Mpango wa USA kumng'oa Bashar Al-Assad na madhara yake

Mpango wa USA kumng'oa Bashar Al-Assad na madhara yake

KAUMZA

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2010
Posts
699
Reaction score
241
Tangu machi 2011, nchi ya Syria imekuwa katika machafuko na hatimaye vita ambapo zaidi ya watu 100,000 wameuawa wengi wakiwa askari wa vikosi vya usalama na maafisa wa kijeshi.

Kwa sasa Syria inakabiliwa na kitisho kutoka USA, Taifa kubwa kabisa lililopanga kuipiga Syria kwa madai kuwa ameruhusu vikosi vyake vitumie silaha za sumu.

Nini yanaweza kuwa madhara ya kushambuliwa Syria na kung'olewa Rais Assad?

(i) Iwapo makundi ya magaidi wa Free Syrian Army (FSA) au Jabhat Al-nusra watafanikiwa kuchukua madaraka, dunia itegemee mauaji makubwa ya jamii za wachache wakiwemo waislamu wa madhehebu ya Shia/Alawi wanaounda 14% ya watu wote na wakristo ambao ni 10%. Ikumbukwe kuwa Assad anaungwa mkono na washia na wakristo

(ii) Iwapo Syria itashambuliwa kuna uwezekano wa kuongezeka kwa makundi ya kigaidi na kuzidi kupata nguvu makundi kama vile Alfarouq Brigade na Islamic State of Iraq

(iii) Kushambuliwa kwa Syria kunaweza kukawa ni chanzo cha vita vikuu vya 3 vya dunia. Maana wakati USA na washirika wake wa Saudia, Qatar, Israel, Uturuki na Ufaransa wamepeleka majeshi na vifaa tayari kwa mashambulizi, Urusi nayo ambaye ni mshirika mkuu wa Assad imepeleka meli zake za kivita katika bahari ya Mediterranean na Rais Putin ameapa kumsaidia Assad. Pia Iran nayo imeapa kumsaidia Assad

(iv) Kushambuliwa na kung'olewa kwa Assad kutafuatiwa na kushambuliwa Hezbollah, Hammas na hatimaye Iran. Baada ya kushambuliwa Iran na kuuvunja ukanda wa kishia (Shiites Crescent) ambao ni washirika wakuu wa Urusi, USA itakuwa tayari imeizunguka Urusi. Ikumbukwe kuwa nchi karibu zote zilizokuwa zikiunda Warsaw Pact kwa sasa zinapiga magoti kuwa wanachama wa NATO

WITO WANGU: Hima hima watanzania na wapenda amani duniani kote, tuombe Mungu aepushe vita hii
 
mpaka nywele zimenisisimka na moyo umenidunda ngoja nitulie ntarudi.
 
Nani Kama marekani Hii Dunia acha hizo U.S wana akili sana wale Jamaa kama Mungu ni Mjomba wao Assad anadundwa then lazima wakae hao Russia. na ishu ya silaha za sarin Gas unakuta FSA walipewa na America ili jus Ushaidi ionekane assad ndio alirelease na chanzo cha Kumchapa anyway its a time kustopisha vita kiivo syria na walw wakimbizi more than 2Mil.warud Home
 
Godbless America. 🇺🇸🇺🇸🇺🇸🇺🇸🇺🇸🇺🇸🌊🌊🌊
 
Tangu machi 2011, nchi ya Syria imekuwa katika machafuko na hatimaye vita ambapo zaidi ya watu 100,000 wameuawa wengi wakiwa askari wa vikosi vya usalama na maafisa wa kijeshi.

Kwa sasa Syria inakabiliwa na kitisho kutoka USA, Taifa kubwa kabisa lililopanga kuipiga Syria kwa madai kuwa ameruhusu vikosi vyake vitumie silaha za sumu.

Nini yanaweza kuwa madhara ya kushambuliwa Syria na kung'olewa Rais Assad?

(i) Iwapo makundi ya magaidi wa Free Syrian Army (FSA) au Jabhat Al-nusra watafanikiwa kuchukua madaraka, dunia itegemee mauaji makubwa ya jamii za wachache wakiwemo waislamu wa madhehebu ya Shia/Alawi wanaounda 14% ya watu wote na wakristo ambao ni 10%. Ikumbukwe kuwa Assad anaungwa mkono na washia na wakristo

(ii) Iwapo Syria itashambuliwa kuna uwezekano wa kuongezeka kwa makundi ya kigaidi na kuzidi kupata nguvu makundi kama vile Alfarouq Brigade na Islamic State of Iraq

(iii) Kushambuliwa kwa Syria kunaweza kukawa ni chanzo cha vita vikuu vya 3 vya dunia. Maana wakati USA na washirika wake wa Saudia, Qatar, Israel, Uturuki na Ufaransa wamepeleka majeshi na vifaa tayari kwa mashambulizi, Urusi nayo ambaye ni mshirika mkuu wa Assad imepeleka meli zake za kivita katika bahari ya Mediterranean na Rais Putin ameapa kumsaidia Assad. Pia Iran nayo imeapa kumsaidia Assad

(iv) Kushambuliwa na kung'olewa kwa Assad kutafuatiwa na kushambuliwa Hezbollah, Hammas na hatimaye Iran. Baada ya kushambuliwa Iran na kuuvunja ukanda wa kishia (Shiites Crescent) ambao ni washirika wakuu wa Urusi, USA itakuwa tayari imeizunguka Urusi. Ikumbukwe kuwa nchi karibu zote zilizokuwa zikiunda Warsaw Pact kwa sasa zinapiga magoti kuwa wanachama wa NATO

WITO WANGU: Hima hima watanzania na wapenda amani duniani kote, tuombe Mungu aepushe vita hii


Majority of Americans say NO to war, yet this autocratic government of America ignores the sentiment of the people. The War Machine dictates the interests of the rich - onward for profit!

Why is U.S. looking for yet one more enemy? Do you want everyone else in the world to hate you? At a time when the U.S. is on the brink of bankruptcy?
I believe there is little or no doubt that some Americans will die because of Obama's decision to carry out an attack on Syria.
Ni vyema huyu obama akawacha kitendo cha kuishambulia Syria. Faida yake sijui itakuwa inamfaidisha nani? Viongozi wa America au Waamerica wanaopinga kitendo hichi cha uvamizi.
 
Japo siungi mkono matumizi ya nguvu za kijeshi comment yangu haitabadilisha dhamira ya Marekani dhidi ya Syria...
 
Acha tu tuone wanachotaka kufanya,maana hata tuongee vipi Marekani haiwezi kubadilisha msimamo!!!!!
 
Hiii vita imekaa kimaslahi zaidi na bahati mbaya RUSSIA ameshatangaza raia wake warudi nyumbani kama alivyofanya wakati wa VITA VYA IRAQ hakafu akakaa kimyaa.......
 
Tangu machi 2011, nchi ya Syria imekuwa katika machafuko na hatimaye vita ambapo zaidi ya watu 100,000 wameuawa wengi wakiwa askari wa vikosi vya usalama na maafisa wa kijeshi.Kwa sasa Syria inakabiliwa na kitisho kutoka USA, Taifa kubwa kabisa lililopanga kuipiga Syria kwa madai kuwa ameruhusu vikosi vyake vitumie silaha za sumu.Nini yanaweza kuwa madhara ya kushambuliwa Syria na kung'olewa Rais Assad?(i) Iwapo makundi ya magaidi wa Free Syrian Army (FSA) au Jabhat Al-nusra watafanikiwa kuchukua madaraka, dunia itegemee mauaji makubwa ya jamii za wachache wakiwemo waislamu wa madhehebu ya Shia/Alawi wanaounda 14% ya watu wote na wakristo ambao ni 10%. Ikumbukwe kuwa Assad anaungwa mkono na washia na wakristo(ii) Iwapo Syria itashambuliwa kuna uwezekano wa kuongezeka kwa makundi ya kigaidi na kuzidi kupata nguvu makundi kama vile Alfarouq Brigade na Islamic State of Iraq(iii) Kushambuliwa kwa Syria kunaweza kukawa ni chanzo cha vita vikuu vya 3 vya dunia. Maana wakati USA na washirika wake wa Saudia, Qatar, Israel, Uturuki na Ufaransa wamepeleka majeshi na vifaa tayari kwa mashambulizi, Urusi nayo ambaye ni mshirika mkuu wa Assad imepeleka meli zake za kivita katika bahari ya Mediterranean na Rais Putin ameapa kumsaidia Assad. Pia Iran nayo imeapa kumsaidia Assad(iv) Kushambuliwa na kung'olewa kwa Assad kutafuatiwa na kushambuliwa Hezbollah, Hammas na hatimaye Iran. Baada ya kushambuliwa Iran na kuuvunja ukanda wa kishia (Shiites Crescent) ambao ni washirika wakuu wa Urusi, USA itakuwa tayari imeizunguka Urusi. Ikumbukwe kuwa nchi karibu zote zilizokuwa zikiunda Warsaw Pact kwa sasa zinapiga magoti kuwa wanachama wa NATOWITO WANGU: Hima hima watanzania na wapenda amani duniani kote, tuombe Mungu aepushe vita hii
Mkuu nakupa pongezi kwa uchambuzi wako makini, leo nimemsikia Asaad akitoa onyo kwa mafumbo na kuzungumzia yote uliyo taja hapo juu - reading between the lines inaonekana Merikani ikishambulia Syria wenda ikiwa Urusi inaweza kuishambulia Saudia na Qatar kulipiza kisasi - Putin aliwahi kutoa dekezo kama hilo. Juzi hapa Israel ilirusha makombola mawili ya aina ya cruise yakitokea kwenye nyambizi yao, kwa bahati nzuri RADAR za Kirusi ziliweza ku-detect makombola hayo yalipo hibuka kutoka baharini, makombola hayo yaliharibiwa/lipuliwa in flight yakielekea Syria, ina aminika hizo zilikuwa na njama za Israel za kutaka kuanzisha vita mapema na Syria. Sasa swali: Nani alilipuwa makombola hayo in flight? Inadaiwa Wamerikani ndio wali-intercept makombola hayo ili kuwadhibiti Waisrael wasianzishe vita na Syria! Je hii ni kweli? - Mwezi miwili hivi uliyo pita nyambizi ya Israel inayo fanana na hii iliyo husika na sakata hili ilizamishwa kwenye mazingira ya kutatanisha - tukiweka maanani kwamba nyambizi hizi huko nyuma zilihusika katika kurusha makombola ya cruise yaliyo haribu maghara nchini Syria ya kuhifadhia silaha za kuzamisha meli, silaha hizo niza Kirusi. Waziri mkuu wa hivi sasa huko Israel wakati akiwa ziarani Urusi aliwahi kumwambia Putin kwamba, Urusi ikiwapa Wasyria makombola ya S-300 basi Israel itayashambulia! Putin alimjibu Netanyau kwamba hasitegemee kwamba anaweza kushambulia silaha hizo bila ya kujibiwa in kind - na kweli nyambizi ya Waisrael ilizamishwa kimya kimya thereafter.
 
Bado ninawashangaa Waisrael wanaotaka kumng`oa Bashar!
 
Back
Top Bottom