Mpendazoe aanika walioanzisha CCJ

Hawa wanasiasa wananichanganya hata siwaelewi..huyu mpendazoe nae anakurupuka sana.
Mkuu si kukurupuka huu ndo muda muafaka kuwaumbua, akina Sitta walikuwa kwenye sherehe kufanikiwa kuwavuruga akina Lowassa, sasa CDM wamewapiga kuwavuruga zaidi.

Hii ni furaha kwa kina Lowassa hivyo hapo CCM inazidi kubaki halijojo. Lakini pia hawa wakina Sitta ni wanafiki, mara nyingi wanakuwa wakali maslahi yao yakiguswa na wanatumia uchafu wa wenzao si kwa maslahi ya taifa rejea issue ya Richmond uwajue vizuri hawa watu na sasa CCJ yale yale!
 
wakuu hii habari inazidi kuwavuruga ccm,fikiria akina sitta na lowasa na mkulu na wale fata upepo meza moja nini watazungumza as a team?
 
Mpendazoe aliwahi kuulizwa kama yeye ni mwanzilishi wa CCJ akasema hapana,leo anasema yeye ni miongoni mwa Wanzilishi! Hopeless kabisa!
umetumwa na nape? kazi unayo hoja imeeleweka sana kwamba nape,sitta,mwakyembe ni wachumia tumbo tu wanapiga kelele ili wapate nafasi wakipewa wanakaa kimya
 
wakuu hii habari inazidi kuwavuruga ccm,fikiria akina sitta na lowasa na mkulu na wale fata upepo meza moja nini watazungumza as a team?
Tena as team mazungumzo yawe ni jinsi ya kuidhibiti cdm na other national interest unafikiri watawaza na kutenda as a team tena? Maana hapa walipo hakuna unafiki tena lazima kundi moja linyanyue mikono juu na lingine lisamehe! Hayo yanawezekana?
 
Wakati ule alibembelezwa awataje akagoma,kwa sasa ni wrong time.Ni sawa na hadithi za kufikirika.Mi namuona sawa tu huyo Nape.Je CCJ ingeandikishwa angekua CDM?

Nadhani amesema kuwa CCJ ilikuwa iungane na CDM kupambana na ufisadi. Na ndio maana CDM ilijivuta kumtangaza mgombea wake wa uraisi, ni baada ya uasi huo wa kina Six na Mwakyembe, ngoma ilibidi ibadilishwe na Dr Slaa akaangukiwa ili aache kugombea ubunge ambapo alishachukua hata fomu akagombee uraisi. But nadhani mvuto wa Dr Slaa ni mara mia mbili ya hao kina Six na Mwakyembe, ooh na Nape loh, and i think CDM walifanya busara sana kumteua Dr Slaa

Nadhani Mpendazoe ni mzalendo wa kweli. Aliacha hata kiinua mgongo chake. But Nape alisema wamuulize Mpendazoe CCJ ilikufaje? Hilo ndo jambo la kujiuliza
 

Mukama: Chadema kiache ubabaishaji


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilson Mukama amekitaka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuacha kile alichodai kuwadanganya wananchi kwamba CCM kujivua gamba si kitu akisema hatua hiyo imefikiwa kukiimarisha chama baada ya kutambua kuwa bila hivyo nchi itayumba.

Mukama alisema hayo kwa nyakati tofauti juzi na jana katika Kijiji cha Kibara, wilayani Bunda na katika Kijiji cha Kaburabura, wilayani Musoma katika mikutano ya hadhara, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku nane mkoani Mara.

Alisema CCM kimetumia dhana hiyo ya kujivua gamba ili kiweze kurudi kwenye misingi imara, ikiwa ni pamoja na kufanya mabadiliko makubwa, hali ambayo itakiweka kwenye mstari unaotakiwa ambao lengo lake ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata maendeleo na huduma zote muhimu.


Alisema anawashangaa wapinzani wanaotumia muda mrefu kujadili falsafa ya kujivua gamba na kuhoji uwezo wao katika kutekeleza miradi ya maendeleo.

Alisema amesikitishwa na kauli ya viongozi wa Chadema kwamba kuna uwezekano Rais Kikwete kuondoka madarakani kabla ya 2015 kwa kutolea mfano wa Waziri Mkuu wa Japan aliyeondolewa madarakani.


Alifafanua kuwa viongozi wa Chadema wanatakiwa kufanya uchunguzi kabla ya kutoa matamko kwa maelezo kuwa Waziri Mkuu wa Japan hawezi kufananishwa na Rais Jakaya Kikwete kwa vile aliwekwa madarakani na Bunge wakati Rais alichaguliwa na wananchi.

Alisema kuwa, hata Mwalimu Julius Nyerere enzi za uhai wake aliwahi kutamka kuwa, bila CCM ya kweli nchi itayumba na kwamba ndiyo maana chama hicho kimeamua kutumia dhana hiyo ya kujivua gamba ili kiweze kuwa imara na kinachoweza kusimamia maendeleo ya wananchi.


"Tunakiweka katika misingi ya kukiimarisha ili kiwe chombo imara ambacho kweli kinaweza kusimamia maendeleo katika maeneo yetu tunayoishi. Sasa hawa Chadema wameichukua dhana hiyo ya kujivua gamba visivyo kabisa," alisema.


Alisema hiyo inatokana na viongozi wa Chadema kuwa na tabia ya kurukia mambo bila kuyafanyia uchunguzi na kwamba wameichukua dhana hiyo visivyo na kuendelea kuwarubuni wananchi ili wakichukie CCM na serikali yao... "Hawa wanataka kwenda Ikulu kwa maneno ya udanganyifu kabisa na maandamano yasiyokuwa na msingi wowote."


Pia alisema kuwa CCM haiwezi kufa kama upinzani wanavyoendelea kuwaambia wananchi, kwani ni chama kikubwa, taasisi na si kampuni ya kibiashara.

Aidha, Mukama amekiponda Chadema ambacho kimekuwa kikidai kwamba CCM imekumbatia wafanyabiashara na kueleza kuwa Chadema ndicho kinayofanya hivyo."Sasa watu wanaokumbatia sera ambazo mwalimu alikuwa anazipinga, eti ndio wanakwenda kwenye kaburi pale wanasema tunakuomba leo utusikilize tuweze kutawala nchi hii kidogo," alisema.


Alisema CCM kina matajiri wachache ambao wanataka kukitumia kwa ajili ya kujinufaisha na kuonya kuwa wafanyabiashara ambao maadili yao hayaendani na chama chao wataondolewa na kuwekwa pembeni mara moja
.


Amewataka wakuu wa wilaya nchini na viongozi wa CCM, kusimama imara na kuhakikisha fedha za miradi mbalimbali zinazoletwa na Serikali katika halmashauri husika, zinafanya kazi iliyokusudiwa na si kuishia kwenye mikono ya wajanja wachache.


Alisema kuwa ni lazima wakuu wa wilaya pamoja na viongozi wa chama hicho watekeleze wajibu wao ipasavyo wa kusimamia fedha za Serikali zinazopelekwa kwenye halmashauri.Habari hii imeandaliwa na Boniface Meena, Njombe; Ahmed Makongo na Christopher Maregesi, Bunda na Beldina Nyakeke, Musoma Vijijini.
Jamani hivi CCM huko kinatenda mambo yake kichama au kila mtu kivyake vyakena wanaunganishwa na ufisadi na sare ya kijani?

Ukichunguza kauli za viongozi wake kuanzia JK utagundua ya kua hotuba zao haziandaliwi kwa makini au hakuna maadalizi yoyote kila mtu anazungumza linalomuijia kinywani nyingi zimejaa ubabaishaji na hazina mantiki.Mfano mzuri jaribu kuipitia hiyo katibu Mkuu wa CCM Mukama mwanzo nilikua nafikiri ya kua tatizo ni Makamba sasa nimegundua ya kua tatatizo ni CCM yenyewe yoyote atakaebadilishwa katika nafasi hiyo ya ukatibu bado atabaki "MAKAMBA"Nawashauri waache kutumia cheo au jina katibu Mkuu badala yake watumibe MAKAMBA ,Makamba, Makamba wa pili.......n.k.Anaposema CHADEMA wanabeza kwao kujivua magamba na kwamba wanasema ya kua CCM inasema uongo.

Hapa anaesema uongo ni nani?Magamba gani waliyoyavua tangu kutangazwa dhana hiyo?Anakanusha na wakati huohuo kubali ya kua CCM kuna wafanyabiashara wanao kitumia chama kwa manufaa yao binafsi.Hapa nani muongo,kua na wafanyabiashara katika chama sio makosa, makosa ni kwa wafanyabiashara hao kukitumia chama kutuibia rasilimali zetu.

Anaposema ya kua CHADEMA wanambeza Baba wa taifa kwa kutembelea makaburi ya baba wa taifa Mwalimu Nyerere wakati wanatenda kinyume chake.Hapa nani anaetenda kinyume na maadili ya Baba wa taifa CCM au CHADEMA? CHADEMA kinapigania walalahoi, rasilimali za taifa na kuwakomboa walalahoi kutoka katika umasikini uliopindukia(Elimu,afya,malazi n.k)Ambao ndio ulikua msingi mkuu katika vitendo vyake.

CCM kujilimbikizia mali kwa viongozi wake na familia zao kwa kujinufaisha na rasilimali zetu na ufisadi.Ushauri wangu " CCM ikome kuitisha mikutano au maandamano na wananchi lau wakifanya hivyo waviachie vikundi vya usanii kutumbuiza kwani kwa sasa hawana cha kuwaambia wananchi,badala yake wafanye vikao vyao vya ndani na kujadili nini cha kufanya na nini cha kuwambia wananchi"

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Mtu akimwaga ugali, wewe unamwaga mboga, haya sasa tuone nani atalia zaidi!
 
Mpendazoe anawataja sasa hivi kwa faida ya nani? Mbona wakati anatoka CCM hakuwataja wenzake. Haya na aseme ni nini kuliwazuia kumfuata. Au walimpiga changa la macho, wao walitaka kuona ni nani CCM damu.
 
Mpendazoe, kada wa ccm, ccj na sasa chadema, natafuta maana ya kada
 
hilo gazeti limeona aibu kuwataja wote ni hawa hapa SITTA,MWAKYEMBE,MWaMbAlASWA,NAPE na yeye mwenyewe MPENDAZOE
 
Mapacha watatu wameshashinda vitani bado asubuhi. Hao kina Mwakyembe na Sitta wana nini kipya kwa sasa? Siasa ya bongo bwana.
 
Hayawi hayawi sasa yamekuwa, kumbe magamba mengi loooh CCM kazi wanayo mwaka huu
 
12mpendazoe.jpg




Alisema kuwa, hata Mwalimu Julius Nyerere enzi za uhai wake aliwahi kutamka kuwa, bila CCM ya kweli nchi itayumba na kwamba ndiyo maana chama hicho kimeamua kutumia dhana hiyo ya kujivua gamba ili kiweze kuwa imara na kinachoweza kusimamia maendeleo ya wananchi.



hahaha...wanajaribu kutisha wananchi?!
 
Wakati ule alibembelezwa awataje akagoma,kwa sasa ni wrong time.Ni sawa na hadithi za kufikirika.Mi namuona sawa tu huyo Nape.Je CCJ ingeandikishwa angekua CDM?

Mpendazoe aliwahi kuulizwa kama yeye ni mwanzilishi wa CCJ akasema hapana,leo anasema yeye ni miongoni mwa Wanzilishi! Hopeless kabisa!
Jibuni hoja katibu mwenezi wa CCJ Nape lini alijitoa CCJ siyo kutuletea story za zamani hapa.
 
Sitta, Mwakyembe, Nape n.k wote wanafiki tu
Tatizo la wanasiasa wa TZ ni njaa, wanapiga kelele ili wapewe ulaji. Nape alipigia kelele swala la mradi wa jengo la umoja wa vijana akapewa Ukuu wa wilaya- akafunga mdomo. Sitta na mwenzake walishikilia Richmond- wakapewa ulaji-wako kimya na leo hii wanafanya kazi na Dr. Hosea na aliyekua N/Katibu wizara ya nishati ambao walipendekeza wafukuzwe kazi.
Ni wanasiasa wachache wakuweza kuaminika.:pound:
 
Aisee sikujua kama Mpendazoe sio mtu makini kwa kiwango hiki, uchungu mwingi moyoni uliotokana na kuruka melini mapema na kisha kupotezwa na mawimbi umempunguzia busara na ufahamu.

Pole sana mpendazoe, ni ajabu sana kwa Chadema kuanza kuwataja wasaliti wa wapinzania wao CCM,eti ili CCM iwajue wale wanaowasaliti ndani yao...inatia shaka sana hii , sasa nauona kwa mbali ule ushirika usio mtakatifu kati ya mapacha watatu na chadema kama ulivyotangazwa na Nape.

Hii sio news kwa CCM, wanachotakiwa kufanya akina Sitta ni kutojibu in detail kuhusu CCJ bali kuutangazia umma kwa urefu kuhusu ushirika wa Chadema na Mafisadi katika kufanya lolote litakalosaidia kuwanusuru Mafisadi, mahakama ya umma itaamua in favour of either Wapiganaji au Chadema+Watuhumiwa wa ufisadi, usinipe jibu!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom