Utd fans tunasumbuliwa na winning mentality na kelele+matusi kutoka kwa wapinzani. Tunataka kocha aje alete miujiza kwa muda mfupi kama Mourinho bila kujua kuwa hao huwa hawadumu zaidi ya misimu 5 kwenye timu zao. Guardiola kakaa muda gani barca, Hyneckes muda gani bayern, Mourinho chelsea, inter na real au Benitez na Pelegrini valencia na wengineo. Mpira ni utamaduni kwa kila timu kama ilivyo mfumo wa kisiasa kwa kila nchi. Utd utamaduni wetu ni kuwa na kocha atakayekaa na timu miaka zaidi ya 10, atakayetengeneza timu yake kwa kwa kutumia mix ya wachezaji wakubwa wachache na watoto kwa wingi, Ndio maana Januzaj anacheza mechi zote leo na Pogba ametangazwa kusajiliwa. Babu kastaafu mwili lakini falsafa yake bado ipo na ndio inatumika. Msimu ujao tutarajie watoto wengi kutoka kikosi B na wazoefu wachache kutoka timu za nje na baadhi waliopo. Misimu 2/3 baada ya hapo ndio tumpime DM tutoe maamuzi.....
Kwa timu ya sasa hata angekuwa Mourinho kapewa utd hii angekuwa na matokeo haya haya tunayoyaona, kila mtu ana mbinu zake za ufundishaji, aina ya wachezaji na falsafa. Kabla ya Mourinho Obi Mikel, Mata Na A. Cole walikuwa tegemeo first eleven chelsea lakini now wanaanzia benchi, na bado Mourinho anakwambia timu haijakaa anavyotaka........ DM ni mtu sahihi, hata Liverpool walimpa muda Rodgers leo wako tunavyowaona, huyu ni kocha ambaye atakaa muda mrefu pale. Martinez kaichukua Everton na anafanya vizuri lakini ameondoka Aston Villa kama sikosei baada ya kutangaziwa dau Everton, Utd na Liverpool hawachukui makocha ambao wakitangaziwa dau kwingine wanakimbia na kuondoka na kuiacha timu ijengwe tena upya na kocha mpya.