Moto wazuka Hosteli za Mabibo

Moto wazuka Hosteli za Mabibo

Poleni Kwa Tukio Hilo, Pia Mwenye Taarifa Rasmi Hadi Sasa Atujuze Kuhusu Madhara Yaliyotokea Kwa Ujumla.
 
kama sio heater basi jiko,maana wanawake kwa kupika room hatujambo
Itakuwa heater au pasi kutokana na muda wa tukio lilivyokuwa reported! Unakuta mtu ndo vile anataka kuwahi daladala, jana yenyewe ni weekend si ajabu hakulala hostel... anachukua pasi, fasta fasta... huku anakunywa chai huku ananyoosha baada ya hapo anatupia, huyooo... pasi kaiacha on!
 
Pole kwa waathirika. Kuna mdogo wangu hapo ananiambia amenusurika kuungua.
 
hayo ndo matokeo ya mitaala mibovu ya elimu ya bongo haizalishi heroes jengo linaungua afu vijana wameshika viuno wanaangalia kama muvi ya anold

Mkuu kweli kabisa. Halafu nnavyokumbuka kuna fire extinguishers , smoke detector pamoja na mipira ya kuzima moto kila ghorofa. Ndo tuseme hakuna anaejua kutumia vitu hivyo?
 
Mkuu kweli kabisa. Halafu nnavyokumbuka kuna fire extinguishers , smoke detector pamoja na mipira ya kuzima moto kila ghorofa. Ndo tuseme hakuna anaejua kutumia vitu hivyo?
Ndugu hivyo vitu inawezekana kweli vipo ,je smoke detectors zinafanya kazi?Huwa kuna utaratibu wa kuzitest?Je fire extinguisher zina gas na zinafanyiwa services?Na je wanafunzi wanafundishwa jinsi ya kutumia hizo fire extinguisher?Hiyo mipira ya kuzimia maji ,je wanajua sehemu ya kuyafungua hayo maji.So usije kuta vitu vipo ila havifanyi kazi au hakuna aliyefundishwa jinsi ya kutumia incase kuna moto.
 
hayo ndo matokeo ya mitaala mibovu ya elimu ya bongo haizalishi heroes jengo linaungua afu vijana wameshika viuno wanaangalia kama muvi ya anold

Elimu yetu imekaa kinadharia zaidi,mtu anasoma mambo ya ''CLASSESS OF FIRE'' kwenye Chemistry tangu kidato cha kwanza,lakini hawezi kutumia fire extinguisher,ni aibu kuwa na Elimu za kwenye vyeti zaidi badala ya vitendo.
 
Yani hao wanafunzi wa mabibo hostel wako busy kupiga picha badala ya kutoa msaada.
Kupiga picha kwenye matukio ndo habar ya mujini cku hiz watu wakiona ajali au tukio lolote wanapiga picha kwanza wanatuma whatsup ndo wanaanza kutoa msaada
 
VIP wamefanikiwa kuzima moto na Hilo zima moto huwaga kaz yake nn mbona kila tukio wanachelewa tu
 
Wananchi na wanachuo wanaonekana kushangaa na kuchukua picha badala ya jitihada za kuzima moto...Watoto hawa wapewe walau kaelimu kidogo juu ya fire fighting & drills...
 
Wananchi na wanachuo wanaonekana kushangaa na kuchukua picha badala ya jitihada za kuzima moto...Watoto hawa wapewe walau kaelimu kidogo juu ya fire fighting & drills...

Wengi wao wana mafunzo ya kijeshi (jkt), ni wakakamavu haswaa....

Nadhan protocol huwa hazielewek kwa wengi. Hapo watu wanasubir amri ili wazime moto
 
Ni mambo ya ajabu Sana chuo kikuu kama udsm kukosa gari hapo hostel standby kwakuzima moto.
 
Na hii tabia ya kuanza kuchukua picha na video wakati wa matukio ya ajali badala ya kutoa msaada ni ya kipuuzi kabisa.
 
Inasemekana chanzo cha moto ni grupu la wadada saba waliokua wanasheherekea bethdei ya mwenzao na kuwasha mishumaa iliyomwagika na kushika godoro.
 
Back
Top Bottom