoa kitu kitakachonisaidia mimi na wengine juu ya hili.
Nawasilisha.
Mkuu huwa unatumia kinywaji gani?
Kwa lugha nyepesi ni kuwa huyo mpenzi wako hakupendi ninapo sema hivyo nina maanisha kuwa ametoka nje kabisa ya dhumuni la mapenzi ambapo ni kusaidiana kwenye shida na raha na kutiana moyo wakati wa kipindi kigumu huku mkipeana matumaini yenye mafanikio.
Mpenzi anayekupenda kutoka moyoni hawezi kuwa miongoni mwa wanaokurudisha nyuma bali miongoni mwa watu wanaokupa moyo ili usonge mbele mpenzi anayekupenda kwa dhati hawezi kuwa miongoni mwa watu wanaofurahia anguko lako au mateso yako bali anatakiwa awe ni mtu anayepambana na wewe bega kwa bega katika kuyakabili mahangaiko yako na kukufariji na kukupa moyo pale unapotaka kukata tamaa.
Kama mpenzi wako anaona upo kwenye kipindi kigumu alafu anapuuza au kukwamisha juhudi zako za kujikwamua kutoka hapo ulipo tambua kuwa huyo si mtu mzuri kwenye maisha yako na yakufaa kumuepuka mara moja kwa wakati huu usiupe moyo wako nafasi ya kuamua jambo zito kama hili kwani moyo unaongozwa na hisia za kimapenzi bali unatakiwa utumie uhalisia wa jambo na akili yako kufanya maamuzi.
Jaribu kuwatazama watu walionyuma yako wanahitaji msaada wako ,jaribu kuthamini juhudi za waliokufikisha hapo ulipo sahihi tathimini hasara na jitihada walizoonyesha wazazi wako hadi kukufikisha hapo je ungependa hayo yote yapotee kwa sababu mtu mmoja mpuuzi mliyekutana tu maishani.
Je upo ladhi kumwona mzazi wako akiteseka kwa kukosa msaada wako kwa ajili ya mtu asiye jua hata uchungu wa mahangaiko waliyopitia wazee wako hadi wewe kufika hapo kuachana nae haimaanishi kuwa hautopata mwingine mzuri kama yeye isipokuwa utapumzika huku ukimsubiri yule aliyeumbwa spesho kwa ajili yako wanawake warembo wamejaa kila kona na kila pembe ya dunia.
THINK BIG
Sioni kama msimamo wa msichana ni wa kukosa upendo. Asiye na upendo atakuruhusu hata kufanya ujambazi mradi ale na siku ukiuwawa au kutiwa mbaroni anahamia kwa mwingine siku hiyo hiyo. Anayekuchagulia kazi ya kufanya "anakupenda sana". Yeye si anaona shida unazopata? Na pengine hata mahitaji ya msingi humtimizii lakini anavumilia ili mradi upate kazi atayoridhika nayo.
Tukija kwenye kazi ya jeshi tambua kuwa kazi ya msingi ya mwanajeshi ni "kuua". Hizo lugha za "kulinda mipaka ya nchi" ni kuzunguka tu. Mtu mwingine lile wazo la kuajiriwa kazi ya "kuua" halikubaliki akilini mwake. Na mke anaweza kuhofu kuwa ukatili unaojifunza jeshini unaweza kuuhamishia nyumbani pale atakapokuudhi!
Pia huenda anahofia ujane wa mapema maana unaweza kutumwa Nigeria kupambana na boko haram likarudi jeneza!
Pia fikiria askari kutumwa nje ya nchi na kukaa miaka 3 huko bila kuonana na familia!
Kwa hiyo binti ni lazima asikilkilizwe na suala hili lisihusishwe na upendo maana tatizo si upendo ni aina ya kazi.
Nenda jeshini kwanza, ukishamaliza halafu ukarudi na kukuta ameolewa unaenda kufata platoon yote mliotoka mafunzoni kuja kuvamia wanapoishi na huyo mume wake mpya mnatembeza vipigo kwa wanaohucka na wasiohucka