Power G
JF-Expert Member
- Apr 20, 2011
- 3,886
- 1,193
Moto mkubwa ulioanza alfajiri umeteketeza kabisa majengo mawili la Accounts na Store hapa chuo cha usafirishaji NIT Dar-es-salaam. Mpaka sasa chanzo hakijajulikana ingawa kuna kaharufu harufu kidogo ka hujuma kwa ajili ya kuficha madhambi yalikuwapo hapo chuoni kabla ya kuingia mkuu mpya aliyekuja wiki hii. Zimamoto kama kawaida walifika wakajitahidi mpaka maji yakawaishia haukuzimika, wakaenda kuchukua mengine mpaka jengo yakateketea kabisaaa.