Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Wakati Serikali ikiwa katika mchakato wa kuhamia rasmi makao makuu ya nchi mkoani Dodoma, imeweka wazi kwamba mpango wa kulifumua upya jiji la Dar es salaam na kulifanya kuwa kitovu cha biashara sasa umeiva.
Akizungumza na wadau mbalimbali wa uwekezaji katika ujenzi jijini Dar es salaam, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, alisema mchakato wa kupanga mpango mpya wa mji 'City Master Plan' wa Dar es salaam tayari umeanza.
Alisema mpango mpya wa Mji wa Dar es salaam unatarajiwa kupatikana kabla ya Desemba mwaka huu ambapo kampuni kutoka Italia kwa kushirikiana na watanzania wanaifanyia kazi.
"Pamoja na kuhamia Dodoma ni lazima tuifumue Dar es salaam na kuifanya kuwa kitovu cha biashara kwa kuwa majengo ya kisasa yatakakuza uchumi wetu.
"Tunatarajia kutumia Dola milioni 300 kwa ajili ya kupiga picha angani kwa ndege ili kuipata Dar es salaam vizuri na kutengeneza mpango mji utakaokuwa wa kisasa "alisema Lukuvi
Pia Waziri Lukuvi aliwahamasisha wadau hao kujiandaa kuwekeza Dar es salaam na Dodoma kwa kuwa Serikali itakapohama jijini majengo yote ya Serikali yatahitaji uwekezaji
" Hii ni fursa ambayo mnatakiwa kuiangalia kwa karibu kwani kwa upande wa Dodoma kutahitajika huduma nyingi ikiwamo ya majengo ambayo yanakuwa ya makazi, ofisi na huduma nyingine za kiuchumi.
"Na wakati huo huo Serikali itakapohamia Dodoma, jijini hili litatakiwa kuwa na mwonekano wa kisiasa ili liwe na mvuto wa kibiashara na kukuza uchumi wetu "alisema Lukuvi
Pamoja na kuwahamasisha wadau hao ambao wengi ni wamiliki wa makampuni ya ujenzi, Waziri Lukuvi aliwataka kuhakikisha wanaotumia teknolojia za kisasa na kuwa na majengo yenye ubora na imara.
Chanzo :Mtanzania
Akizungumza na wadau mbalimbali wa uwekezaji katika ujenzi jijini Dar es salaam, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, alisema mchakato wa kupanga mpango mpya wa mji 'City Master Plan' wa Dar es salaam tayari umeanza.
Alisema mpango mpya wa Mji wa Dar es salaam unatarajiwa kupatikana kabla ya Desemba mwaka huu ambapo kampuni kutoka Italia kwa kushirikiana na watanzania wanaifanyia kazi.
"Pamoja na kuhamia Dodoma ni lazima tuifumue Dar es salaam na kuifanya kuwa kitovu cha biashara kwa kuwa majengo ya kisasa yatakakuza uchumi wetu.
"Tunatarajia kutumia Dola milioni 300 kwa ajili ya kupiga picha angani kwa ndege ili kuipata Dar es salaam vizuri na kutengeneza mpango mji utakaokuwa wa kisasa "alisema Lukuvi
Pia Waziri Lukuvi aliwahamasisha wadau hao kujiandaa kuwekeza Dar es salaam na Dodoma kwa kuwa Serikali itakapohama jijini majengo yote ya Serikali yatahitaji uwekezaji
" Hii ni fursa ambayo mnatakiwa kuiangalia kwa karibu kwani kwa upande wa Dodoma kutahitajika huduma nyingi ikiwamo ya majengo ambayo yanakuwa ya makazi, ofisi na huduma nyingine za kiuchumi.
"Na wakati huo huo Serikali itakapohamia Dodoma, jijini hili litatakiwa kuwa na mwonekano wa kisiasa ili liwe na mvuto wa kibiashara na kukuza uchumi wetu "alisema Lukuvi
Pamoja na kuwahamasisha wadau hao ambao wengi ni wamiliki wa makampuni ya ujenzi, Waziri Lukuvi aliwataka kuhakikisha wanaotumia teknolojia za kisasa na kuwa na majengo yenye ubora na imara.
Chanzo :Mtanzania