Safari_ni_Safari
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 23,268
- 17,099
kwa mpango huu wa kutumia vyombo vya dola kama walivyotumia makaburu Afrika Kusini sasa natoa rai kwa upinzani tutumie mbinu zile zile walizotumia ANC kukabiliana na udhalimu huu.Tuna base support ya kutosha,tupo na umma.Tusikubali kurudi nyuma.
Na sisi tuwaonyeshe rangi halisi ya wanamageuzi baada ya wao kutuonyesha rangi halisi ya ukoloni na ukandamizaji
Tukiwaonyesha woga wetu, itakua silaha imara zaidi kwao kutumaliza
Watanzania wanataka Mabadiliko Bila kujali hayo Mabadiliko yataasaidia nini au bila kujali waleta mabadiiko ni watu wa aina gani, so hata wangefungua kesi ngapi hazitasaidia kitu chochote
CCM vs CHADEMA
Inakuja sasa mpango mpya wa kutolea kafara watu ili kujenga hoja ya kubambikiza kesi za kijasusi sheria ambayo haiwapi dhamana wala kuwatoa vifungoni hadi uchaguzi Mkuu upite, wakati tukijua sheria za kugombea vyeo kisiasa aliyekwisha onja kifungo cha muda uliowekwa kisheria haruhusiwi kugombea nafasi za uwakilishi na ukuu wa nchi. Mbaya zaidi vyombo vya dola vinapojenga mfumo wa kuegemea upande mmoja kiutendaji badala ya mfumo wa kutofungamana upande wo wote ili kutendea haki wananchi wote maana dola na vyombo vyake ni mali ya wananchi katu kisheria si miliki ya chama fulani.
Katika kile kilichoelezwa na Wasira hadharani kwamba Chadema itasambaratika katika mwaka huu, dalili za wazi zimeanza kujionyesha kwa suala la Rwekatare. Hoja za Chadema zinaonekana kuwa nzito na za kueleweka na kwa lugha inayoeleweka kwa wananchi. CCM kujenga ushawishi kwa wananchi inaelekea kugonga mwamba kwa sababu hoja zao hazionyeshi uwezo wa kuzipiku zile za Chadema. Wananchi wanapokea hoja za upende wa upinzani kutokana na hali halisi ilivyo nchini kwa sasa. Kwa mantiki hiyo CCM kinachoendelea ni kujaribu kutumia zaidi nguvu ili kuendelea kushika dola kwa nguvu badala ya ridhaa ya kidemokrasia. Hivi wajibu wa Wasira katika wizara yake sera na taratibu ni kuratibu sera na taratibu za kuangamiza demokrasia nchini?
Tangazo la Chadema la kujiimarisha kikanda linaonekana kutibua nyongo za CCM, maana kwa mfumo huo ni dhahiri mtandao wa Chadema utakuwa na nguvu ya ziada kanda zote na kuwa na nafasi ya kupenya kotekote mikoani hadi vijijini ambako CCM inajivunia kuwa hazina ya ushindi wake. CCM ilibweteka kwa hoja kwamba vyama vya upinzani ni vya msimu na havikubaliki vijijini ambako kuna wapiga kura asilimia 80. Leo mambo yamegeuka ni sera ndiyo yenye kuteka wapiga kura badala ya mazoea ya rangi ya chama.
Kauli ya Kikwete Mkutano Mkuu CCM Dodoma ni ya uchochezi?Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkutano wa CCM mjini Dodoma alitoa kauli kwamba atahakikisha kwa njia ye yote anaukabidhi urais kwa CCM si chama cha Upinzani.
Rais ni wa wananchi wote wa Tanzania bila kujali itikadi akisha shika kiti cha Ikulu ni wa wote. Waliomchagua ni watanzania wote wakiwemo CCM na vyama vingine vya siasa hali kadhalika wasio wanachama wa chama cho chote. Kauli ile kimantiki si sahihi kwa Kiongozi wa nchi, maana kwa kauli ile kwa mamlaka aliyo nayo anaweza akayatumia vibaya madaraka yake kwa sababu tu ametamka wazi kwamba atafanya kila liwezekanalo kuhakikisha urais anamwanchi mwanachama wa CCM. Kauli ile ielewekaje?
Polisi kutotenda haki usawa kwa vyama vyote vya siasa
Kashfa ya Mwigulu Mchemba Dola kutochukulia hatua stahiki
[*=1]Kashfa alizonazo Mwigulu Mchemba kuhusika kutuma gari lililojaa vijana kwenda kuvuruga mkutano wa Chadema na kusababisha kifo cha mtu mmoja huko mkoani Singida, polisi kutoa ushuhuda huo mahakamani, lakini Mwigulu Mchemba hajaitwa kutoa maelezo polisi na alitakiwa akamatwe kuunganishwa katika kesi hiyo.
[*=1]Mwigulu Mchemba katika uchochezi kwamba anazo kanda za video za Chadema kupanga mauaji hajaitwa na vyombo vya dola kutoa ufafanuzi and to release kanda hizo kama ushahidi ili vyombo vya dola vifanyie kazi.
Zuio la mikutano ya hadhara dola huthibiti upinzani tuWakati wa zuio la mikuano ya hadhara, CCM ruksa kufanya mikutano ya hadhara na hawabughudhiwi na vyombo vya dola lakini vyama vya upinzani wakati wa zuio hata mikutano ya ndani husambaratishwa hadi kusababisha majeruhi na mauaji.
Tuko la kuuawa mwanahabari wa Chanel Ten huko Iringa ni mfano dhahiri ambapo zuio la mikutano ya hadhara kwa sababu ya zoezi la kuhesabu watu wakati Chadama walikuwa na mkuano wa ndani wakati huo huo CCM ikifanya mkutano mkuwa wa hadhara huko kisiwani Unguja na mkutano mkubwa mwingine wa tamasha kwenye uwanja mojawapo huku bara lakini hawakuguswa na sheria hiyo.
Pamoja na mengi ambayo yanaelekea Chadema kushikishwa adabu kwa sheria zilezile zinazovunjwa na CCM kutoshikishwa adabu inatia shaka katika vyombo vya dola kutendea haki watanzania, vyama vya siasa ambavyo vyote vina haki sawa kikatiba na wananchi kwa ujumla. Vyama vyote vinawakilisha wananchi walewale walio chini ya dhamana ya kulindwa na vyombo vile vile vya dola.
Ushindani wa kweli ni hoja, sera na pengine hata utani
Ushindani wa kisiasa si vita, bali hoja na sera
Tujifunze kuendesha siasa za ustaarabu kwa kutumia hoja na kuuza sera kwa wananchi kwa nguvu ya hoja badala ya kuendesha siasa kwa kutumia mfumo wa hoja ya nguvu. Mambo yakielekea kukukalia vibaya bora kutulia na kuangalia wapi umeteleza, jipange upya na mkakati mpya ili kuanza kujenga ushawishi wenye kuwakuna wananchi. Chama kinachoshika dola kina nafsi zaidi ya kuonyesha utendaji wake ili kuwavutia wananchi kuliko chama ambacho kisicho shika dola kwa vile kinanadi sera bila utekelezaji. Kitanzi kwa chama chenye kushika dola ni pale kinapohangaika majukwaani kunadi sera wakati ndio watekelezaji wa sera walizozinadi kipindi cha uchaguzi.
Wapigania haki si Wanachadema bali wapenda mabadiliko ya kweli
Wapigania haki tulio wengi si wanachama wa chama fulani ila ni wapenda maendeleo na mabadiliko ya kweli kwa manufaa ya nchi bila kujali chama gani kifanikishe kuibadili Tanzania ya leo iwe tuitakavyo.
Sera ambazo zinatukuna wapigania haki na wananchi ndizo zinazofanya tupende sera hizo si chama. Ushindani wa kimaendeleo ni pale miamba miwili inaposhindana katika kujenga nchi badala ya mmoja asiye na upinzania hatakuwa na ushindani wa kweli bali kuongoza nchi kwa mazoea. Hiyo ndiyo njia nzuri ya kukuza uongozi unaojengeka kwa misingi ya kidemokrasia kwa kupinduana kwenye masanduku ya kura.
mabadiliko hata kama unatumbukia shimoni?
watu wote wanaojua kuwa dola iko kama mwavuli wa kuwafanyia wao kuendelea kuitafuna nchi hawatakaa hata siku 1 wakubali mabadiliko kirahis kama wengine tunavyofikiria inawezekana kabisa wataua watu wengi sana kwa mitindo tofauti tofauti wanaweza kukuajiri wakuuwe ukiwa mikononi mwao wanaweza kucheka nawe wakuuwe ukiwa na wengine ili watengeneze mazingira ya kuchanganya umma vyovyote vile cha msingi na cha kufahamu ni kuwa ccm si wenzetu kabisa
kwa mpango huu wa kutumia vyombo vya dola kama walivyotumia makaburu Afrika Kusini sasa natoa rai kwa upinzani tutumie mbinu zile zile walizotumia ANC kukabiliana na udhalimu huu.Tuna base support ya kutosha,tupo na umma.Tusikubali kurudi nyuma.
Na sisi tuwaonyeshe rangi halisi ya wanamageuzi baada ya wao kutuonyesha rangi halisi ya ukoloni na ukandamizaji
Tukiwaonyesha woga wetu, itakua silaha imara zaidi kwao kutumaliza
Makala imetulia. Sasa hawa ndugu zetu ccm badala ya mapenzi kwa wananchi, huku ni kubakana hadharani. hata wakitawala hatuwapendi. Kwa nini kulazimisha penzi pasipo penzi? Wanaitafuta laana. nami nauliza Lwakarare ameshtakiwa kwa uchochezi, ni yupi zaidi yeye na mwigulu au shikh igunga?
wewe ni bendera fuata upepo hata hujui unachokiandika...lwaka ni gaidi na ushahidi wa video upo, acha kuropoka
Wewe subiri ukajieleze ule unga uliutoa wapi na nani alikutuma ukamuue Zitto.
mambo yalianza kwa kumteka, kumnyanyasa na kumdhalilisha dc kule igunga
baada ya wiki moja mpiga kampeni wa ccm akamwagiwa tindikali igunga na vijana wa chdm
hamad, tukasikia dkt ulimboka kanyofolewa kucha na kuteswa
Mungu wangu, na kibanda naye baada ya kuhama chumba cha habari akatobolewa jicho
tuache siasa za jazba. tusilazimishe kila mtanzania aamini na kuikubali chadema. kila mtu ana uhuru wa kukiunga mkono chama akipendacho.
CCM vs CHADEMA
Inakuja sasa mpango mpya wa kutolea kafara watu ili kujenga hoja ya kubambikiza kesi za kijasusi sheria ambayo haiwapi dhamana wala kuwatoa vifungoni hadi uchaguzi Mkuu upite, wakati tukijua sheria za kugombea vyeo kisiasa aliyekwisha onja kifungo cha muda uliowekwa kisheria haruhusiwi kugombea nafasi za uwakilishi na ukuu wa nchi. Mbaya zaidi vyombo vya dola vinapojenga mfumo wa kuegemea upande mmoja kiutendaji badala ya mfumo wa kutofungamana upande wo wote ili kutendea haki wananchi wote maana dola na vyombo vyake ni mali ya wananchi katu kisheria si miliki ya chama fulani.
Katika kile kilichoelezwa na Wasira hadharani kwamba Chadema itasambaratika katika mwaka huu, dalili za wazi zimeanza kujionyesha kwa suala la Rwekatare. Hoja za Chadema zinaonekana kuwa nzito na za kueleweka na kwa lugha inayoeleweka kwa wananchi. CCM kujenga ushawishi kwa wananchi inaelekea kugonga mwamba kwa sababu hoja zao hazionyeshi uwezo wa kuzipiku zile za Chadema. Wananchi wanapokea hoja za upende wa upinzani kutokana na hali halisi ilivyo nchini kwa sasa. Kwa mantiki hiyo CCM kinachoendelea ni kujaribu kutumia zaidi nguvu ili kuendelea kushika dola kwa nguvu badala ya ridhaa ya kidemokrasia. Hivi wajibu wa Wasira katika wizara yake sera na taratibu ni kuratibu sera na taratibu za kuangamiza demokrasia nchini?
Tangazo la Chadema la kujiimarisha kikanda linaonekana kutibua nyongo za CCM, maana kwa mfumo huo ni dhahiri mtandao wa Chadema utakuwa na nguvu ya ziada kanda zote na kuwa na nafasi ya kupenya kotekote mikoani hadi vijijini ambako CCM inajivunia kuwa hazina ya ushindi wake. CCM ilibweteka kwa hoja kwamba vyama vya upinzani ni vya msimu na havikubaliki vijijini ambako kuna wapiga kura asilimia 80. Leo mambo yamegeuka ni sera ndiyo yenye kuteka wapiga kura badala ya mazoea ya rangi ya chama.
Kauli ya Kikwete Mkutano Mkuu CCM Dodoma ni ya uchochezi?Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkutano wa CCM mjini Dodoma alitoa kauli kwamba atahakikisha kwa njia ye yote anaukabidhi urais kwa CCM si chama cha Upinzani.
Rais ni wa wananchi wote wa Tanzania bila kujali itikadi akisha shika kiti cha Ikulu ni wa wote. Waliomchagua ni watanzania wote wakiwemo CCM na vyama vingine vya siasa hali kadhalika wasio wanachama wa chama cho chote. Kauli ile kimantiki si sahihi kwa Kiongozi wa nchi, maana kwa kauli ile kwa mamlaka aliyo nayo anaweza akayatumia vibaya madaraka yake kwa sababu tu ametamka wazi kwamba atafanya kila liwezekanalo kuhakikisha urais anamwanchi mwanachama wa CCM. Kauli ile ielewekaje?
Polisi kutotenda haki usawa kwa vyama vyote vya siasa
Kashfa ya Mwigulu Mchemba Dola kutochukulia hatua stahiki
[*=1]Kashfa alizonazo Mwigulu Mchemba kuhusika kutuma gari lililojaa vijana kwenda kuvuruga mkutano wa Chadema na kusababisha kifo cha mtu mmoja huko mkoani Singida, polisi kutoa ushuhuda huo mahakamani, lakini Mwigulu Mchemba hajaitwa kutoa maelezo polisi na alitakiwa akamatwe kuunganishwa katika kesi hiyo.
[*=1]Mwigulu Mchemba katika uchochezi kwamba anazo kanda za video za Chadema kupanga mauaji hajaitwa na vyombo vya dola kutoa ufafanuzi and to release kanda hizo kama ushahidi ili vyombo vya dola vifanyie kazi.
Zuio la mikutano ya hadhara dola huthibiti upinzani tuWakati wa zuio la mikuano ya hadhara, CCM ruksa kufanya mikutano ya hadhara na hawabughudhiwi na vyombo vya dola lakini vyama vya upinzani wakati wa zuio hata mikutano ya ndani husambaratishwa hadi kusababisha majeruhi na mauaji.
Tuko la kuuawa mwanahabari wa Chanel Ten huko Iringa ni mfano dhahiri ambapo zuio la mikutano ya hadhara kwa sababu ya zoezi la kuhesabu watu wakati Chadama walikuwa na mkuano wa ndani wakati huo huo CCM ikifanya mkutano mkuwa wa hadhara huko kisiwani Unguja na mkutano mkubwa mwingine wa tamasha kwenye uwanja mojawapo huku bara lakini hawakuguswa na sheria hiyo.
Pamoja na mengi ambayo yanaelekea Chadema kushikishwa adabu kwa sheria zilezile zinazovunjwa na CCM kutoshikishwa adabu inatia shaka katika vyombo vya dola kutendea haki watanzania, vyama vya siasa ambavyo vyote vina haki sawa kikatiba na wananchi kwa ujumla. Vyama vyote vinawakilisha wananchi walewale walio chini ya dhamana ya kulindwa na vyombo vile vile vya dola.
Ushindani wa kweli ni hoja, sera na pengine hata utani
Ushindani wa kisiasa si vita, bali hoja na sera
Tujifunze kuendesha siasa za ustaarabu kwa kutumia hoja na kuuza sera kwa wananchi kwa nguvu ya hoja badala ya kuendesha siasa kwa kutumia mfumo wa hoja ya nguvu. Mambo yakielekea kukukalia vibaya bora kutulia na kuangalia wapi umeteleza, jipange upya na mkakati mpya ili kuanza kujenga ushawishi wenye kuwakuna wananchi. Chama kinachoshika dola kina nafsi zaidi ya kuonyesha utendaji wake ili kuwavutia wananchi kuliko chama ambacho kisicho shika dola kwa vile kinanadi sera bila utekelezaji. Kitanzi kwa chama chenye kushika dola ni pale kinapohangaika majukwaani kunadi sera wakati ndio watekelezaji wa sera walizozinadi kipindi cha uchaguzi.
Wapigania haki si Wanachadema bali wapenda mabadiliko ya kweli
Wapigania haki tulio wengi si wanachama wa chama fulani ila ni wapenda maendeleo na mabadiliko ya kweli kwa manufaa ya nchi bila kujali chama gani kifanikishe kuibadili Tanzania ya leo iwe tuitakavyo.
Sera ambazo zinatukuna wapigania haki na wananchi ndizo zinazofanya tupende sera hizo si chama. Ushindani wa kimaendeleo ni pale miamba miwili inaposhindana katika kujenga nchi badala ya mmoja asiye na upinzania hatakuwa na ushindani wa kweli bali kuongoza nchi kwa mazoea. Hiyo ndiyo njia nzuri ya kukuza uongozi unaojengeka kwa misingi ya kidemokrasia kwa kupinduana kwenye masanduku ya kura.
Mambo mengine ni magumu sana kuyaamini. Lakini kama mpango huo ni wa kweli kwanini serikali iliridhia uwepo wa vyama vingi? Basi mfumo wa vyama vingi ufutwe. Maana kama ni kweli wananchi si wataogopa? Binafsi sikubaliani ni dhana hii ya kwamba kuna mipango ya kuwafunga viongozi wa upinzani. Kwasababu hata kwenye nomination ya CCM 2015 baadhi ya vigogo wa CCM ambao hawataridhika na watakayempendekeza kugombea watakimbilia kwa upinzani sasa kwanini wawatie hofu wananchi?