Tuanzia hapa… Kumekuwa na wimbi kubwa la taasisi za kijamii kuanzishwa, kuyumba hata kupelekea kufa kutokana na ukosefu wa mbinu za kutafuta fedha za kuendeshea shughuli zao au miradi yao.
Nathubutu kusema ni kukosa mbinu za kutafuta fedha kwa sababu fedhaa zipo ila tambua ili uzipate lazima uwe na mbinu pamoja na ubunifu.
Tuanzie hapa… nitaeleza baadhi ya njia ambazo taasisi inaweza kufanya na kujihakikishia uhai wake.
Nakaribisha mwenye nyama zaidi.
whatsapp /call 0759600809
private fundraising consulting
Nathubutu kusema ni kukosa mbinu za kutafuta fedha kwa sababu fedhaa zipo ila tambua ili uzipate lazima uwe na mbinu pamoja na ubunifu.
Tuanzie hapa… nitaeleza baadhi ya njia ambazo taasisi inaweza kufanya na kujihakikishia uhai wake.
- Kutafuta ufadhiri kutoka kwa mashirika ya kimataifa: Mashirika ya kimataifa yanayojihusisha na maswala ya kijamii hua yanatafuta mashirika ya ndani ya nchi kadhaa ili kufikisha huduma zao kwa kundi waliolilenga, hivyo hutoa ufadhiri kwa mashirika ya nchi kadhaa yanayojihusisha na huduma au miradi sawa na yao. Kwa kua NGO zipo nyingi inawabidi wapate NGO mahususi kwa kuweka dirisha la maombi.NGO za nchi husika zitatakiwa kutuma maombi ya ufadhili (GRANT PROPOSAL). Unaweza kuona hizi fursa kwa kufanya regular visiting kwenye websites zao.
- Kutafuta ufadhiri kutoka kwenye makampuni ya ndani ya nchi: Makampuni mengi ya ndani ya nchi huwa yana utaratibu wa kurudisha fadhira kwa jamii kutokana na kutumia huduma zao au bidhaa zao, hivyo inakupasa kujua kampuni husika inapendelea kufadhiri miradi ya aina gani kisha kama NGO yako inafanya miradi sawa na matakwa ya kampuni hiyo basi unapoomba huu ufadhili ni rahisi kupata. Mfano Millicom Tanzania wamekua wakifadhili miradi ya uchimbaji wa visima karibia kila mwaka.. mifano ni mingi sana.. Chakutambua kuwa huku pia wanahitaji proposal yako ya kishindani.
- Michango kutoka kwa taasisi za ndani: Ikiwa NGO yako imedhamilia kutekeleza mradi au huduma ya kijamii ndani ya jamii ya eneo furani, si jambo mbaya kuhusisha taasisi mbalimbali za eneo hilo ili kupata msaada Zaidi juu ya changamoto mlizonazo taasisi hizo inaweza kuwa kanisa, msikiti, vikundi vya kijamii, n.k.
- Mfadhiri binafsi: Inaweza kuwa shirika, kampuni au mtu binafsi ambapo mtamwona anaharakati za kijamii basi kama NGO mkithibitisha hilo sasa manapanga mbinu za kumshawishi kufadhili taasisi yako/yenu hili linachukua muda sana ila linapofanikiwa huwa linamanufaa sana kwa sababu taasisi inakuwa na uwakika wa fedha kila mwaka kutoka kwa huyu mfadhili. Moja ya mbinu ya kushawishi ni kumtaka kuwa mlezi au rafiki wa taasisi kwa kumtumia barua ya mwaliko na kuomba meetings za mara kwa mara.
- Kutumia kampeni: Njia hii ya kutafuta fedha kwa ajiri ya miradi, kuendesha taasisi au kununua asset inahusisha kampeni maalumu ambayo ndani yake kunakuwa na mkusanyiko wa matukio, ,matukio hayo ndio haswa yanayochangisha fedha mfano michezo ya riadha,mpira wa miguu, muziki, bonanza, n.k. Kampeni hizi zinaweza kufanyika kila mwaka (annual appeal campaign) au mara moja baada ya kipindi cha miaka kadhaa (capital campaign). fedha itatoka kwa sponsors, participants na attendees.
Nakaribisha mwenye nyama zaidi.
whatsapp /call 0759600809
private fundraising consulting